Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa Pori Tengefu la Loliondo uliodumu zaidi ya miaka 25?

Supplementary Question 1

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.
Je, Serikali baada ya kupata repoti iliyoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha kuhusu Pori Tengefu la Loliondo inampango gani wa kutoa suluhu ya kudumu kwenye mgogoro huu uliodumu zaidi ya miaka 20?
Swali la pili, je, Serikali inaweza kuahidi nini juu ya mgogoro huu wananchi wa Loliondo ili waweze kuendelea na kazi zao? (Makofi)

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Catherine Magige Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Arusha ambaye kwa kweli licha ya swali hili amekuwa akifuatilia kwa karibu sana juu ya masuala yanayohusiana na changamoto za Pori la Loliondo moja kwa moja akija kuhoji ofisini, lakini kuhusu maswali yake mawili ya nyongeza yote yanafanana kwamba hatua ambayo Serikali inaenda kuchukua ili kuwawezesha wananchi wa maeneo haya waweze kuendelea na shughuli zao kama ambavyo ameuliza.
Mheshimiwa Spika, Kama ambavyo nimejibu katika swali langu la msingi kamati iliyoundwa imefanya kazi kubwa ya kina kazi ambayo imezingatia maslahi ya pande zote upande wa wananchi lakini pia upande wa maslahi ya Taifa, lakini kwa kuwa ile ni taarifa ambayo ni ya kitaalam lakini pia iliyozingatia kama nilivyosema maslahi ya pande zote na kwa kuwa nimesema tayali iko kwenye dawati la Mheshimiwa Waziri Mkuu basi nimuombe Mheshimiwa Mbunge avute subira Waziri Mkuu bila shaka atakuwa anaipitia kwa kutumia wataalam chini ya ofisi yake baada ya pale taarifa itakayotolewa itakuwa na maelekezo ya namna gani tunaweza kusonga mbele katika kutatua mgogoro huu. (Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa Pori Tengefu la Loliondo uliodumu zaidi ya miaka 25?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, asante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa kuna kampuni ya OBC ambayo inamirikiwa
na mwarabu na imekuwa ikiwepo Loliondo kwa muda mrefu na wamekuwa wakifanya uwindaji, wamekuwa wakiangalia maslahi yao zaidi bila kuangalia maslahi mapana ya uhifadhi wa Bonde Tengefu la Loliondo. Ni kwa nini Serikali inamshirikiali au inamaslahi gani na huyu mwarabu amekaa huko kwa muda mrefu?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kama ambavyo ulipata mashaka, lakini na mimi nilikuwa na mwelekeo huo huo, lakini hata hivyo kwa ajili tu ya kuweza kuboresha, niseme tu kwa kifupi kwamba kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, kamati iliyoundwa ile ya kitaalam ilihusisha makundi yote, wataalam lakini pia wawekezaji na wananchi. Unapohusisha makundi yote, basi kila jambo ambalo ni changamoto linajadiliwa kwa mapana na marefu wakati kamati ikiwa inafanya kazi. Ninaamini ndani ya taarifa ambayo iko kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu, mambo yote ambayo yanahusiana hasa na wawekezaji, na napenda hapa tutumie lugha sahihi ya kuwa-address wawekezaji, na nafikiri jambo la msingi ni kwamba hawa ni wawekezaji wana haki zao nchini wa mujibu wa sheria, lakini kama yapo yale ambayo ni changamoto na yanatakiwa kufanyiwa kazi, basi hiyo ndiyo kazi ambayo kamati imefanya. (Makofi)

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa Pori Tengefu la Loliondo uliodumu zaidi ya miaka 25?

Supplementary Question 3

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi, unapokuwa katika eneo la huyu mwekezaji Loliondo, unaambiwa welcome to etisalat Arabic network kwa maana kwamba unatumia mtandao wa huko Arabuni na tunafahamu nchi yetu kwa hapa Tanzania kuna mitandao mitano ikiwepo Halotel, Zantel, Tigo pamoja na Airtel na Vodacom.
Je, ningependa kufahamu sheria zinasemaje kwa sababu hawa waliopo wanatambulika na kuna kiasi kinachopatikana kwa Serikali kutokana na mapato ya mitandao hii, sasa je, kwa huyu ambaye anakuambia welcome to etisalat Arabic network naomba ufafanuzi kutoka kwa Mheshimiwa Naibu Waziri. Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, mtandao huu anaousema umesajiliwa na TCRA na unasimamiwa na TCRA na unalipa ada zote zinazotakiwa zilipwe chini ya TCRA, tofauti yake tu ni kwamba wao hawajapanua mtandao wao ukaenda na maeneo mengine. Kwa hiyo, wao wamechukua masafa na masafa hayo yanafanya kazi katika lile eneo na inaruhusiwa kisheria, ni mtandao ambao unasimamiwa na nchi yetu.