Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 4 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 42 2017-09-08

Name

Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:-
(a) Je, kuna vituo vingapi vinavyorusha matangazo kwa njia ya televisheni nchini na vinamilikiwa na Kampuni zipi?
(b) Je, ni vituo vingapi vinarusha matangazo ya televisheni bure kwa wananchi kupitia ving’amuzi?

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO, alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Martin Alexander Mtonda Msuha, Mbunge wa Mbinga Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya mawasiliano Tanzania imetoa leseni kwa vituo 32 vya Television hapa nchini. Orodha ya vituo hivyo na wamiliki wa vituo hivyo ni ndefu naomba nisiisome hapa ila nimekwishamkabidhi Mheshimiwa Mbunge na ninaomba iingie kwenye Hansard.
(b)Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania hutoa leseni ya maudhui ya utangazaji wa televisheni za aina mbili. Leseni za maudhui yanayotazamwa bila kulipia (free to air) na maudhui ya kulipia (pay tv). Aidha, leseni hizi zimegawanywa kimasoko. Kuna leseni za kitaifa ambazo hupaswa kuonekana nchi nzima na kuna leseni za kimkoa ambazo huruhusiwa kutangaza mikoa kumi ya Tanzania Bara na leseni za kiwilaya ambazo huonekana mkoa mmoja.
Mgawanyo huu wa kimasoko unatoa fursa kwa waombaji kutangaza maeneo wanayochangua kutokana na uwezo wao wa kifedha na na kiuendeshaji. Maudhui haya ya bila kulipia huonekana kupitia ving’amuzi vya Mkampuni ya Agape Associates Limited, Basic Transmission Limited na Star Media Tanzania Limited. Visimbuzi hivi ni TING, Startimes, DIGITEC na CONTINENTAL Vituo vyenye leseni ya soko la kitaifa ni TBC1, Channel 10, East Africa Televison, Independent Television, Star Television, Clouds TV na Bunge TV. Vituo vyenye soko la kimkoa ni TV Imaan, Agape TV (ATV) na TV1 zilizobaki zina soko la kiwilaya.
Aidha, Kituo cha TBC1 ambacho ni kituo cha umma (public broadcaster) kinapatikana bila malipo ya mwezi kwenye ving’amuzi vyote vya miundombinu isiyosimikwa ardhini yaani Digital Terrestrial Television na vile vinavyotumia mitambo ya satelite yaani direct to home kama vile Azam TV, DSTV na Zuku. Kituo cha TBC1 kinalazimika kuonekana bila malipo kwa mujibu wa masharti ya leseni za makampuni ya miundombinu ya utangazaji wa ardhini yaani DTT na Satelite (DTH).

ORODHA YA VITUO VYA TELEVISHENI NA WAMILIKI WAKE

1. Independent Television (ITV) - Reginald Mengi & Family Trust 99% & Reginald Abraham Mengi 1%
2. Star Television - Diallo Investment Co. Limited 50% & Nyalla Investment Co. Limited 50%
3. Channel Ten Television - Africa Media Group Limited 100%
4. TBC 1 - Tanzania Broadcasting Corporation 100%
5. TBC 2 - Tanzania Broadcasting Corporation 100%
6. East Africa Television (EATV) - Reginald Mengi & Family Trust 99% & Reginald Abraham Mengi 1%
7. Agape Television (ATV) - World Agape Ministries 100%
8. C2C Television - Africa Media Group Limited 100%
9. Dar es Salaam Television (DTV) - Africa Media Group Limited 100%
10. Abood Television - Aziz Mohammed Abood 50% & Fauzi Mohammed Abood 50%
11. CTN Television - Africa Media Group Limited 100%
12. Capital Television - Reginald Mengi & Family Trust 99% & Reginald Abraham Mengi 1%
13. Clouds TV - Joseph Mlebya Kusaga 50%, Andrew Dogan Kusaga 20% & Alex Kusaga Mkama 30%
14. VIASAT 1 Television - Dr. Gideon H. Kaunda 7.5%, Ambassador Paul Milyango Rupia 7.5% & Dr. Wilbert Basilius Kapinga 36%