Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:- Walimu Wilayani Biharamulo na kwingineko nchini wanalalamika kwamba jitihada zao kwenda masomoni kujiendeleza zinafuatiwa na kusitishwa kwa upandaji wa madaraja yao katika utumishi wa umma. Pale ambapo mwalimu kapanda daraja kunaenda sanjari na yeye kuwa masomoni. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kero hii na kukatishwa tamaa kwa walimu wetu?

Supplementary Question 1

MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini naomba kufahamu kwamba kwa maelekezo hayo ambayo Serikali imeyatoa kwa waajiri kutekeleza upandishwaji wa madaraja hayo.
Je, Serikali iko tayari sasa kuratibu suala hilo ili kuhakikisha kwamba tunafanya uhakiki wa walimu wote wenye malalamiko haya ili yapatiwe utatuzi.
Swali la pili, kwa sababu pia yako malalamiko kutoka kwenye Halmashauri zetu kwamba Walimu wanapokwenda kujiendeleza unatokea upungufu wa Walimu kwenye shule wanazotoka.
Je, Serikali iko tayari kutumia vizuri fursa ya Chuo Kikuu Huria ili yenyewe kwa ngazi ya Serikali Kuu iratibu namna ya kuwasaidia Walimu wajiendeleze kwa kupitia Chuo Kikuu Huria bila kuathiri uwepo wao kwenye shule zao? Ninakushukuru.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hoja ya Mheshimiwa Oscar ni kwamba kufanya tathmini ya kuratibu vizuri mchakato huu, naomba tulipokee hili kwa sababu lengo kubwa ni kwamba kama Serikali tuna haja ya watumishi mbalimbali ambao malalamiko yao yapo yaweze kufanyiwa kazi kwa sababu tunajua yakifanyiwa kazi vizuri ndiyo wataweza kufanya kazi vizuri wanapokuwa ofisini mwao.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Mheshimiwa Mukasa nadhani hii ni hoja ya mapendekezo na sisi tutaangalia jinsi gani tuweze kuratibu vizuri ili haki ya mfanyakazi iweze kupatikana.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili katika eneo la pili ni kwamba jinsi gani tufanye kwamba tutoe maelekezo ya watumishi wote kada ya ualimu kutumia Chuo Kikuu Huria. Nadhani tuweke hili dirisha wazi kwa sababu kila mwalimu ana preference yake na kitu gani anachokihitaji, isipokuwa jambo la misngi ni lazima tuweke mipango mizuri lengo ni kwamba walimu watakapoenda kujiendeleza basi tusiwe na mapungufu makubwa katika maeneo yetu. Tunajua kwamba tatizo hili limekabili maeneo mbalimbali lakini hoja hii ni hoja ya msingi nadhani hili sasa katika mamlaka ya Serikali za Mitaa tutatoa maelekezo mahsusi ya kiutawala/kiofisi kwamba nini kifanyike kama walimu wangapi wanatakiwa wakiondoka wengine wabaki, ili watoto wasiathirike.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo katika mchakato wetu ambao tunaufanya hivi sasa lengo kubwa ni kuajiri walimu wapya tunajua kwamba tukiongeza idadi ya Walimu tutaweza kupunguza kwa kiwango kikubwa tatizo hili ambalo liko hivi sasa katika Halmashauri zetu. (Makofi)

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini nataka kuweka msisitizo tu kwamba msimamo wa Serikali kuhusu wanafunzi kujiunga na vyuo vikuu ni kwamba mwanafunzi anachagua mwenyewe mahali ambapo anataka kusoma, kwa hiyo utaratibu huo unawahusu watarajiwa wote wa vyuo vikuu ikiwa ni pamoja na walimu. Kwa hiyo, Serikali itaendelea kuweka tu mazingira mazuri ili wanafunzi waweze kuendelea kuwa na fursa ya kwenda mahali wanapotaka lakini Serikali haiwezi ikampangia mtu kinyume na matakwa yake. (Makofi)

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:- Walimu Wilayani Biharamulo na kwingineko nchini wanalalamika kwamba jitihada zao kwenda masomoni kujiendeleza zinafuatiwa na kusitishwa kwa upandaji wa madaraja yao katika utumishi wa umma. Pale ambapo mwalimu kapanda daraja kunaenda sanjari na yeye kuwa masomoni. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kero hii na kukatishwa tamaa kwa walimu wetu?

