Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Wilfred Muganyizi Lwakatare

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Bukoba Mjini

Primary Question

MHE. WILFRED M. LWAKATARE aliuliza:- Mji wa Manispaa ya Bukoba una vijiji ambavyo havina umeme kabisa na havikuingizwa katika mpango wa REA wa kusambaza umeme. Je, Serikali ina mpango gani wa kuvipatia umeme vijiji vya kata za Nyanga, Ijuganyondo na Kahororo ambavyo mazingira na hali ya kiuchumi haitofautiani na vijiji vilivyosambaziwa umeme katika wilaya nyingine vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. WILFRED M. LWAKATARE: Mheshimiwa Naibu Spika, nishukuru majibu mazuri kutoka kwa Mheshimiwa Waziri lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, Mheshimiwa Waziri atakubaliana na mimi kwamba mojawapo ya faida zilizomo katika mradi wa REA ambayo kawaida inaleta mvuto kwenye mradi huu ni pamoja na complementary au unafuu wa bei ambao wanapewa watu wanaosambaziwa umeme huo. Kwa mazoea ambayo yamezoeleka kwa umeme ambao unasambazwa na TANESCO ni kwamba bei za TANESCO zinakuwa kubwa kuliko zile bei au gharama za REA.(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nitaomba Mheshimiwa Waziri anihakikishie kwamba hizi fedha zilizotengwa kwa ajili ya TANESCO na kwa maeneo ambayo ameyazungumza, ikiwemo na vijiji vya Ijuganyundo B ambavyo havina umeme kabisa, maeneo ya Makongo kule Kahororo na maeneo ya Chaya kule Busimbe, hizi gharama pia za TANESCO zitakuwa complimented au itakuwa ni gharama zilezile za TANESCO ambazo zimekuwa kubwa na watu wa maeneo haya ambao hawana uwezo wasiweze kupata umeme?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili,...
Mheshimiwa Naibu Spika, nitaomba tu atajibu mojawapo atakaloliona linafaa kwenye…

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba baadhi ya vijiji ambavyo vinaonekana viko ndani ya mji vinapelekewa umeme kupitia Shirika la Umeme TANESCO na ni kweli kabisa bei ni tofuati, bei za TANESCO kwa wateja wa awali kabisa ni shilingi 177,000 na kwa upande wa REA ni shilingi 27,000.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Lwakatare kwa jinsi anavyofuatilia maslahi ya wananchi wa Bukoba Mjini, ni mdau mzuri, lakini tunamhakikishia kwamba tutafanya upembuzi kwa ukina kabisa tuangalie kama vijiji vina sifa ya kupelekewa umeme kwa mradi wa REA tutafanya hivyo, tutakaa naye pamoja ili ikibainika basi wapelekewe kwa utaratibu wa REA.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie pia Mheshimiwa Muganyizi Lwakatare kwamba vijiji vyote ambavyo amevitaja vikiwemo vya Kashai, Mafumbo Tweyambe, Turabirere, Kahororo pamoja na visiwa vyake vya Nyabisaka pamoja na Msira vitapata umeme kupitia Mradi wa REA. (Makofi)

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. WILFRED M. LWAKATARE aliuliza:- Mji wa Manispaa ya Bukoba una vijiji ambavyo havina umeme kabisa na havikuingizwa katika mpango wa REA wa kusambaza umeme. Je, Serikali ina mpango gani wa kuvipatia umeme vijiji vya kata za Nyanga, Ijuganyondo na Kahororo ambavyo mazingira na hali ya kiuchumi haitofautiani na vijiji vilivyosambaziwa umeme katika wilaya nyingine vijijini?

