Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 27 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 225 2017-05-17

Name

Wilfred Muganyizi Lwakatare

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Bukoba Mjini

Primary Question

MHE. WILFRED M. LWAKATARE aliuliza:-
Mji wa Manispaa ya Bukoba una vijiji ambavyo havina umeme kabisa na havikuingizwa katika mpango wa REA wa kusambaza umeme.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuvipatia umeme vijiji vya kata za Nyanga, Ijuganyondo na Kahororo ambavyo mazingira na hali ya kiuchumi haitofautiani na vijiji vilivyosambaziwa umeme katika wilaya nyingine vijijini?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Wilfred Muganyizi Lwakatare, Mbunge wa Bukoba Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Usambazaji Umeme Vijijini Awamu ya Tatu umeanza rasmi nchi nzima mwezi Machi, 2017. Mradi huu utajumuisha vipengele vya mradi vitatu vya Densification, Grid Extension na Off-Grid Renewable. Mradi huu unalenga kusambaza umeme katika vijiji vyote nchi nzima, vitongoji vyote, taasisi zote za umma na maeneo yote ya pembezoni, ikiwa ni pamoja na visiwa. Mradi wa REA Awamu ya Tatu utakamilika mwaka 2020/2021.
Mheshimiwa Naibu Spika, TANESCO inaendelea na usambazaji wa umeme katika maeneo ya mijini ambayo hayajapata umeme, vikiwemo vijiji vya Kata za Ijuganyundo, Kahororo, Nyanga pamoja na Jimbo zima la Bukoba Mjini. Kazi hii inafanyika mwaka huu wa fedha 2016/2017 kwa gharama ya shilingi bilioni 22.96.
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo mengine ikiwemo kata ya Nyanga na vijiji vya Hyolo, Kyakailabwa pamoja na Vijiji vingine vya Rubumba, vitapatiwa umeme kupitia umeme wa Urban Electrification Program chini ya TANESCO. Mradi huu unatarajiwa pia kuanza mwaka 2018. Upembuzi yakinifu wa mradi huo umeshakamilika. Mradi utafikisha umeme kwa wateja wote wa awali 469 na utagharimu shilingi bilioni 782.6.