Supplementary Question 2

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na tabia kwenye Halmashauri wanapokwenda masomoni baadhi ya watumishi kwenye Halmashauri, Halmashauri zinakuwa zinagharamia hususan wale walioko kwenye ngazi ya pale Halmashauri. Lakini si kwa kada za ualimu na kada zingine.
Je, nini kauli ya Serikali kwamba Halmashauri zinagharamia masomo kwa wale watumishi waliopo ndani ya Halmashauri pale pale au kwa watumishi wa Halmashauri nzima? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu ni kwamba kuna utaratibu wa mapendekezo ya watu kuonyesha preference yao kwamba watu wanataka kwenda kusoma, hili mara nyingi sana huwa inawekwa katika mchanganuo wa kibajeti katika kila Idara, kwamba kila Idara ina utaratibu na mipango yake kwamba mwaka huu kuna watu wangapi wataenda kusoma. Kwa hiyo, jambo hili sio wale wa Makao Makuu peke yake hapana, jambo hili maana yake ni kwa Halmashauri nzima, kama kuna Halmashauri ambayo inafanya kuwapa upendeleo maalum wale waliopo Makao Makuu peke yake, hilo ni kosa na halikubaliki.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, utaratibu ni kwamba mpango wa bajeti wanapopanga bajeti wanapanga mwaka huu Idara fulani tutapeleka watu fulani kusoma katika level fulani ambayo inaingizwa katika bajeti, then unaweka hilo open door policy katika hiyo Idara, kila mtu aweze ku-apply kuangalia nani ata-qualify katika kipindi hicho kuweza kupata fursa ya masomo, kwa sababu mkate huo ni mkate wa Halmashauri nzima siyo watu maalum katika Makao Makuu ya Halmashauri.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:- Walimu Wilayani Biharamulo na kwingineko nchini wanalalamika kwamba jitihada zao kwenda masomoni kujiendeleza zinafuatiwa na kusitishwa kwa upandaji wa madaraja yao katika utumishi wa umma. Pale ambapo mwalimu kapanda daraja kunaenda sanjari na yeye kuwa masomoni. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kero hii na kukatishwa tamaa kwa walimu wetu?

Supplementary Question 3

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naomba kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, walimu wengi walipata fursa ya kwenda kujiendeleza na waliweza kujiendeleza, pale wanapokuwa wanafanya hayo masomo yao katika ngazi ya shahada wanapokwenda kwenye ile Block Teaching Practice walimu hawa wanapangiwa kwenye shule za sekondari na wanapomaliza bado walimu hawa wanarejeshwa kwenye shule za msingi. Wanaporejeshwa kwenye shule za msingi, yale waliyosomea hayapo kwenye shule za msingi bali yapo kwenye shule za sekondari.
Serikali hapa ina utaratibu gani wa kubadilisha au wa kutengeneza mitaala kuhusiana na shule za msingi ili wakitoka kule warudi kule kule walikotoka? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani Mama yangu Salma Kikwete anazungumzia changamoto za jinsi gani tuweze kuboresha elimu yetu kwa watu walioko katika vyuo wanapoenda kwenye katika zile field practical na wanapoenda kufundisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, hili ni wazo kwa sababu bahati nzuri Mheshimiwa ni mwalimu anajua changamoto gani zipo na vipi tuziboreshe. Mimi naomba tulichukue hili kama wazo jema, kwamba nini tufanye hasa katika suala zima la mitaala kiujumla wake, hata hivyo, tuangalie ni jinsi gani wanafunzi wetu wanapokuwa katika masomo, kile kitu ambacho anaenda kufanyia field practical na iwe best practice akienda kwenye kazi. Kwa hiyo, nasema huu ni ushauri mzuri, Serikali tumeuchukua, tunachukua mawazo mazuri, kwa sababu tuko katika mchakato wa kuboresha elimu yetu iwe elimu shindani tunachukua mawazo haya kwa ajili ya kuyafanyia kazi vizuri. (Makofi)

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TAKNOLOJIA:
Mheshiwa Naibu Spika, ahsante sana. nampongeza Mheshimiwa kwa majibu mazuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuongezea tu kwamba lengo la kufanya mafunzo kwa vitendo ni kutoa fursa kwa wanafunzi kuweza kufanya kwa vitendo kile ambacho wanajifunza. Katika teaching practice jambo kubwa ambalo linaangaliwa ni ule mfumo wa ufundishaji yaani kwa kingereza tunaita pedagogical skills, jinsi ambavyo mwalimu anaweza akalihimili darasa, anaweza akafanya yale ambayo yanatakiwa kumudu darasa lake. Kwa hiyo, mwalimu ambaye anajifunza mafunzo ya sekondari principal za darasani kwenda kujifunza, hata akienda kufanya katika shule za msingi hakuna jambo lolote ambalo linaharibika. Ndio maana wapo walimu wa sekondari wanapangiwa kwenda kufundisha shule za msingi kwa sababu kinachoangaliwa ni ule uwezo wa mwalimu kufanya ule ufundishaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na nini anachokifundisha, ukiangalia maudhui ya mtaala katika elimu ya msingi ni ya kiwango cha chini kuliko ya sekondari. Kwa hiyo, ni dhahiri kwamba mwalimu ambaye ana uwezo wa kufundisha sekondari atakuwa ni mwalimu mzuri sana katika kufundisha shule za msingi. (Makofi)