Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 53 2017-09-11

Name

Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:-
Walimu Wilayani Biharamulo na kwingineko nchini wanalalamika kwamba jitihada zao kwenda masomoni kujiendeleza zinafuatiwa na kusitishwa kwa upandaji wa madaraja yao katika utumishi wa umma. Pale ambapo mwalimu kapanda daraja kunaenda sanjari na yeye kuwa masomoni.
Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kero hii na kukatishwa tamaa kwa walimu wetu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oscar Rwegasira Mukasa, Mbunge wa Biharamulo Magharibi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, tunawapongeza walimu wote na wataalam mbalimbali wanaojiendeleza kwa lengo la kuongeza ufanisi wao wawapo kazini. Kwa utaratibu wa sasa kupanda daraja kunaendana na matokeo ya ufanisi kazini baada ya kupimwa jinsi mtumishi alivyotekeleza malengo yake. Kwa utaratibu uliopo, mwalimu aliyejiendeleza hadi ngazi ya stashahada au shahada anapaswa kubadilishiwa muundo baada ya kuwasilisha vyeti vyake kwa mwajiri wake. Hivyo, waajiri wote wanapaswa kuzingatia taratibu za utumishi kwa kutenga bajeti kwa watumishi walio katika maeneo yao.