Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 84 2017-11-15

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:-
Wakati Rais akiwa katika kampeni aliahidi kuwa ataondoa ushuru na kodi ndogo ndogo zinazoleta usumbufu kwa wajasiriamali wadogo wadogo kama vile machinga, wachuuzi wa mboga mboga na matunda, mama lishe, waendesha bodaboda na kadhalika, lakini mpaka sasa ahadi hiyo haijatekelezwa. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani Msongozi, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imefanya uamuzi wa kufuta ushuru unaotozwa kwa wafanyabiashara ndogo ndogo wasio rasmi na wanaofanyia biashara katika maeneo yasiyo rasmi wakiwemo mama lishe, wauzaji mitumba wadogo, wauza mboga mboga, ndizi na matunda. Vile vile, wafanyabiashara walio nje ya maeneo maalum ya kibiashara wenye mitaji chini ya shilingi 100,000 hawaruhusiwi kulipa ada, tozo na kodi za aina yoyote.
Mheshimiwa MWenyekiti, uamuzi huu umeanza kutekelezwa kuanzia tarehe 1 Julai 2017 baada ya marekebisho ya Sheria ya Fedha ya mwaka 2017 iliyotangaza kufuta ushuru na kodi kero kwa wafanyabiashara wadogo wadogo. Hatua inayoendelea sasa hivi nikuwatambua wafanyabiashara wadogo wote ili kuwapatia vitambulisho maalum vya kazi wanazozifanya. Hivyo, Serikali imetekeleza kwa vitendo ahadi hii iliyoko katika Ilani ya Chama Tawala ya mwaka 2015 inayolenga kuwapatia unafuu wa maisha wananchi wa hali ya chini kiuchumi ili waweze kukua na kuchangia vizuri katika uchumi wa Taifa lao. (Makofi)