Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:- Katika Mradi wa REA II, Jimbo la Bagamoyo lilipewa vijiji 10 tu na bado utekelezaji wake unasuasua na uko nyuma ya ratiba:- Je, ni lini miradi ya umeme kwa Vijiji vya Kongo, Kondo na nyongeza ya Matimbwa itakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yenye kutia moyo, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Kwanza; nilijulishwa na uongozi wa REA kwamba Vijiji vya Kongo na Kondo ambavyo havikutekelezewa miradi yake katika awamu ya pili vimeingizwa kwenye orodha ya miradi ya nyongeza kwenye REA-III ambayo imeombewa kibali kwa ajili ya utekelezaji. Sasa swali; je, lini kibali hicho kitaweza kutolewa ili miradi hiyo itekelezwe?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kufuatana na orodha ya miradi ya REA Awamu ya Tatu kwenye Jimbo la Bagamoyo, vijiji vingi katika Kata za Fukayosi, Makurunge, Mapinga, Kerege na Zinga havitopata umeme. Je, Serikali ina mkakati gani kuweza kuvipatia umeme vitongoji hivyo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nampongeza Mheshimiwa Dkt. Kawambwa kwa juhudi zake anavyofuatilia mahitaji ya umeme kwa wananchi wa Bagamoyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama alivyotaja, Vijiji vya Kondo, Kongo, Matimba pamoja na Fukayosi kimsingi vilishapata approval na viko kwenye REA awamu ya tatu hii inayoanza sasa hivi. Naomba nimhakikishie kwamba katika shule yake ya sekondari aliyojenga Fukayosi kwa wafadhili, tayari wiki ijayo wanafanya survey ili ianze kupelekewa umeme katika awamu hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vilivyobaki ambavyo amevitaja; Mapinga, Kerenge pamoja na maeneo ya Zinga ambavyo ni vijiji 22, navyo vitaanza kupelekewa umeme kuanzia mwezi Machi, 2019 na kufikia mwaka 2020 vyote vitakuwa vimeshapata umeme.

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:- Katika Mradi wa REA II, Jimbo la Bagamoyo lilipewa vijiji 10 tu na bado utekelezaji wake unasuasua na uko nyuma ya ratiba:- Je, ni lini miradi ya umeme kwa Vijiji vya Kongo, Kondo na nyongeza ya Matimbwa itakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa matatizo yanayowakabili wananchi wa Bagamoyo yanafanana kabisa na ya Morogoro Kusini Mashariki. Kwenye mipango ya Serikali ya REA awamu ya tatu, Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki tumepata vijiji saba tu na kuacha vijiji 47 kati ya vijiji 64 ambavyo vyote havina umeme katika Kata za Tegetero, Kibuko, Tomondo, Maturi, Mkulazi na Seregeti. Je, Serikali ina mkakati gani wa kupeleka umeme katika huu mradi wa REA awamu ya tatu, katika Kata hizo na vijiji vyake vyote?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa Mheshimiwa Mbunge anavyosema. Kwanza nimpongeze, nilipokuja kuzindua Morogoro tulishirikiana na Mheshimiwa Omary na nilimwambia alete vijiji vyake tuviboreshe.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, tumeshafanya mapitio siyo vijiji saba vinavyopelekewa umeme raundi ya kwanza bali ni vijiji 14. Hata hivyo, vile vijiji vingine 47 alivyotaja basi tutakaa tuvipitie, lakini vyote vitapatiwa umeme kwenye raundi inayofuata itakayoishia mwaka 2021.