Supplementary Question 2

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Mwezi mmoja uliopita Wizara ilikuwa inazindua umeme wa REA Awamu ya Tatu katika maeneo mbalimbali lakini baadaye wamesimama. Ni lini wanafanya uzinduzi huo katika Mkoa wa Geita na hasa Jimbo la Geita Mjini?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa ni kweli tulianza kuzindua mikoa kumi kwa Tanzania Bara na tulibakiza mikoa takribani 15. Nimhakikishie Mheshimiwa Kanyasu kwamba tumemaliza taratibu zote za kuwapata wakandarasi. Nitumie nafasi hii kwa heshima ya Bunge lako Tukufu kuwaambia Waheshimiwa Wabunge wote na wananchi kwa ujumla, kesho tarehe 18 Mei, saa 08.00 mchana hapa Mjini Dodoma, kupitia Ukumbi wa Mikutano wa Hazina, wakandarasi wote katika mikoa ya nchi nzima watakabidhiwa katika mikoa yao. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii pia niwakaribishe Waheshimiwa Wabunge watakaokuwa na nafasi ya kuhudhuria katika ukabidhiwaji wa mikataba hiyo na majukumu yale ili muweze kushiriki.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hayo tutakwenda kuwatambulisha wakandarasi wote mkoa kwa mkoa ili Waheshimiwa Wabunge muweze kufuatilia uwajibikaji wao na orodha pia mtakabidhiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nichukue nafasi hii pia kuwataka wakandarasi wote watakaokabidhiwa mikataba yao kesho, waende katika maeneo yao ya kazi na waanze sasa kutekeleza mradi wa REA kwa nchi nzima, kijiji kwa kijiji, kitongoji kwa kitongoji na bila kuruka kijiji wala tarafa.
Nichukue nafasi hii kuwaeleza Waheshimiwa Wabunge kama ambavyo umeme haubagui itikadi, umeme pia wa REA hautabagua aina ya nyumba, iwe nyumba ya tembe au vinginevyo, kila aina ya nyumba watapatiwa umeme kupitia mradi huu. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. WILFRED M. LWAKATARE aliuliza:- Mji wa Manispaa ya Bukoba una vijiji ambavyo havina umeme kabisa na havikuingizwa katika mpango wa REA wa kusambaza umeme. Je, Serikali ina mpango gani wa kuvipatia umeme vijiji vya kata za Nyanga, Ijuganyondo na Kahororo ambavyo mazingira na hali ya kiuchumi haitofautiani na vijiji vilivyosambaziwa umeme katika wilaya nyingine vijijini?

Supplementary Question 3

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Naomba nimuulize swali dogo Mheshimiwa Naibu Waziri, kwanza nampongeza sana kwa kazi nzuri ambayo anafanya…
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Ukonga, Kata za Msongola, Buyuni, Zingiziwa, Majohe, Pugu, Pugu Station na Chanika hazina umeme na Mheshimiwa Naibu Waziri anafahamu. Kwa sababu kuna mkanganyiko kule Dar es Salaam kwamba ni mjini siyo vijijini, je, REA inaenda maeneo hayo au haiendi? Ahsante sana.(Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa, yako maeneo yako mjini, lakini kwa Mheshimiwa Mbunge wa Ukonga tumeshakaa naye. Maeneo anayoyataja ya Majohe, Chanika, Zingiziwa mpaka kwenye gereza lako kijijini kule, yale ni maeneo ya vijijini yatapatiwa umeme kupitia Mradi wa REA na tumeshaanza. Hata hivyo shule yake aliyosema Mheshimiwa ya Bombambili tumeshaifanyia kazi na yeye ni shahidi. Kwa hiyo, maeneo hayo yatapelekewa umeme kwa kupitia mradi wa REA.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. WILFRED M. LWAKATARE aliuliza:- Mji wa Manispaa ya Bukoba una vijiji ambavyo havina umeme kabisa na havikuingizwa katika mpango wa REA wa kusambaza umeme. Je, Serikali ina mpango gani wa kuvipatia umeme vijiji vya kata za Nyanga, Ijuganyondo na Kahororo ambavyo mazingira na hali ya kiuchumi haitofautiani na vijiji vilivyosambaziwa umeme katika wilaya nyingine vijijini?

Supplementary Question 4

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, natambua kwamba umeme wa REA ni wa vijijini, lakini yako maeneo ya mjini ambayo yana maeneo mengi na makubwa ya vijijini. Nashukuru kwamba REA wameweza kutupatia umeme katika mitaa michache kama ya Nyabisare pamoja na kule Bukanga.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu, kwa kuwa, maeneo mengi ya taasisi yako kwenye hizo kata za pembezoni, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba REA wanaweza kutupatia umeme katika maeneo yote hayo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa yako maeneo, najua Tarime mko wawili na kuna Musoma na Tarime lakini ki-TANESCO ni Tarime, hakuna shida Mheshimiwa, nimeshakuona Mheshimiwa Esther Matiko.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda tu kusema kwamba, ukweli yako maeneo ambayo yako pembezoni ingawaje yanasemeka yako mjini. Tumeshakaa na Mheshimiwa Manyinyi, yako maeneo na hasa kwa taasisi za umma, taasisi zote za umma zitapelekewa umeme kupitia mradi wa REA.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini viko vijiji ambavyo itabidi tuviangalie, vile vijiji ambavyo vinaonekana viko mjini vitapelekewa umeme kupitia miradi ya TANESCO lakini vile vya vijijini kama ambavyo amesema Nyabisare na vingine, tutachambua ili kuona ni vijiji gani vipelekewe kwa Mradi wa REA. Vijiji vyote vya Miradi ya REA tumeshakabidhiwa, kwa hiyo, kwa Mheshimiwa Mbunge ambaye anaona kuna sehemu kuna utata ni vema tukae ili isionekane kijiji fulani kinarukwa.