Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 116 2017-09-15

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:-
Katika Mradi wa REA II, Jimbo la Bagamoyo lilipewa vijiji 10 tu na bado utekelezaji wake unasuasua na uko nyuma ya ratiba:-
Je, ni lini miradi ya umeme kwa Vijiji vya Kongo, Kondo na nyongeza ya Matimbwa itakamilika?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa, Mbunge wa Bagamoyo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ilikamilisha kupeleka umeme vijijini kupitia Mradi wa REA Awamu ya Pili ikiwemo Wilaya ya Bagamoyo mwezi Desemba, 2016. Kazi ya mradi huo katika Wilaya ya Bagamoyo ilijumuisha ujenzi wa njia kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 80.13, ujenzi wa njia kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 106.67 pamoja na ufungaji wa transfoma 41, kazi nyingine ilikuwa kuwaunganisha wateja wa awali 2,066 na gharama za utekelezaji wa mradi zilikuwa shilingi bilioni 30.
Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu ya Kijiji cha Matimbwa iliyobaki kupatiwa umeme pamoja na vijiji vingine ikiwemo Kondo vitafikishiwa umeme kupitia Mradi wa REA Awamu ya Tatu iliyoanza mwezi Juni, 2017 utakaokamilika mwaka 2020/2021.