Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 40 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 327 2017-06-02

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa Pori Tengefu la Loliondo uliodumu zaidi ya miaka 25?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALI: alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Catherine Valentine Magige, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, mwezi Desemba, 2016 Mheshimiwa Waziri Mkuu alipofanya ziara katika Wilaya ya Ngorongoro pamoja na mambo mengine, alitoa maelekezo ya jinsi ya kupata ufumbuzi wa mgogoro wa matumizi ya ardhi katika Pori Tengefu Loliondo ambao unahusisha wananchi, wawekezaji na wahifadhi. Katika utekelezaji wa agizo hilo, Kamati Maalum Shirikishi inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha iliundwa ili kupata mapendekezo ya namna ya kutatua mgogoro huo. Kamati hiyo maalum ilifanya kazi yake kwa njia mbalimbali zikiwemo kufanya vikao na wadau mbalimbali, kutembelea eneo lenye mgogoro ili kujua hali halisi na kuandaa taarifa yenye mapendekezo ya jinsi ya kutatua mgogoro husika. Mapendekezo ya Kamati hiyo yamewasilishwa kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa hatua zaidi.