Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Wakati Rais akiwa katika kampeni aliahidi kuwa ataondoa ushuru na kodi ndogo ndogo zinazoleta usumbufu kwa wajasiriamali wadogo wadogo kama vile machinga, wachuuzi wa mboga mboga na matunda, mama lishe, waendesha bodaboda na kadhalika, lakini mpaka sasa ahadi hiyo haijatekelezwa. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kw amajibu mazuri. Pamoja na majibu mazuri hayo napenda kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika utekelezaji huu bado kuna maeneo mbalimbali katika Halmashauri mbalimbali katika Mkoa wangu wa Ruvuma na maeneo mengine kwenye Halmashauri nyingine maeneo mbalimbali ya nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali ina mpango gani wa kuwachukulia hatua kali halmashauri ambazo bado wanawanyonya kwa kuwatoza ushuru wajasiriamali wadogo wadogo wote katika Halmashauri zote zilizoko mkoani Ruvuma na maeneo mengine? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa wafanyabiashara hao wadogo wadogo wanafanya biashara katika mazingira magumu sana jua la kwao, mvua ya kwao, vumbi lao. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawekea mazingira bora ili wamachinga hao waweze kuepuka adha hiyo wanayoipata? (Makofi

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi sote ni mashuhuda kwamba, Sheria hii ilipitishwa na Bunge lako Tukufu na kwa vyovyote vile hakuna kisingizio chochote ambacho kinaweza kikatolewa na halmashauri eti kwa sababu, wakidhani kwamba, sheria ndogo ambazo wao hawajazipitisha zinakuwa zinakinzana kwamba hazitawaletea mapato. Naomba niwasihi Wakurugenzi wote Halmashauri zote, na jambo hili hata Mheshimiwa Rais amekuwa akilirudia, naomba niliseme kwa mara ya mwisho; Mkurugenzi yeyote wa halmashauri iwayo yoyote ambaye atapingana na maelekezo haya na sheria aambayo imetungwa na Bunge lako Tukufu, sisi kama Serikali hatutasita kumchukulia hatua. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili anaulizia namna ya kuwawekea mazingira mazuri wafanyabiashara wadogo wadogo. Ni dhamira ya Serikali na ndio maana tunaanza kwa kuwatambua kwa kuwapa vitambulisho ili tuhakikishe kwamba, wanatengewa maeneo mazuri ili wafanye kazi katika mazingira yaliyo mazuri kwa ajili ya kuongeza kipato cha nchi.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Wakati Rais akiwa katika kampeni aliahidi kuwa ataondoa ushuru na kodi ndogo ndogo zinazoleta usumbufu kwa wajasiriamali wadogo wadogo kama vile machinga, wachuuzi wa mboga mboga na matunda, mama lishe, waendesha bodaboda na kadhalika, lakini mpaka sasa ahadi hiyo haijatekelezwa. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Pamoja na majibu yanayoridhisha ya Mheshimiwa Naibu Waziri, mimi nilikuwa tu nataka niweke msisitizo kwenye hili jambo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kwamba, Mheshimiwa Rais amekuwa akirudia na wewe leo hapo umejaribu kuweka msisitizo, lakini bado kuna shida kule chini kwa Wakurugenzi wa Halmashauri kukataa hili agizo kwa maana circular bado haijafika.
Sasa nataka nijue tu kabisa kwamba, je, circular hiyo inahusu ile mizigo ya wakulima ama wananchi wa kawaida wenye chini ya tani moja, kama Rais alivyoagiza kwamba ukisafirisha mzigo kutoka eneo moja kwenda lingine, chini ya tani moja hutakiwi kulipa ushuru; kwa hiyo, nilitaka nijue kama circular na yenyewe inazungumzia hivyo? Ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimetangulia katika jibu langu la msingi kwamba tozo hizi ziliondolewa ndani ya Bunge lako Tukufu na ndani ya Bunge hili tulisema ni tozo zipi ambazo zinafutwa kwa sababu ni kodi kero. Hakuna by-law yoyote kwenye halmashauri ambayo inazidi Sheria ambayo inatungwa na Bunge lako Tukufu. Kwa hiyo, nazidi kuomba na nawasihi wakurugenzi wote hawana option nyingine zaidi ya kutekeleza Sheria ambayo imepitishwa na Bunge lako Tukufu.

Name

Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Wakati Rais akiwa katika kampeni aliahidi kuwa ataondoa ushuru na kodi ndogo ndogo zinazoleta usumbufu kwa wajasiriamali wadogo wadogo kama vile machinga, wachuuzi wa mboga mboga na matunda, mama lishe, waendesha bodaboda na kadhalika, lakini mpaka sasa ahadi hiyo haijatekelezwa. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Bunge lililopita tulitunga sheria ya kufuta hotel levy, lakini katika Mkoa wa Dar-es-Salaam hotel levy imeendelea kutozwa. Na Mheshimiwa Waziri anakiri na kusema kwamba, Sheria za Bunge zinazotungwa ziheshimiwe. Nini kauli ya Waziri?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, ile Sheria ya Hotel Levy inajieleza, ukiisoma vizuri kuna definition ya hoteli, inatakiwa iwe na sifa ipi ili ikidhi kuwa hoteli. Sasa kumekuwa na mchanganyiko kati ya hoteli na guest house. Ukiisoma Sheria ya Hotel Levy inaelekeza wale ambao ni VAT registered hawatakiwi kutoa hotel levy, lakini wale ambao wako chini ya Halmashauri bado sheria imesimama. Kwa hiyo, ni suala tu la kusoma sheria vizuri na kuitafsiri vile inavyotakiwa.

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nilikuwa napenda tu kutoa msisitizo kuhusiana na masuala yale ya kutoza ushuru. Nilikuwa naomba Halmashauri kwa kuwa, zenyewe ndio zinazoweka maeneo ya vizuizi na kukagua juu ya masuala ya kutoza ushuru ni vema sasa kuwe na mizani ambayo itawezesha hawa wananchi kuona kwamba mzigo wao una hiyo tani moja iliyoruhusiwa au la. Kinyume na hapo kwa kuangalia tu magunia kwa upande mmoja inakuwa inawafanya aidha wananchi wananyanyasika au wenyewe Halmashauri kutokupata ushuru ulio sahihi.