Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 110 2017-09-15

Name

CAN.RTD Ali Khamis Masoud

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mfenesini

Primary Question

MHE. KANALI (MST) MASOUD ALI KHAMIS aliuliza:-
Kwa muda mrefu sasa Serikali imekuwa ikitoa ahadi za kutatua tatizo la usafiri kwa Jeshi la Polisi bila mafanikio. Kwa mfano, Kituo cha Polisi Mfenesini, Zanzibar hakina gari la uhakika kwa takribani miaka 10 sasa:-
(a) Je, ni lini Serikali itapeleka gari Kituo cha Polisi Mfenesini?
(b) Je, ni lini magari ambayo yamekuwa yakizungumzwa kwa muda mrefu yatawasili nchini ili kuondoa adha ya usafiri?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kanali (Mst) Masoud Ali Khamis, Mbunge wa Mfenesini, lenye sehemu
(a) na (b), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Polisi Mfenesini kipo Mkoa wa Kaskazini Unguja katika Wilaya ya Kipolisi Mjini Magharibi A. Mkoa wa Kaskazini Unguja una jumla ya magari 13 ambayo yanatoa huduma za doria na kazi nyingine za Polisi katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mjini Magharibi ikiwemo Kituo cha Polisi Mfenesini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kituo cha Polisi Mfenesini kitapatiwa gari mara baada ya taratibu za upatikanaji wa magari utakapokamilika. Hata hivyo, gari la Mkuu wa Polisi wa Wilaya hutoa huduma pale inapotokea dharura ikiwa ni pamoja na kuwachukua mahabusu waliopo katika kituo hicho.
Mheshimiwa Naibu Spika, magari haya yamekuwa yakiwasili nchini awamu nchini awamu kwa awamu ambapo hadi sasa jumla ya magari 231 yamekwishawasili kati ya magari 777 yaliyokuwa yameagizwa.