Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 54 2017-09-11

Name

Haroon Mulla Pirmohamed

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA (K. n. y MHE. HAROON M. PIRMOHAMED) aliuliza:-
Mji Mdogo wa Rujewa ni kitovu cha shughuli za biashara na Makao Makuu ya Wilaya ya Mbarali na kwa bahati mbaya barabara nyingi za mji huo hazipitiki kutokana na ubovu. Wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2015 Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliahidi kujenga kilometa tano za barabara kwa kiwango cha lami.
Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo kwa wananchi wa Mbarali?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Haroon Mulla Pirmohamed, Mbunge wa Mbarali, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2016/2017, Halmashauri Wilaya ya Mbarali iliidhinishiwa na kupokea shilingi milioni 793.02 kwa ajili ya matengenezo ya barabara kilomita 20, kalavati kubwa 17 na matengenezo ya madaraja matano. Serikali itafanya kila liwezekanalo ili ahadi hiyo ya Mheshimiwa Rais iweze kutekelezwa ndani ya miaka mitano ya utekelezaji wa Ilani. Halmashauri imepanga kuweka kipaumbele na kutenga bajeti katika mwaka wa fedha 2018/2019 ili kuanza utekelezaji wa ahadi ya kujenga kilometa tano za barabara kwa kiwango cha lami kwa usimamizi wa Wakala wa Barabara Vijijini na Mjini (TARURA).