Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 23 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 193 2017-05-12

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali katika Wilaya mpya ya Wanging’ombe?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema William Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe imeanza maandalizi ya awali ya kuanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya kwa kutenga eneo la ekari 60 katika kijiji cha Igwachanya ambalo limetolewa na wananchi bila kuhitaji fidia. Katika mwaka wa fedha 2016/2017 Halmashauri imepanga kutumia shilingi milioni 35 kwa ajili ya kupima eneo hilo na kuliweka mipaka.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2017/2018 zimetengwa shilingi milioni 24 kupitia mapato ya ndani kwa ajili ya maandalizi ya awali ili kuanza ujenzi. Serikali itaendelea kushirikiana na Halmashauri katika kusukuma vipaumbele vilivyoainishwa na Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe sambamba na kutafuta fedha ili kufanikisha huduma ya afya kwa wananchi wa Wanging’ombe.