Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Serikali imefanikiwa kupeleka umeme katika Wilaya ya Mbogwe kupitia Electricity V na REA lakini huduma hii haijawafikia wananchi walio wengi; Je, ni lini Serikali itaongeza usambazaji wa huduma hiyo muhimu kwa wananchi wengi walio tayari kulipia gharama za kufungiwa umeme katika nyumba zao hususan katika Miji ya Masumbwe na Lulembela?

Supplementary Question 1

MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kuipongeza Serikali kwa kazi nzuri sana ambayo imefanyika katika Jimbo la Mbogwe la kusambaza umeme maeneo mengi. Sasa naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza, ni lini sasa Serikali itapeleka umeme katika Kata Nyasato, Bunigonzi na Vijiji vyote vya Jimbo la Mbogwe ambavyo bado havijapa huduma hii ya umeme?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni lini sasa mradi wa REA awamu ya tatu utaanza katika Mkoa wa Geita na Wilaya ya Mbogwe in particular? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Masele kwa sababu ameshughulikia sana masuala ya umeme katika jimbo lake ambapo kati ya vijiji 72, vijiji 44 vyote vimeshapatiwa umeme. Hongera sana Mheshimiwa Masele.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie vijiji vyote vilivyobaki, ameuliza suala la msingi sana ni lini sasa umeme utapelekwa katika Kata za Nyasato pamoja na Budigonzi. Nimhakikishie Mheshimiwa Masele kwa niaba ya wananchi wa Mbogwe, ni vijiji vyote 28 sasa tunavipelekea, Vijiji hivyo ni pamoja na Budigonzi, Buzigozigo, Mtakuja, Budura pamoja na maeneo mengine ya Kashenda na Nyashimba, yote yatapelekewa umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini tunazindua Mkoa wa Geita? Nipende kuliambia Bunge lako Tukufu kwamba tumeanza kuzindua utekelezaji wa mradi wa awamu ya tatu tangu tarehe 24 mwezi huu na tumeanza na Mkoa wa Manyara. Katika Mkoa wa Manyara tumefanya katika Jimbo la Babati na mengine. Tarehe saba na nane tunazindua katika Mkoa wa Kagera, tutakwenda katika Wilaya ya Karagwe. Tarehe 10 tutazindua katika Mkoa wa Geita Mheshimiwa Mbunge; na maeneo ya kuzindua ni maeneo ya Nyangh’wale pamoja na maeneo ya Mbogwe. Kwa hiyo niwahakikishie wananchi wa Mbogwe, wananchi wa Mkoa wa Geita na Wabunge wote wa Mkoa wa Geita basi tushirikiane wote tarehe 8 na 10 tutakapokuwa tunazindua katika Mkoa wa Geita.

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Serikali imefanikiwa kupeleka umeme katika Wilaya ya Mbogwe kupitia Electricity V na REA lakini huduma hii haijawafikia wananchi walio wengi; Je, ni lini Serikali itaongeza usambazaji wa huduma hiyo muhimu kwa wananchi wengi walio tayari kulipia gharama za kufungiwa umeme katika nyumba zao hususan katika Miji ya Masumbwe na Lulembela?

Supplementary Question 2

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Nataka niulize Serikali kwa kuwa katika Mkoa wa Mbeya, REA III imezinduliwa tayari na mkandarasi yupo aliyeanzia Wilaya ya Rungwe. Sasa ni lini huyo mkandarasi atakwenda Wilaya ya Chunya ili akapeleke umeme kwenye Kata zilizobaki za Ifumbo, Kasanga, Nkunungu, Lwalaje, Kambi Katoto na Mafyeko?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Mheshimiwa Mwambalaswa nampongeza sana, hata tulipokwenda kule ni kwa sababu pia alishirikiana na sisi sana kwa hiyo hongera kwa kazi hiyo. Nimhakikishie kwa niaba ya wananchi wake; ni kweli kabisa katika Kijiji cha Ifumbwe pamoja na Kasanga bado hatujaenda; lakini tarehe 17 mwezi huu mkandarasi atakuwa kwenye Kijiji cha Kasanga katika jimbo lake. Kwa hiyo, katika maeneo mengine yataendelea kufanya kazi hiyo hiyo na niwaombe sana Wabunge wa Mkoa wa Mbeya tushirikiane kwa kazi hiyo kwa sababu mkandarasi tayari ameshaingia mkoani.

Name

Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Serikali imefanikiwa kupeleka umeme katika Wilaya ya Mbogwe kupitia Electricity V na REA lakini huduma hii haijawafikia wananchi walio wengi; Je, ni lini Serikali itaongeza usambazaji wa huduma hiyo muhimu kwa wananchi wengi walio tayari kulipia gharama za kufungiwa umeme katika nyumba zao hususan katika Miji ya Masumbwe na Lulembela?

Supplementary Question 3

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tatizo la Mbogwe ni sawa na tatizo lililoko katika Mkoa wa Mara hasa Musoma Vijijini. Naomba Mheshimiwa Naibu Waziri atuhakikishie kwamba ni lini wananchi wa Musoma Vijijini watapata umeme wa REA?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa, tulipokwenda katika Mkoa wa Mara wakati tunazindua Mheshimiwa Mbunge alitupa support kubwa sana. Hongera sana pamoja na Wabunge wote wa Mkoa wa Mara; lakini ni lini sasa umeme vijiji hivyo vitapelekewa; tumeshaanza na kuja kufikia mwezi ujao wakandarasi watakuwa wameingia vijiji 42 katika Mkoa wa Mara na vijiji vilivyokuwa vimebaki vitakamilika sasa ifikapo mwaka 2020. Hata hivyo, si kwenye vijiji tu na vitongoji vyote Mheshimiwa Sokombi, Taasisi zote za Umma, Makanisa na Misikiti pamoja na visiwa ambavyo viko Mkoa wa Mara.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Serikali imefanikiwa kupeleka umeme katika Wilaya ya Mbogwe kupitia Electricity V na REA lakini huduma hii haijawafikia wananchi walio wengi; Je, ni lini Serikali itaongeza usambazaji wa huduma hiyo muhimu kwa wananchi wengi walio tayari kulipia gharama za kufungiwa umeme katika nyumba zao hususan katika Miji ya Masumbwe na Lulembela?

