Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 58 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 481 2017-07-03

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:-
Serikali imefanikiwa kupeleka umeme katika Wilaya ya Mbogwe kupitia Electricity V na REA lakini huduma hii haijawafikia wananchi walio wengi; Je, ni lini Serikali itaongeza usambazaji wa huduma hiyo muhimu kwa wananchi wengi walio tayari kulipia gharama za kufungiwa umeme katika nyumba zao hususan katika Miji ya Masumbwe na Lulembela?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Manyanda Masele, Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa Mradi kabambe wa usambazaji umeme vijijini awamu ya tatu umeanza nchi nzima tangu Mwezi Machi, 2017. Mradi huu utajumuisha vipengele-mradi vitatu vya Densification, kwa maana ya vitongoji, Grid Extention kwa maana ya vijiji vyote pamoja na Off- Grid Renewable katika maeneo ya visiwa. Mradi huu unalenga kuongeza wigo wa usambazaji umeme katika vijiji vyote ambavyo havijafikiwa na umeme ikiwa ni pamoja na vitongoji vyote nchi nzima, taasisi zote za umma, mashine za maji pamoja na visiwa vyote nchi nzima.
Mheshimiwa Naibu Spika, Miji ya Lulembela na Masumbwe imewekwa katika utekelezaji wa mradi wa REA awamu ya tatu utakaokamilika mwaka 2020/2021.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya kupeleka umeme katika Miji ya Masumbwe unaojumuisha vijiji vya Budoda, Ilangale, Masumbwe, Nyakasaluma na Shenda; na katika Lulembela unaojumuisha Vijiji vya Bugomba, Kabanga, Kashelo, Mtakuja, Nyikonga pamoja na maeneo mengine. Ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti utapelekwa kwenye maeneo yote yenye urefu wa kilometa 38.7; ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 110; ufungaji wa transfoma 20; pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wapya 678. Kazi hii itakamilika mwaka 2020/2021 na itagharimu shilingi bilioni 5.18.