Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:- (a) Je, kuna vituo vingapi vinavyorusha matangazo kwa njia ya televisheni nchini na vinamilikiwa na Kampuni zipi? (b) Je, ni vituo vingapi vinarusha matangazo ya televisheni bure kwa wananchi kupitia ving’amuzi?

Supplementary Question 1

MHE. MARTIN M. MSUHA: Ahsante sana kwa kupata nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, ninalo swali moja la nyongeza.
Lipo tatizo kubwa na la muonekano na upatikanaji
wa TBC1 kwenye maeneo mengi ya Wilaya ya Mbinga lakini pia ukanda mzima wa Ziwa Nyasa hususani kule kwenye tarafa ya Mhagati, Tarafa ya Mkumbi lakini pia Tarafa ya Namswea. Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha upatikanaji wa TBC1 katika maeneo tajwa hapo juu ukizingatia hicho ndicho kituo pekee kutoa matangazo bila kulipia? Ahsante.

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, kama tutakumbuka katika bajeti ya mwaka huu zilitengwa shilingi bilioni tatu zaidi kama fedha za maendeleo kwa TBC na hizi ni pamoja na kuboresha television ya TBC1 pamoja na usikivu wa redio. Kwa hiyo, mpaka sasa katika maeneo aliyoyataja ya Mhagati, Namsweha na maeneo mengine, TBC bado inafanya tathmini kuona mgawanyo huo wa fedha uelekee wapi kwa upande kwa radi na uelekee wapi kwa upande wa television. Naomba kuwasilisha na ahsante.

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:- (a) Je, kuna vituo vingapi vinavyorusha matangazo kwa njia ya televisheni nchini na vinamilikiwa na Kampuni zipi? (b) Je, ni vituo vingapi vinarusha matangazo ya televisheni bure kwa wananchi kupitia ving’amuzi?

Supplementary Question 2

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.
Wakati Tanzania inatoka katika mfumo wa analojia kuingia katika mfumo wa dijitali inaeleweka kwamba Startimes ndio waliopewa jukumu hilo na katika makubaliano ilikuwa kwamba unapolipia kile king’amuzi cha kwa maana ya kwamba hizi channel za hapa nchini ni bure lakini ni tofauti na ilivyo sasa ni kwamba wamekuwa wakiondoa hizi channel za hapa nchini hazionekani tena kama ilivyokuwa awali. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri na jitihada hizo, ninaomba kufahamu ni kwa nini Startimes imekiuka mkataba huo na badala yake hivi sasa hakuna tena kituo chochote cha television ambacho unaweza kukiona baada ya malipo tuliyokuwa tunapaswa kulipia kuisha?

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwanza nichukue nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Amina Mollel, Mbunge wa Viti Maalum, kwa kuuliza swali ambalo limekuwa likiulizwa mara nyingi sana na wateja na watumiaji wa tv.
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba wakati mwingine utakuta kwamba mteja anapokuwa amelipia kifurushi na kifurushi chake kikawa kimekwisha basi zile channel ambazo tunaziita kwamba ni free to air zinakuwa hazionekani. Sasa tatizo ni kwamba, kama nilivyotangulia kusema TBC1 peke yake ndiyo ambayo inaonekana katika hivi ving’amuzi vya DDT pamoja na DTH bure bila kulipia. Kwa hiyo, TBC1 hailipi chochote kwa hawa transmitters kabisa. Lakini Sheria ya Leseni walizopata hawa transmitters ina masharti kwamba hizi free to air zote wale wamiliki au makampuni ya televisheni wanatakiwa wawe wanalipa ada fulani kila mwezi, sheria inamruhusu yule transmitter kumkatia au kumuondoa pale ambapo atakuwa ameshindwa kulipa.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tatizo linatokea kwamba hawa content providers wanapokuwa wameshindwa kulipa basi wanaondolewa na hawa transmitters. Kwa sasa hatua zimeshachukuliwa, TCRA imewaita na kuwataka wajieleze vizuri ni kwa nini hawalipi kwa sababu wao ndiyo wanaosababisha sasa hizi zisionekane na Sheria inawaruhusu wale transmitters waoneshe kama hawatalipa.
Kwa hiyo, kutokana na kutokulipa kwao ndiyo maana unakuta hizi free to air channel hazionekani lakini sio kwamba yule mteja ndiyo anayetakiwa alipe.
Mheshimiwa Spika, mteja ananunua kifurushi kwa ajili ya zile pay channels lakini sio kwa hizi free to air. Kwa hiyo kimsingi anatakiwa aendelee kuziona hata kama hakulipia/hakununua kifurushi. Kwa hiyo, pale itakapoonekana kwamba maelezo yao hayaridhishi watachukuliwa hatua kali. Hivyo nichukue nafasi hii kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuwataka wamiliki wote wa tv stations walipie mara moja ada zao za mwezi ili kusudi wananchi waweze kufaidi hizi free to air services. Ahsante.(Makofi)