Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 69 2017-09-12

Name

Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:-
Fedha zinazokusanywa za asilimia 0.3 ya service levy zimeshindwa kusaidia Halmashauri nchini kwa uwiano unaolingana.
Je, Serikali haioni kuwa ni wakati muafaka fedha hizo kukusanywa na TAMISEMI ili kila Halmashauri iweze kupata mgao unaolingana?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ester Alexander Mahawe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, service levy ni chanzo kinachokusanywa na Halmashauri kwa mujibu wa Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa Sura 290 kifungu cha 6(1) na 7(1). Ushuru huo unatozwa kutoka kwa makampuni, matawi ya makampuni na mfanyabiashara yeyote mwenye leseni ambaye anafanya shughuli zake katika Halmashauri husika. Hivyo, Halmashauri ndiyo yenye mamlaka ya kukusanya ushuru huo kwa mujibu wa sheria. Ofisi ya Rais, TAMISEMI kazi yake ni kuandaa sera, sheria, kanuni na miongozo na kusimamia utekelezaji wake kwenye mamlaka za Serikali za Mitaa.
Mheshimiwa Spika, Serikali imepanga kuboresha utaratibu unaotumika kukusanya ushuru huo kwenye Halmashauri kwa kufanya marekebisho ya Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa ili kuondoa utata uliokuwepo ambapo makampuni yalikuwa hayalipi ushuru huo kwa kuzingatia kuwa unalipwa Makao Makuu ya Kampuni.
Mheshimiwa Spika, Bunge litapata fursa ya kujadili marekebisho hayo ambayo yanakusudia kuziwezesha Halmashauri kukusanya ushuru wa huduma kwa kiwango cha kuridhisha.