Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA (K. n. y MHE. HAROON M. PIRMOHAMED) aliuliza:- Mji Mdogo wa Rujewa ni kitovu cha shughuli za biashara na Makao Makuu ya Wilaya ya Mbarali na kwa bahati mbaya barabara nyingi za mji huo hazipitiki kutokana na ubovu. Wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2015 Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliahidi kujenga kilometa tano za barabara kwa kiwango cha lami. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo kwa wananchi wa Mbarali?

Supplementary Question 1

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana vilevile nishukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna kazi zilizokuwa zinaendelea zilizokuwa zinafanywa na Halmashauri na hizo zimehamishiwa kwenye TARURA sasa hivi. Je, ni lini TARURA wataanza na kuendeleza hizo kazi?
Swali la pili, kama ilivyo katika Mji Mdogo wa Rujewa vilevile Mheshimiwa Rais aliahidi kumalizia ujenzi wa kituo cha mabasi cha Mbalizi katika Mji Mdogo wa Mbalizi.
Je, ni lini kazi hiyo ya kujenga kituo cha mabasi cha Mji Mdogo wa Mbalizi kitaanza? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tumekuwa na kipindi cha mpito ambapo kazi za ujenzi wa barabara katika Halmashauri zilikuwa zikisimamiwa ndani ya Halmashauri zetu, lakini chini ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Sasa hivi tumeunda Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini ambao unaitwa TARURA sasa umeshaanza kuchukua majukumu hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, tunafahamu wazi kwamba kulikuwa na mikataba mingine na kazi mbalimbali zilikuwa zinaendelea na tulitoa maelekezo katika ofisi yetu kwamba zile kazi zote kutokana na mikataba iliyokuwa inaendelea ambazo ziliingiliwa na Halmashauri kazi zile zilipaswa kuendelea, isipokuwa taratibu za malipo ndio zilikuwa zinafanyiwa utaratibu maalum. Tulitoa maelekezo haya kwa Mameneja wa TARURA katika nchi nzima katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hata hivyo, wakati mwingine kulikuwa na uelewa tofauti katika baadhi ya maeneo, baadhi ya maeneo kazi zilikuwa zinaendelea vizuri lakini sehemu zingine kazi zilisimama, kazi kubwa iliyofanyika ni kuhamisha zile akaunti ziweze kufanya kazi vizuri ili utaratibu uendelee kufanyika kama ilivyokusudiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na concern yako Mheshimiwa Oran naomba niiagize Halmashauri yako Meneja kama kuna changamoto ambayo ameipata katika ofisi yake tuwasiliane na ofisi na hasa na Mtendaji Mkuu wa TARURA ampe maelekezo ya kutosha nini kifanyike, ili kazi kule site isiendelee kukwama, ziendelee kufanyika.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala zima la ujenzi wa stendi hii ya Mbarali, naomba nilichukue hili halafu nijue kwamba kuna kitu gani kilichokubaliwa na imefikia hatua gani? Changamoto iko wapi? Hili naomba niwahakikishie ofisi yangu itasimamia kwa sababu ahadi ya Mheshimiwa Rais lazima itekelezwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nilichukue jambo hili tutaenda kulifanyia kazi haraka iwezekanavyo, kuangalia nini tufanye ili kuhakikisha ile stendi inatengenezwa.(Makofi)

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA (K. n. y MHE. HAROON M. PIRMOHAMED) aliuliza:- Mji Mdogo wa Rujewa ni kitovu cha shughuli za biashara na Makao Makuu ya Wilaya ya Mbarali na kwa bahati mbaya barabara nyingi za mji huo hazipitiki kutokana na ubovu. Wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2015 Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliahidi kujenga kilometa tano za barabara kwa kiwango cha lami. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo kwa wananchi wa Mbarali?

Supplementary Question 2

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, TARURA imepokea kazi hizi za barabara katika Halmashauri zetu, sasa katika masuala haya ya barabara katika Halmashauri tulikuwa tunakarabati barabara hata katikati ya msimu, inaweza ikatokea mvua nyingi ikasomba barabara, Halmashauri ikatoa lori, wananchi wanashiriki kujenga ile barabara.
Je, katika kipindi hiki cha TARURA, wataendelea kufanya hiyo Kazi? Kwa sababu sasa TARURA haina malori, Halmashauri ina malori haina mafungu ya barabara, lakini TARURA wana mafungu hawana malori. Hapa huu utaratibu wa kurekebisha hizi barabara utakuwaje? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, hili jambo wala kwanza halina mashaka, kwa sababu jukumu hili sasa liko chini ya TARURA. Lakini ufahamu siyo Halmashauri yako peke yake, kuna Halmashauri mbalimbali wengine wana greda. Nafahamu magreda haya au malori haya sio kwamba yatakuwa yanafanya kazi peke yake lakini inawezekana ni kitega uchumi cha kwenu ninyi kama Halmashauri. Wakati TARURA inafanya kazi yake, wakati inatekeleza kupitia Meneja wa TARURA katika ngazi husika lazima kama utaratibu wa kukodi malori utafanywa katika utaratibu ule usiokuwa na kikwazo. Kwa hiyo, kama mna malori yenu, mna magreda yenu ambayo nanyi ni sehemu ya kitega uchumi kwenu barabara zitakapokuwa zinajengwa katika maeneo yale kama mtakuwa na utaratibu wa kukodisha jukumu kubwa ni kwamba TARURA itemize wakibu wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Mwalongo naomba usihofu kila kitu kitaenda vizuri, ni kipindi cha mpito tu kina mashaka kwa sababu ni jambo jipya lakini jambo hili litakuwa halina matatizo ya aina yoyote, tutafika muda mtaona kila kinaenda vizuri katika Halmashauri zetu.

