Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali katika Wilaya mpya ya Wanging’ombe?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Wanging’ombe wametumia nguvu kubwa sana kujenga zahanati na vituo vya afya vilivyopo kule Mdandu, Saja, Ilembula na maeneo mengine. Je, Serikali itapeleka lini pesa ili vituo hivyo vya afya na zahanati viweze kumalizika ujenzi?
Swali langu la pili, kule Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Jimbo la Lupembe wananchi wamejitolea ekari 52 za kuweza kujenga hospitali; je, Serikali pia inafikiria lini itaanza ujenzi wa hospitali ndani ya Halmashauri ya Njombe?(Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, kwanza naomba nimpongeze Mbunge kwa initiative kubwa sana ya Mkoa wake wa Njombe. Nafahamu kwamba Wanging’ombe tunatumia Hospitali ya Ilembura kama DDH kwa ajili ya Wananchi kupata huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge ndiyo maana katika mwaka huu wa fedha mnafahamu kwamba zile fedha ambazo nyuma zilikuwa hazipatikani za Local Government Development Grants ambazo zilikuwa zinaenda kusaidia hii miradi ya mabomba na ujenzi ulioanza, mwaka huu sasa zimeweza kutoka. Ninashukuru sana Halmashauri mbalimbali wameelekeza fedha hizo hasa katika kumalizia viporo vya zahanati, vituo vya afya, sehemu zingine na madarasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo naomba nimuagize Mkurugenzi wa Wanging’ombe na Baraza la Madiwani kwamba mpaka mwezi wa sita tutaendelea kutoa fedha zingine mpaka ziweze kukamilika katika bajeti yetu ya mwaka huu, zikija kule lazima zingine wazielekeze katika kuhakikisha hizi zahanati na vituo vya afya katika eneo la Wanging’ombe zimefanyiwa kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo katika Halmashauri ya Njombe kama ulivyosema ni kweli jambo hilo limejitokeza mara kadhaa hapa katika Bunge hili na eneo limeshatengwa. Naomba niwahakikishe kwamba Halmashauri kwa kadri itakavyoibua katika bajeti yake mpango wa bajeti wa Serikali katika Halmashauri husika na Ofisi ya TAMISEMI tutashirikiana nao.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo letu kubwa ni kwamba kila Halmashauri kuwe na hospitali ya Wilaya ili wananchi waweze kuhudumiwa katika eneo hilo. Kwa hiyo, Serikali iko tayari kushirikiana na wananchi wa Njombe kuhakikisha katika mipango yetu hii tunafanikisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Njombe ili wananchi waweze kupata huduma vizuri. (Makofi)

