Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA aliuliza:- Polisi wamekuwa wakifanya msako na kamatakamata ya waganga wa kienyeji sehemu nyingi hapa nchini:- (a) Je, ni waganga wangapi wa kienyeji walikamtwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu? (b) Je, ni waganga wa kienyeji wangapi walifikishwa Mahakamani na kutiwa hatiani katika kipindi hicho katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu?

Supplementary Question 1

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali madogo ya nyongeza. Namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri na pia nimshukuru kwa kutupa Kituo cha Wilaya cha Polisi katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Sheria Na.23 ya mwaka 2002 inatoa fursa kwa msajili kwa ajili ya kusimamia hawa waganga wa tiba asili na tiba mbadala lakini kwa kuwa kamatakamata hii imesababishwa na wale waganga wasio waadilifu na hawajasajiliwa ambao kimsingi wamesababisha kuwa na mgongano na kusababisha mauaji ya vikongwe. Kwa mfano, katika Halmashauri ya Ushetu kuna watu 25 wameuawa katika kipindi cha mwaka 2012 na 2017.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kwa kuwa, kamatakamata hii inaleta usumbufu kwa waganga wanaofanya shughuli hii kihalali, je, Serikali imejipangaje kuliimarisha Baraza hili la Tiba Asili au Tiba Mbadala ili lishirikiane na vyombo vingine kama polisi na kuwaondoa kabisa waganga wanaowachonganisha wananchi na kuwalinda vikongwe hawa dhidi ya mauaji? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni lini Serikali itafungua vituo vya usajili mikoani ili kurahisisha usajili na kudhibiti waganga hawa na kuweza kushughulikia kabisa wasiokuwa na sifa na kuboresha huduma hii? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli utaratibu wa kusajili waganga wa kienyeji ambao kimsingi wanasajiliwa na Wizara ya Afya na Maendeleo ya Jamii, Wazee na Watoto, baada ya mganga kuthibitishwa na Baraza hilo ndipo anapatiwa usajili, kwa hiyo, ni utaratibu mzuri tu. Kupitia utaratibu huu na mabaraza haya, nishauri waganga wote ambao wanajishughulisha na tiba asili kujisajili kisheria ili waweze kutambulika kihalali. Nina hakika watakapofanya hivyo hata kazi ya Jeshi la Polisi kuwabaini waganga wachochezi wanaopiga ramla chonganishi itakuwa ni nyepesi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na hoja ya kupeleka vituo hivi vya usajili mikoani, nadhani ni wazo zuri na kama Serikali tutalichukua na tutalifanyia kazi.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA aliuliza:- Polisi wamekuwa wakifanya msako na kamatakamata ya waganga wa kienyeji sehemu nyingi hapa nchini:- (a) Je, ni waganga wangapi wa kienyeji walikamtwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu? (b) Je, ni waganga wa kienyeji wangapi walifikishwa Mahakamani na kutiwa hatiani katika kipindi hicho katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kutambua uwakilishi wangu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa muda mrefu nimekuwa nikisikia Wabunge wanalalamika na kuwatetea sana wasanii pindi wanapopata matatizo kwamba tunawatumia kwenye chaguzi lakini baada ya chaguzi hatuwasaidii. Hata hivyo, waganga wa kienyeji kwa karama niliyonayo nikiangalia humu ndani wakati wa uchaguzi wawili, watatu hamkupita kwao labda Mzee Selasini...
Na siyo Wabunge peke yake ni jamii nzima na waganga hawa baada ya chaguziā€¦
Sawa Mheshimiwa Spika. Waganga hawa baada ya chaguzi tunawatelekeza na kuwatumia Polisi.
e, Serikali haioni umuhimu wa kujenga chuo cha kuwasaidia waganga hata kama ni kwa elimu ndogo? (Makofi)

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Musukuma kwa swali lake la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba nchi yetu inathamini na kuheshimu kazi za waganga wa asili na ndiyo maana tumepitisha Sera ya Waganga wa Asili na Tiba Mbadala ya 2002 lakini pia kanuni. Lengo la sera hii ni kuendeleza tiba asili na tiba mbadala kwa sababu ni kweli asilimia 60 ya Watanzania wanatumia huduma za waganga wa tiba asili na tiba mbadala.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, siyo tu kujenga chuo lakini tunalo pia Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala ambalo linafanya mafunzo ya mara kwa mara kwa waganga wetu especial katika kuhifadhi dawa zao na kufanya ufumbuzi. Sasa hivi tumeweka mfumo mzuri wa kuwasajili waganga wetu, tumewateua ma-DMO wote kuwa ni wasajili wasaidizi kwa ajili waganga wetu wa asili na tunaendelea kuwaenzi kwa sababu wana mchango mkubwa sana katika kutatua huduma za afya kwa wananchi. (Makofi)