Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

CAN.RTD Ali Khamis Masoud

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mfenesini

Primary Question

MHE. KANALI (MST) MASOUD ALI KHAMIS aliuliza:- Kwa muda mrefu sasa Serikali imekuwa ikitoa ahadi za kutatua tatizo la usafiri kwa Jeshi la Polisi bila mafanikio. Kwa mfano, Kituo cha Polisi Mfenesini, Zanzibar hakina gari la uhakika kwa takribani miaka 10 sasa:- (a) Je, ni lini Serikali itapeleka gari Kituo cha Polisi Mfenesini? (b) Je, ni lini magari ambayo yamekuwa yakizungumzwa kwa muda mrefu yatawasili nchini ili kuondoa adha ya usafiri?

Supplementary Question 1

MHE. KANALI (MST) MASOUD ALI KHAMIS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kuna magari 13 yanatoa huduma za doria katika maeneo hayo. Nataka nimfahamishe tu Mheshimiwa Naibu Waziri, mimi naishi karibu na kituo hiki, hata kilomita moja haitimii. Yameshatokea matukio kadhaa na Askari wanawajibika kuondoka kituoni kwenda kwenye matukio yale wanashindwa kufanya hivyo na wakati mwingine tumekuwa tukitoa msaada wa magari yetu binafsi kuwasaidia. Je, kati ya magari haya 13, kwa nini sasa gari moja lisipelekwe Kituo cha Polisi Mfenesini.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa ufahamu wangu mkataba wowote wa kuagiza vifaa vyovyote vile vya kijeshi ama vya kiraia unakuwa na makubaliano na supplier vitu vile vitawasili lini. Magari haya tunaambiwa yanakuja kwa awamu na swali lilikuwa yatawasili lini hata kama kwa awamu, je, magari yatawasili lini? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimejibu katika majibu ya msingi, kwamba tutapeleka gari katika kituo cha Wilaya cha Mfenesini kwa kutambua kwamba magari haya 13 ya Mkoa na gari ambalo anatumia OCD hayakidhi haja. Nimhakikishie tu kwamba hivi sasa tuna mpango wa kupata magari 50, bahati mbaya hatuna hakika kama yapo magari ya kutosha yenye sifa za kukidhi kuwa magari ya kituo, kwa sababu mengi ya magari ambayo tunatarajia yaje sasa hivi ambayo tayari yameshafika tupo katika mkakati wa kuyatoa mengi ni malori.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ikionekana kwamba magari hayo yanakidhi vigezo vya kuweza kuhudumia Kituo cha Mfenesini, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kituo chake cha Mfenesini ni moja katika maeneo ambayo yatapata gari hizo.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KANALI (MST) MASOUD ALI KHAMIS aliuliza:- Kwa muda mrefu sasa Serikali imekuwa ikitoa ahadi za kutatua tatizo la usafiri kwa Jeshi la Polisi bila mafanikio. Kwa mfano, Kituo cha Polisi Mfenesini, Zanzibar hakina gari la uhakika kwa takribani miaka 10 sasa:- (a) Je, ni lini Serikali itapeleka gari Kituo cha Polisi Mfenesini? (b) Je, ni lini magari ambayo yamekuwa yakizungumzwa kwa muda mrefu yatawasili nchini ili kuondoa adha ya usafiri?

Supplementary Question 2

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Tatizo lililopo Mfenesini linafanana kwa ukaribu kabisa na tatizo ambalo lipo katika Mkoa wa Songe na ukizingatia kwamba Mkoa wa Songwe ni mpya na umekuwa na changamoto kubwa sana za kiuhalifu. Changamoto kubwa iliyopo ni suala la usafiri kwa Jeshi la Polisi hususan katika Wilaya mpya ya Songwe. Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka magari katika Mkoa wa Songwe hususan katika Wilaya mpya ya Songwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, tunatambua Mikoa na Wilaya mpya nyingi zina changamoto sio tu za magari pamoja hata na vitendea kazi, ofisi na nyumba. Kwa hiyo, ni kipaumbele cha Wizara yetu kuona kwamba tunapopata vifaa na uwezo wa kuweza kuimarisha vitendea kazi katika maeneo hayo, tunaangalia mikoa hii ambayo ni mipya ukiwemo Mkoa wa Songwe.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. KANALI (MST) MASOUD ALI KHAMIS aliuliza:- Kwa muda mrefu sasa Serikali imekuwa ikitoa ahadi za kutatua tatizo la usafiri kwa Jeshi la Polisi bila mafanikio. Kwa mfano, Kituo cha Polisi Mfenesini, Zanzibar hakina gari la uhakika kwa takribani miaka 10 sasa:- (a) Je, ni lini Serikali itapeleka gari Kituo cha Polisi Mfenesini? (b) Je, ni lini magari ambayo yamekuwa yakizungumzwa kwa muda mrefu yatawasili nchini ili kuondoa adha ya usafiri?

Supplementary Question 3

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kituo cha Polisi Himo kinatoa huduma kwa watu zaidi ya laki tano na kipo mpakani na Serikali ilishaahidi hapa Bungeni tangu mwaka 2013 kwamba itapeleka magari mawili (2) mapya kwa ajili ya kutoa huduma kwenye kituo hicho kutokana na umuhimu wake. Hali sasa ni tete sana, kituo kinatumia pikipiki wako kwenye hali mbaya sana. Je, sasa Serikali ni lini kwa dharura itapeleka magari haya mawili waliyoahidi kwa zaidi ya miaka minne (4) katika Kituo cha Polisi cha Himo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbatia kwamba kama ni ahadi ambayo imetolewa na Serikali ya kupeleka gari katika kituo cha Himo, basi nitaifuatilia nitakapotoka tu hapa, kujua ni kitu gani kinachokwamisha ahadi hiyo isitekelezwe mpaka leo ili tuone jinsi gani tunaweza tukaitekeleza pale tutakapopata uwezo wa magari ya kutosha tuangalie haraka iwezekanavyo tunaweza vipi kutimiza ahadi hiyo ya Serikali ya muda mrefu.

Name

Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. KANALI (MST) MASOUD ALI KHAMIS aliuliza:- Kwa muda mrefu sasa Serikali imekuwa ikitoa ahadi za kutatua tatizo la usafiri kwa Jeshi la Polisi bila mafanikio. Kwa mfano, Kituo cha Polisi Mfenesini, Zanzibar hakina gari la uhakika kwa takribani miaka 10 sasa:- (a) Je, ni lini Serikali itapeleka gari Kituo cha Polisi Mfenesini? (b) Je, ni lini magari ambayo yamekuwa yakizungumzwa kwa muda mrefu yatawasili nchini ili kuondoa adha ya usafiri?

Supplementary Question 4

MHE. MAGANLAL MEISURIA BHAGWANJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana umenipa nafasi, Mungu akuweke.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niseme jambo moja katika Jimbo langu la Chwaka, hakuna gari katika Jimbo la Chwaka pamoja na Jozani kwa sababu pana bahari na hoteli zipo nyingi sana. Kwa hiyo, wanaweza kuja majambazi, inaweza kuwa ni mambo ya siasa, hivyo ni muhimu sana gari ipatikane haraka kwa watu wangu wa Jimbo la Chwaka pamoja na Jozani, kwa hisani yako. (Makofi/Kicheko

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, tumelipokea ombi la Mheshimiwa Mbunge na tutalifanyia kazi. (Makofi)