Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. MOHAMED MCHENGERWA) aliuliza:- Ni takribani miaka miwli sasa Serikali imeshindwa kuwahakikishia wananchi wa Jimbo la Rufiji kuwa na umeme wa uhakika kufuatia hitilafu ya mara kwa mara kwenye mitambo ya umeme unaozalishwa na gesi kutoka Kilwa. Je, ni lini Serikali itawaunganisha wananchi wa Rufiji, Kibiti na Kilwa kwenye Gridi ya Taifa?

Supplementary Question 1

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa watu wa Rufiji na sehemu nyingine ambapo gesi hiyo itapita ni watu ambao wanasubiria kwa hamu jambo hilo. Bado hawajapata elimu ya kutosha kujua umuhimu wa jambo hilo kwenye maeneo yao. Sasa Serikali itakuwa tayari kupita kutoa elimu ya kutosha, hasa mashuleni, ili wananchi kazi hiyo itakapoanza ya kupitisha gesi waone kwamba ile ni rasilimali yao?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa wananchi sasa walio wengi wanategemea gesi ikianza kutoka kwa wingi na tumepewa taarifa kwamba, kuna gesi ambayo inaweza ikatumika kwenye magari. Anatuambiaje Mheshimiwa tujue kwamba unafuu wa kutumia gesi ama petroli kutakuwa kuna tofauti kubwa?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Mwamoto kwa kuuliza swali kwa niaba ya Mheshimiwa Mbunge wa Rufiji na Waheshimiwa Wabunge hawa wanafanya kazi nzuri sana kwenye majimbo yao. Ni matarajio yao kwamba wananchi wanawasikia vema.
Mheshimiwa Spika, elimu ambayo tumetoa mpaka sasa, nitoe tu taarifa kwa Mheshimiwa Mbunge wa Rufiji na Mheshimiwa Mwamoto, tumeshatoa elimu katika vijiji vya Mwaseni, vijiji vya Ngarambe, kijiji cha Korongo pamoja na Kotongo, lakini tunakwenda sasa kutoa mwezi wa 10 na wa 11 elimu katika maeneo ya Jaribu Magharibi na maeneo mbalimbali. Kwa hiyo, tutaendelea kutoa elimu kwa ajili ya manufaa ya miradi hii ili wananchi wa Rufiji nzima waweze kuipata kwa hiyo, tunaendelea na utaratibu wa elimu kama kawaida.
Mheshimiwa Spika, suala la pili kuhusiana na gesi kwenye magari, ni kweli kabisa ule mradi wa kutengeneza gesi kwa ajili ya matumizi ya kwenye magari na majumbani ulishaanza tangu mwaka 2016 na hivi sasa mwakani mradi huo utaendelea. Tulishaanza katika Vituo viwili vya DIT pamoja na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na mpaka sasa magari 16 yameshaunganishwa kwa kutumia gesi badala ya petroli. Na unafuu wake ni kwamba, unapunguza asilimia 40 ya matumizi ya kawaida ya petroli unapotumia gesi.
Mheshimiwa Spika, mradi huu kwa niaba ya Watanzania wote, utaanza mwaka 2018 hadi 2020 kwa kwenda katika Mkoa wa Dar es Salaam, Mtwara pamoja na Lindi.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. MOHAMED MCHENGERWA) aliuliza:- Ni takribani miaka miwli sasa Serikali imeshindwa kuwahakikishia wananchi wa Jimbo la Rufiji kuwa na umeme wa uhakika kufuatia hitilafu ya mara kwa mara kwenye mitambo ya umeme unaozalishwa na gesi kutoka Kilwa. Je, ni lini Serikali itawaunganisha wananchi wa Rufiji, Kibiti na Kilwa kwenye Gridi ya Taifa?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika,ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kutokana na kuharibikaharibika kwa mara kwa mara kwa kinu cha gesi pale Kilwa na kutokana na uchakavu wa mitambo ile, hitajio la Wilaya za Kilwa, Lindi pamoja na Liwale, I mean Kilwa pamoja na Rufiji pamoja na Liwale kuingizwa kwenye Gridi ya Taifa ni muhimu sana.
Mheshimiwa Spika, sasa naomba Waziri atueleze hapa ni nini kinachelewesha wilaya hizi kuongizwa kwenye Gridi ya Taifa kwa sababu ya uchakavu wa mitambo ya Kilwa kunafanya umeme usiwe wa uhakika katika Wilaya hizi tatu? Ahsante sana.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa maeneo ya Kilwa, Rufiji na maeneo ya Mkuranga hivi sasa hayapati umeme wa gridi na maeneo mengine ya karibu na pale, lakini hatua zinazofanyika sasa hivi tunajenga mradi wakusafirisha umeme kutoka Somangafungu ambao nimeutaja, lakini kutakuwa na Mradi wa Rufiji Stiegler’s Gorge ambao unaanza Disemba mwaka huu. Kwa hiyo, kinachochelewesha ni maandalizi ya ujenzi kabambe wa miradi mahususi ambayo itaunganisha wananchi wa maeneo yale na Gridi ya Taifa.
Mheshimiwa Spika, Mradi wa Stiegler’s Gorge na huu niliosema ambao ni wa kusafirisha umeme wa kutoka Somangafungu kupita Kinyerezi mpaka Dar es Salaam ndio pia, utawapatia nguvu ya kutosha ya umeme na kuunganisha kwenye Gridi ya Taifa, maeneo yote ya Rufiji, Kilwa pamoja na Mkoa wa Mtwara pamoja na Lindi. Kwahiyo, wananchi wa mikoa hii miwili niwahakikishie kwamba, ifikapo mwaka 2019/2020 tayari watakuwa wameshaunganishwa na Grid ya Taifa.