Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Salma Mohamed Mwassa

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALMA M. MWASSA aliuliza:- Miongoni mwa changamoto zinazokwamisha kuleta tija katika ukusanyaji wa kodi kwenye Halmashauri zetu ni pamoja na ubutu wa Sheria Ndogo Ndogo (By laws):- Je, ni lini sheria hizo zitarekebishwa ili zilete tija katika ukusanyaji kodi?

Supplementary Question 1

MHE. SALMA M. MWASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, lakini nina swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na mazoea ya kuchelewa kurekebishwa kwa sheria hizi ndogo ndogo na Serikali Kuu na badala yake kwa zile Halmashauri ambazo zinajitahidi zenyewe hasa zikiwemo za mijini, zinakuwa zinanyang’anywa mamlaka yake na Serikali Kuu. Kwa mfano, Kodi ya Majengo (Property Tax) kupelekwa TRA na tume-prove kwa miaka miwili ya nyuma TRA ilishindwa kabisa kukusanywa kodi hii; na sasa tunaambiwa kodi hii inaenda tena TRA. Je, ni lini hasa Serikali Kuu itaacha kuingilia mamlaka au kunyang’anya mamlaka ya Serikali za Mitaa ili ziweze kujitegema?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli wakati mwingine Marekebisho ya Sheria yanachelewa lakini mara nyingi sana yanafanyika mara baada ya mahitaji mahususi yanapotokea. Kwa sababu tuelewe kwanza katika suala zima la Serikali za Mitaa kuna maeneo matatu; kuna Sura Namba 287, 288 na 290. Sura ya 290 ndiyo inalenga hasa katika ukusanywaji wa kodi na ushuru mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, ajenda ya kusema kwamba ni lini sasa Serikali itaanza kuzuia suala zima la kunyang’anya mamlaka ya Serikali za Mitaa, kutoa kodi kwa mfano katika kodi ya majengo; Serikali sasa hivi tuko katika Serikali ya Awamu ya Tano, naamini Bunge hili ndiyo Bunge ambalo mara ya kwanza tunajadili bajeti yetu katika kipindi hiki cha Awamu ya Tano na ninaamini kwamba mjadala huu wa bajeti utakapofika katika suala zima la Wizara ya Fedha, mwisho katika Wizara ya Fedha kuna ile Sheria ya Fedha ya mwisho pale ndio tutapata way forward tunapokwenda ni wapi. Lengo kubwa la Serikali ni kuhakikisha mapato yanakusanywa katika Serikali yake ili mradi mambo yaweze kuendelea vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwahiyo, nina imani tutakapofika katika suala zima la Sheria ya Kodi ambayo mwisho wa siku Waziri wa Fedha ata-table hapa mezani, tutakuwa tumefika mahali muafaka na kupewa maelekezo ya kutosha nini tunataka tufanye. Lengo kubwa ni kwamba Serikali iweze kukusanya kodi ya kutosha na miradi ya maendeleo iweze kufanikiwa.