Supplementary Question 4

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibnu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa, Serikali inaendelea kufanya kazi nzuri kupitia miradi ya REA, lakini nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba yako maeneo mengine kwenye miji na majiji bado yanazo sura za vijiji; kwa mfano kwenye Jimbo la Nyamagana iko mitaa inafanana kabisa bado na maeneo ya vijijini kama Fumagila, Rwanima, Isebanda, Kakebe na maeneo mengine kama Nyakagwe. Ni lini Serikali itakuwa na utaratibu wa kuhakikisha na maeneo haya yanapatiwa umeme wa REA ili yaweze kupata sawasawa na mengine? Ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Mabula. Wakati ananiletea vijiji hivi tulipozungumza aliniletea vijiji vingine ambavyo vilikuwa kwenye hali ya kimtaa, lakini kisura vinaonekana kivijiji na tumeviingiza kwenye Mradi wa REA. Katika vijiji ambavyo ametaja hivi ambavyo inaonekana viko mjini, kwanza kabisa kuna mradi ambao unapeleka umeme kwenye miji yote nchi nzima na mradi huu unaitwa Urban Electrification na utapeleka katika miji na mitaa 314 kwa nchi nzima. Kwa hiyo, hata vijiji au mitaa ambayo iko mijini bado itapelekewa umeme kwa utaratibu huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, tutakaa katika vijiji ambavyo amesema vya Fumagila pamoja na Kakene tuone hali itakavyokuwa. Nimwombe sana mara baada ya hapa tukutane na Mheshimiwa Mabula ili ikiwezekana vijiji hivi vipelekewe katika Mradi wa REA.

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Serikali imefanikiwa kupeleka umeme katika Wilaya ya Mbogwe kupitia Electricity V na REA lakini huduma hii haijawafikia wananchi walio wengi; Je, ni lini Serikali itaongeza usambazaji wa huduma hiyo muhimu kwa wananchi wengi walio tayari kulipia gharama za kufungiwa umeme katika nyumba zao hususan katika Miji ya Masumbwe na Lulembela?

Supplementary Question 5

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kutokana na mauaji yanayoendelea Wilayani Kibiti bado tunahitaji umeme. Je, Serikali ina mpango gani kupeleka umeme katika vijiji vilivyobakia?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze nilienda kwake na tulitembea sana mpaka kwenye Kijiji cha Jaribu Mpakani na tulipeleka umeme Jaribu Mpakani. Hata hivyo, Serikali imekusudia kuangaza umeme vijiji vyote nchi nzima. Napenda nitoe nafasi hiyo kwa sababu, Mheshimiwa Ungando tumeshirikiana sana, lakini niseme tu vijiji vyote vya Jimbo la Kibiti vitapelekewa umeme sasa kupitia Mradi wa REA; hadi kufikia mwaka 2021 vijiji vyake vyote vya Kibiti vitakuwa vimeshapata umeme. (Makofi)

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Serikali imefanikiwa kupeleka umeme katika Wilaya ya Mbogwe kupitia Electricity V na REA lakini huduma hii haijawafikia wananchi walio wengi; Je, ni lini Serikali itaongeza usambazaji wa huduma hiyo muhimu kwa wananchi wengi walio tayari kulipia gharama za kufungiwa umeme katika nyumba zao hususan katika Miji ya Masumbwe na Lulembela?

Supplementary Question 6

MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa, Mkoa wa Mtwara na Lindi ndiyo mikoa ambayo ina vijiji vingi sana ambavyo havijapatiwa umeme. Je, ni lini mikoa hii itapewa kipaumbele maalum ili vijiji vingi viweze kupata umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni kweli kabisa Mikoa ya Mtwara na Lindi maeneo mengi hayajafikiwa na miundombinu ya umeme. Nimhakikishie Mheshimiwa Bwanausi na namshukuru sana, alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini hapo nyuma, tumeshirikiana sana na amefanya kazi kubwa kwenye jimbo lake, naomba nimpongeze kwa hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, tumeipa kipaumbele kikubwa sana mikoa hii miwili. Tarehe 15 hadi tarehe 18 tutakuwa tunafanya kazi ya kuzindua na kuelekeza Wataalam wetu wa TANESCO kupeleka umeme katika mikoa hii miwili, hilo la kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili; tunarekebisha miundombinu ya Mtwara. Hivi sasa tunajenga transmission line ya kutoka Mtwara umbali wa kilometa 80 na umeme wa KVA 132, ili umeme huo upelekwe Mtwara Mkoa mzima na maeneo mengine ya Lindi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Bwanausi Serikali imetumia hatua kubwa sana na imegharimu shilingi bilioni mia nane sabini na nane kufanya kazi hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Bwanausi, lakini nampa uhakika kwamba, Serikali inaipa vipaumbele sana Mikoa ya Lindi na Mtwara na mwaka 2020 na 2021 vijiji vyote vya Mtwara na Lindi vitakuwa vimepata umeme.