Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 58 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 479 2017-07-03

Name

Salma Mohamed Mwassa

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALMA M. MWASSA aliuliza:-
Kumekuwa na mrundikano wa wagonjwa kwenye Hospitali za Mwananyamala, Temeke na Amana:-
Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya mpya katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Salma Mohamed Mwassa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kigamboni, Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni imetenga eneo lenye ukubwa wa ekari 10 katika Kata ya Somangila kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali kubwa ya Wilaya ya Kigamboni. Ujenzi wa Hospitali hiyo unatarajiwa kufanywa na Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni kwa kushirikiana na wananchi na wadau mbalimbali ikiwemo Serikali ya Morocco. Kwa sasa Serikali inaendelea na mazungumzo na Serikali ya Morocco ili kuanza ujenzi huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Serikali inaendelea kuboresha Zahanati na vituo vya afya vilivyopo ambapo katika bajeti ya mwaka 2017/2018 zimetengwa shilingi milioni 557.3 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba pamoja na ujenzi wa vituo vya afya na zahanati.