Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Salma Mohamed Mwassa

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALMA M. MWASSA aliuliza:- Kumekuwa na mrundikano wa wagonjwa kwenye Hospitali za Mwananyamala, Temeke na Amana:- Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya mpya katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Supplementary Question 1

MHE. SALMA M. MWASA: Ahsante Mheshimiwa Naibu Spika, naomba urekebisa kidogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza swali langu lilikuwa ni Hospitali za Wilaya za Ubungo na Kigamboni, lakini hapa naona limekuja la Kigamboni peke yake. Sasa maswali yangu ya nyongeza ni mawili. La kwanza, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya kwenye Wilaya mpya ya Ubungo?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je, ni lini Serikali tena itapandisha hadhi kituo cha afya cha Mbezi? Kama huu mchakato wa kujenga Hospitali ya Wilaya utachukua muda basi ipandishe Hospitali ya Mbezi iwe Hospitali ya Wilaya.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli na tunafahamu hizi Kigamboni pamoja na Ubungo ni Wilaya mpya, zimezaliwa kutoka katika Wilaya mama ya Temeke na Wilaya Kinondoni, tukifahamu kwamba Wilaya ya Ubungo ina changamoto hiyo. Kwa hiyo, jambo la msingi ni kwamba, kwa sababu tumegawanyika si muda mrefu sasa niombe Baraza la Madiwani la Ubungo pamoja na timu yote ya Management wafanye utaratibu wa kuandaa hii mipango ya ujenzi wa hospitali mpya ya Ubungo na sisi Serikali katika nafasi yetu tutafanya kila liwezekanalo ili kuhakikisha kwamba eneo la Ubungo linakuwa na hospitali yake kwa sababu tunajua kwamba population ya watu wa Ubungo ni kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo kupandisha hadhi kituo cha Mbezi kwa hivi sasa kiweze kutumika, kikubwa zaidi nimuagize Mkurugenzi pamoja na Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ubungo kwamba kama wakiona kinatosha waanze kuhakikisha tunaanza harakati za kwanza kukiwezesha kituo hiki kama tulivyofanya kituo cha Vijibweni pale Kigamboni. Tukifanya hivi tutaweza kusaidia kwa kiwango kikubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwasihi hasa Mkurugenzi na DMO wetu, waweze kufanya harakati za haraka na kufanya analysis ya kutosha nini kinaweza kufanyika pale ili kuweza kuongeza tija katika Sekta ya Afya katika wilaya ambayo Mheshimiwa Mbunge anaipigania sana.

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALMA M. MWASSA aliuliza:- Kumekuwa na mrundikano wa wagonjwa kwenye Hospitali za Mwananyamala, Temeke na Amana:- Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya mpya katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Supplementary Question 2

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Baada ya kupandishwa hadhi Zahanati ya Likombe katika Manispaa ya Mtwara Mikindani kuwa Hospitali ya Wilaya kumekuwa na changamoto kubwa sana ya mrundikano wa wagonjwa hasa katika wodi ya wazazi. Je, ni lini Serikali itapanua wodi ile ili akinamama wale waweze kusitirika wakati wanatimiza haki yao ya msingi kama wanawake?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, population ya Mtwara Mikindani sasa hivi imekuwa kubwa kutokana na kuingiliana na mambo ya gesi. Hata hivyo, hivi sasa tunaenda katika harakati za kufanya ukarabati wa vituo vipatavyo 142. Zoezi hili haliishi hapa; Serikali inajielekeza tena kupanua vituo vingine vipya ambako kuna population kubwa. Kituo hiki ambacho Mheshimiwa Mbunge amekizungumzia hapa tutakichukua kama sehemu ya kipaumbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la Serikali ya Awamu ya Tano ni kufanya commitment katika kuwahudumia wananchi. Kwa hiyo, hii tutaweka ni sehemu ya kipaumbele kuwahudumia wananchi wa Mikindani ili waweze kupata afya bora katika maeneo yao.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. SALMA M. MWASSA aliuliza:- Kumekuwa na mrundikano wa wagonjwa kwenye Hospitali za Mwananyamala, Temeke na Amana:- Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya mpya katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Changamoto ya huduma ya afya iliyopo Kigamboni na Ubungo inafanana na ile iliyopo Jimbo la Nanyamba ambako hakuna kituo cha afya hata kimoja, hakuna hospitali ya wilaya, hakuna ambulance na hakuna DMO (Mganga Mkuu wa Wilaya). Sasa nataka kujua Serikali ina mpango gani wa muda mfupi wa kutatua changamoto hizi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwamba Mheshimiwa Chikota tulikuwa wote site na tulifika eneo ambalo wao wameweka kipaumbele kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunakarabati eneo lile ili kupata kituo cha afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na ziara ile nimhakikishie Mheshimiwa Chikota kwamba Serikali imefanya commitment ya kutosha na pale muda si mrefu kuanzia sasa tutawekeza fedha nyingi takribani milioni mia saba katika kile kituo chake ambacho alikiwekea kipaumbele siku tulipofika pale. Kwa hiyo, naomba niwaambie wananchi wa Nanyamba kwamba Mbunge wao amepigana na Serikali imesikia na muda si mrefu tutakwenda kufanya uwekezaji mkubwa sana wa sekta ya afya katika eneo hilo.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. SALMA M. MWASSA aliuliza:- Kumekuwa na mrundikano wa wagonjwa kwenye Hospitali za Mwananyamala, Temeke na Amana:- Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya mpya katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Supplementary Question 4

