Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 32 2016-04-22

Name

Salma Mohamed Mwassa

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALMA M. MWASSA aliuliza:-
Miongoni mwa changamoto zinazokwamisha kuleta tija katika ukusanyaji wa kodi kwenye Halmashauri zetu ni pamoja na ubutu wa Sheria Ndogo Ndogo (By laws):-
Je, ni lini sheria hizo zitarekebishwa ili zilete tija katika ukusanyaji kodi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Salma Mohamed Mwassa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Sheria Ndogo katika Halmashauri zinatungwa chini ya Sura Namba 290 ya Sheria za Fedha za Serikali za Mitaa ambayo imewekwa sharti la faini isiyozidi shilingi 50,000/= na kifungo kisichozidi miezi mitatu au miezi sita au vyote kwa pamoja kutegemea na aina ya kosa ambalo mtu amefanya. Hivyo, kukosa umadhubuti kwa sheria ndogo hizi ni kutokana na masharti yaliyomo katika Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa inayotumika kwa sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya Rais (TAMISEMI) imeandaa mapendekezo ya marekebisho ya Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa Sura Namba 290 ambayo yatawasilishwa hapa Bungeni ili Bunge lako liweze kuijadili na kuridhia. Lengo letu siyo kuwaumiza wananchi, bali kuongeza umadhubuti wa Sheria za Serikali za Mitaa na hatimaye kuzipa makali Sheria Ndogo za Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kukuza mapato ya Halmashauri.