Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Fedha zinazokusanywa za asilimia 0.3 ya service levy zimeshindwa kusaidia Halmashauri nchini kwa uwiano unaolingana. Je, Serikali haioni kuwa ni wakati muafaka fedha hizo kukusanywa na TAMISEMI ili kila Halmashauri iweze kupata mgao unaolingana?

Supplementary Question 1

MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa muda mrefu sasa Halmashauri nyingi nchini zimekuwa zikipoteza mapato ambayo yamepotea kupitia kampuni mbalimbali za simu kwa kutokulipa hizo service levy katika maeneo mengi nchini.
Je, ni lini sasa Serikali itazibana kampuni hizo ili ziweze kulipa hiyo service levy?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kutokana na Halmashauri nyingi nchini kuwa na vyanzo vichache vya mapato. Je, ni lini Serikali itaweza kufanya mpango wa kuziongezea Capital Development Grants Halmashauri hizo nchini? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI MIKOA: Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Ester kwa sababu najua kwamba anaguswa na Halmashauri zake zote ambazo anazisimamia katika mkoa wake. Naomba niwahakikishie kwamba ndiyo maana tumeandaa sheria hii ya fedha, mabadiliko ya Sura Namba 290 kwa lengo la kufanya utaratibu mzuri wa kukusanya hizi kodi.
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Ester amezungumzia suala zima la minara ambalo lilikuwa linaleta mkanganyiko mkubwa sana. Katika jambo ambalo litashughulikiwa kwa undani zaidi ni suala zima la ushuru wa minara ambalo tunaliwekea utaratibu kwa mujibu wa sheria.
Mheshimiwa Spika, nina imani ikifika hapa Bungeni, tutajadili tuone ni utaratibu gani tutafanya. Ninaamini na sheria itakuja siyo muda mrefu, tutaweka utaratibu mzuri ili tuweze kuwabana vizuri hawa wenye makampuni mbalimbali hasa ya simu, waweze kulipa kodi vizuri. Lengo kubwa ni kuziwezesha Halmashauri zetu ziweze kufanya vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, katika mchakato huu wote wa sheria hizi, lengo kubwa la Serikali ni kuziongezea Halmashauri zetu uwezo wa kupata mapato ya kutosha kwa ajili ya kujiendesha.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, katika suala zima la kujiendesha, kuongeza ile Capital Development Grand ni jukumu la Serikali. Ndiyo maana hata ukiachia hilo, ukiangalia ile Local Government Development Grants hata mwaka huu tumeongeza zaidi ya shilingi bilioni 251 kwa lengo tu la ku- facilitate Halmashauri ziweze kufanya kazi yake vizuri.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, eneo hilo tutaangalia nini tufanye Halmashauri zetu ziweze kufanya vizuri tukijua kwamba Halmashauri zikifanya vizuri ndiyo nchi itaenda vizuri katika suala zima la maendeleo.