Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 83 2017-09-13

Name

Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. MOHAMED MCHENGERWA) aliuliza:-
Ni takribani miaka miwli sasa Serikali imeshindwa kuwahakikishia wananchi wa Jimbo la Rufiji kuwa na umeme wa uhakika kufuatia hitilafu ya mara kwa mara kwenye mitambo ya umeme unaozalishwa na gesi kutoka Kilwa.
Je, ni lini Serikali itawaunganisha wananchi wa Rufiji, Kibiti na Kilwa kwenye Gridi ya Taifa?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omary Mohamed Mchengerwa, Mbunge wa Rufiji, lililoulizwa kwa niaba yake na Mheshimiwa Mbunge maarufu sana wa Kihesa Mgagao, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kilwa, Rifiji pamoja na Kibiti zimeunganishwa katika Gridi ya Taifa kupitia utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Somangafungu, Lindi hadi Kinyerezi, Dar es Salaam. Ujenzi wa mradi huu utaanza mwezi Julai, 2018 na utakamilika mwaka 2019/2020.
Mheshimiwa Spika, kazi za ujenzi wa mradi huu zinahusisha ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 400 yenye urefu wa kilometa 198 kutoka Somangafungu, Lindi hadi Kinyerezi, Dar es Salaam. Lakini pia, kujenga Kituo cha Kupoza Umeme, lakini pamoja na mambo mengine mradi huu utaunganisha wateja mbalimbali na kusafirisha umeme utakaozalishwa kutoka Kituo cha Somangafungu chenye uwezo wa kuzalisha megawati 240. Mradi utafadhiliwa na Kampuni ya Sumitomo ya Japan kwa gharama ya dola za Marekani milioni 340.