Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 21 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 184 2017-05-10

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA aliuliza:-
Polisi wamekuwa wakifanya msako na kamatakamata ya waganga wa kienyeji sehemu nyingi hapa nchini:-
(a) Je, ni waganga wangapi wa kienyeji walikamtwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu?
(b) Je, ni waganga wa kienyeji wangapi walifikishwa Mahakamani na kutiwa hatiani katika kipindi hicho katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Elias John Kwandikwa, Mbunge wa Ushetu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, waganga wa kienyeji waliokamatwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu ni 26 na kushtakiwa kwa makosa ya kufanya biashara ya uganga bila kibali na kupatikana na nyara za Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha mwaka 2010 hadi 2015 jumla ya waganga 16 walikamatwa na kufikishwa Mahakamani. Kati ya hao, waganga saba walipatikana na hatia kwa kufungwa miaka miwili kila mmoja au kulipa faini ambapo jumla ya watuhumiwa sita katika kesi tofauti walilipa faini ya jumla ya Sh.1,250,000/=. Mtuhumiwa wa kesi moja alihukumiwa miaka miwili bila yeye kuwepo Mahakamani, juhudi za kumsaka zinaendelea.