Name

Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA (K. n. y MHE. HAROON M. PIRMOHAMED) aliuliza:- Mji Mdogo wa Rujewa ni kitovu cha shughuli za biashara na Makao Makuu ya Wilaya ya Mbarali na kwa bahati mbaya barabara nyingi za mji huo hazipitiki kutokana na ubovu. Wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2015 Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliahidi kujenga kilometa tano za barabara kwa kiwango cha lami. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo kwa wananchi wa Mbarali?

Supplementary Question 3

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la miundombinu ya barabara katika Mji Mdogo wa Rujewa linafanana kabisa na ubovu wa miundombinu ya barabara katika Mji Mdogo wa Mloo, Jimbo la Mbozi.
Je, nini ahadi ya Mheshimiwa Waziri kwa wananchi wa Mloo kuhusu miundombinu mibovu ya barabara ambayo ni tatizo la muda mrefu sana?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Haonga unapozungumza suala la Mloo nafahamu kwamba changamoto kubwa ya Wabunge wengi humu ni suala zima la miundombinu ya barabara katika Halmashauri zetu. Ndiyo maana nawashukuru sana katika Mpango ule wa bajeti mwaka huu mmeona tumetenga bajeti kubwa karibuni ya shilingi bilioni 263. Lengo kubwa ni kwamba barabara za vijijini zenye vikwazo na zile barabara nyingine tuweze kuzihudumia.
Kwa hiyo, naomba niseme kwamba katika eneo la kwako ulilozungumza na kwa sababu tumeshawaajiri watu tena tunawapa performance contract ya jinsi gani kila meneja katika Halmashauri anapoenda kule afanye kazi yake na tutaipima na meneja atakaposhindwa ku-deliver maana yake hatokuwa na hiyo nafasi atapewa mtu mwingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba ondoa hofu ni kwamba tutakuwa katika mkakati wa kutofanya kazi tena kimazoea katika utaratibu wa sasa, na kwa sababu jambo hili liliahidiwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi lazima tuwe na TARURA tutaenda kutekeleza kwa nguvu zote, naomba ondoa hofu katika eneo la Mloo tutalifanyia kazi haraka iwezekanavyo. (Makofi)

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA (K. n. y MHE. HAROON M. PIRMOHAMED) aliuliza:- Mji Mdogo wa Rujewa ni kitovu cha shughuli za biashara na Makao Makuu ya Wilaya ya Mbarali na kwa bahati mbaya barabara nyingi za mji huo hazipitiki kutokana na ubovu. Wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2015 Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliahidi kujenga kilometa tano za barabara kwa kiwango cha lami. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo kwa wananchi wa Mbarali?

Supplementary Question 4

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Wakati wa kampeni Mheshimiwa Rais alitembelea Namanyere na akatoa ahadi kwamba akipita tutapata kilometa tano za barabara ya lami. Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo amekuwa akilisema mara kwa mara lakini mpaka sasa halijatekelezwa.
Nataka kujua Serikali ina mpango gani kutekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli na hata nilipotembelea Namanyere Mheshimiwa Keissy alizungumza katika mkutano nilipokuwa ninaongea na Watumishi kuhusu ahadi hiyo sambamba na ahadi ya maji ambapo bwawa lilikuwa linaendelea kujengwa.
Mheshimiwa Mipata kwa sababu nafahamu pale Namanyere ndiyo Makao yenu Makuu ya Mji kwa ahadi hii ya Serikali na sisi ametupa dhamana kuhudumu katika ofisi yake, tutafanya kila liwezekanalo katika kipindi hiki cha miaka mitano, ahadi ya Mheshimiwa Rais kupitia TARURA tutaitekeleza, tutakapofika mwaka 2020 tusiwe na changamoto nyingine yoyote katika suala la hiyo kilometa tano Mheshimiwa Rais alizoziahidi. (Makofi)