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru nami niulize swali fupi. Hospitali yetu ya Makambako ilipandishwa hadhi tangu 2013 na kuwa hospitali kutoka kituo cha afya, lakini mgao wa dawa mpaka sasa tunapata kama kituo cha afya. Je, Serikali itakuwa tayari sasa kupeleka mgao kama ambavyo ilipandisha kuwa hospitali kwa sababu wataalam, Madaktari wapo na chumba cha kufanyia upasuaji kinaanza mwezi huu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, nilipofika pale jimboni kwake nikiwa naye ni miongoni mwa watu ambao wame-invest pesa zao binafsi kuwasaidia wananchi wao. Mheshimiwa Mbunge hongera sana katika hilo. Changamoto ya mgao wa dawa, kwamba bado unapata kwa mfumo wa kituo cha afya; wakati huo huo ikiwa kwamba Makambako ni center kubwa sana ya watu kutoka katika hizi barabara mbili; ya kutoka Ruvuma na kutoka Mbeya; tunajua ni changamoto kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kwamba eneo lile kwa bajeti ya mwaka huu tutaliangalia vizuri. Tutafanya kila liwezekanalo kumwongezea bajeti kwa sababu tunataka ile center ya upasuaji ifanye kazi vizuri. Hata hivyo, Serikali tutaangalia tufanyeje ili wananchi wa Makambako waweze kupata huduma vizuri. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba niseme kwamba Serikali imelisikia na itakwenda kulifanyia kazi jambo hili.

Name

Savelina Slivanus Mwijage

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALMA M. MWASSA aliuliza:- Kumekuwa na mrundikano wa wagonjwa kwenye Hospitali za Mwananyamala, Temeke na Amana:- Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya mpya katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Supplementary Question 5

MHE. SAVELINA S. MWIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwa kuwa Hospitali ya Wilaya ya Bukoba Vijijini, ni hospitali ya mission na leo hii walivyotoa ambulance imekwenda kwenye Zahanati ya Kishanje. Ni lini Serikali itapandisha hadhi Hospitali ya Mission ambayo tayari wameshakubali kuitoa Serikali, kuwa hospitali ya wilaya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MITAA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tumesikia lile suala la ambulance alilizungumza nadhani hii ni mara ya pili, kwamba maelekezo ilitakiwa iende katika kituo kingine na nimesema kwamba nitafika kule site kufanya verification, maagizo yalikuwaje na hii ambulance imeenda wapi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, kuhusu mchakato wa kuipandisha hii hospitali tutapitia mikataba, tutawasiliana na wenzetu wa Wizara ya Afya kuangalia nini kilichopo na jambo lipi ambalo ni rafiki zaidi tunaloweza kulifanya kwa mustakabali wa wananchi wa Bukoba. Kwa hiyo, tunachukua haya mawazo lakini lazima tufike field pale tuangalie uhalisia wa jambo lilivyo ili tupate majibu muafaka kusaidia wananchi wa Bukoba.