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali katika Wilaya mpya ya Wanging’ombe?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa Wilaya mpya nyingi hazina Hospitali za Wilaya ikiwemo na Wilaya yangu ya Tanganyika; ni nini mkakati wa Serikali wa kuweza kujenga hospitali sambamba na kuimarisha vituo vya afya wakati inajipanga kujenga hospitali hizo za Wilaya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mheshimiwa Moshi pale kwake wanahudumiwa na Hospitali ya Halmashauri ya Mpanda iko Mpanda Mjini na Makao Makuu ya Wilaya ya Tanganyika Majarila na eneo lingine lote mpaka unaenda ziwani, wananchi wanapata shida kubwa sana. Mheshimiwa Mbunge unakumbuka tulivyokuwa Jimboni kwako tumeenda mpaka katika Makao Makuu ya Halmashauri yako ambayo inatarajiwa kujengwa hivi sasa na miongoni mwa jambo ulilolipendekeza ni kwamba tufanye utaratibu wa kuboresha kile kituo cha afya cha Majarila.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikuhakikishie kwamba, Serikali sasa imetenga takribani shilingi milioni 700 kupeleka katika eneo lako, lengo kubwa ni kuwasaidia wananchi wako ambao wanachangamoto kubwa ya kiafya. Serikali imesikia sana kilio cha wananchi wa Tanganyika na Serikali iko tayari nadhani katika kipindi hiki kuanzia mwezi huu wa Mei mpaka tutakapofika mwezi wa Julai ni imani yangu kubwa tutapeleka nguvu kubwa sana kujenga theatre na kuweka vifaa vyote vya wazazi ili tupunguze vifo vya mama na watoto tuweze kuvipunguza katika eneo lako. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali katika Wilaya mpya ya Wanging’ombe?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Mji wa Tarime ina Hospitali ambayo ni Hospitali ya Mji, lakini inahudumia Wilaya nzima, ningetaka kujua ni lini Serikali itajenga Hospitali kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Tarime wakati inasubiria kujenga, iipe ile hadhi kama Hospitali ya Wilaya na kuweza kuleta mahitaji kama inavyotakiwa kwa idadi wa watu wa Tarime nzima na siyo Halmashauri ya Mji tu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kesi anayoizungumzia Mheshimiwa Esther hapa inafanana na ya ndugu yangu Mheshimiwa Chumi, tuna Halmashauri zile za Mji na Halmashauri za Wilaya, kwa bahati mbaya ukiangalia Tarime Halmashauri ya Mji ndiyo ina hospitali, Halmashauri ya Wilaya haina hospitali na bajeti mnayopata ni ndogo, hali kadhalika ukiangalia Mufindi na Mafinga, Mafinga kuna Hospitali ya Wilaya bajeti ikienda inakuwa ndogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimepita maeneo mbalimbali niliwapa maelekezo watu, kwa nini maeneo ambayo hakuna Hospitali ya Wilaya kama kuna hospitali zingine zile za mission tunaweka DDH na tunapeleka funds pale kwa nini kunapokuwa kwa mfano katika Halmashauri ya Tarime kuna Hospitali ya Wilaya, kwa nini watu wa Halmashauri ya Wilaya pale, fedha tunazozipeleka ambao wana bajeti kubwa sana wasielekeze fedha zingine kwa ajili ya kununua dawa na vifaa tiba katika Halmashauri ya Mji.
Mheshimiwa Naibu Spika, hili ni jambo nadhani hasa Wakurugenzi wetu katika maeneo husika na viongozi mliopo huko tuangalie haja ya wananchi wetu kuweza kuwahudumia, hili ni jambo kubwa na shirikishi. Kwa hiyo, naomba niagize, katika maeneo ambayo yana scenario kama hii, lazima viongozi mkae muangalie ni jinsi gani tutafanya tuweze kuhudumia eneo hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, nakuunga mkono Mheshimiwa Esther Matiko ni jambo lenye mantiki na lina busara zaidi, naomba maagizo haya yachukuliwe sehemu zote kama ni jambo la kujifunza, nini tufanye tuwasaidie wananchi wetu katika suala la afya. (Makofi)

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali katika Wilaya mpya ya Wanging’ombe?

Supplementary Question 4

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kituo cha afya cha Manonga jengo lake la upasuaji limekamilika; na kwa kuwa mpaka sasa hakifanyi kazi, je, Serikali ni lini, itapeleka vifaa vya upasuaji katika kituo hicho cha afya? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tuna tatizo katika kituo cha afya cha Manonga, pia tulikuwa na tatizo hili katika vituo vya afya mbalimbali ambapo tulivijenga kupitia mradi wa ADB, bahati nzuri tumepata mafanikio katika Mkoa wako katika kituo cha afya cha Itobo na Bukene vimeshaanza kufanya kazi, Manonga pale vifaa vilikuwa bado havijakamilika. Hivi sasa tunaendelea kuangalia ni jinsi gani tufanye kwa sababu pale kulikuwa na mapungufu ambayo yalijitokeza huku, katika suala zima mchakato wa ujenzi ule kuna mambo mengine hayakwenda sawa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inalichukua hili tuangalie nini tufanye ili kituo cha afya cha Manonga kiweze kukamilika vizuri kuwa na vifaa pale na wananchi wa eneo lile wajisikie kwamba wana viongozi wao Mbunge wao Mheshimiwa Mwanne Mchemba na Mheshimiwa Gulamali wanawawakilisha huku. Sasa Serikali tumelichukua hili kwa ajili ya kulifanyia kazi. (Makofi)