Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA (K.n.y. MHE. ZUBEDA H. SAKURU) aliuliza:- Magereza mengi nchini hayapo katika viwango na ubora unaotakiwa na hivyo kuvunja haki za wafungwa. Je, Serikali ina mkakati gani katika kufanya matengenezo na kulinda haki za wafungwa?

Supplementary Question 1

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Magereza mengi nchini yanaendeshwa kinyume kabisa na Kanuni Namba 10 ya Umoja wa Mataifa ambayo inazungumzia namna ya kuwahifadhi wafungwa kwamba ni lazima wakidhi vigezo ikiwemo afya, hali ya hewa, joto na nafasi ya kutosha. Magereza mengi nchini likiwemo Gereza la Songea ni mojawapo ya magereza kongwe nchini ambalo lilijengwa tangu mwaka 1948. Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba gereza hili nalo linakidhi vigezo?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tangu Rais aseme maneno ka-ta yameleta athari kwa magereza mengi nchini ikiwemo magereza 14 ya Mkoa wa Morogoro ambayo hivi sasa yako kwenye giza tororo. Serikali haioni kama magereza haya kuendelea kuwa na giza ni kinyume kabisa na haki za Umoja wa Kimataifa na pia inasababisha Askari Magereza kushindwa kufanya kazi zao vizuri? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, moja, nimpongeze kwa kuonyesha concern ya msongamano wa wafungwa kwenye magereza na ameuliza Serikali tuna mkakati gani. Moja ya mkakati wa muda mrefu tunaofanya ni wa kuhahakisha kwamba tunajenga magereza hasa kwenye maeneo ambayo ni ya kilimo yawe na ukubwa wa kutosha na magereza ya mijini yawe kwa ajili ya mahabusu ambao wanahitajika kuwa karibu na mahakama kwa ajili ya usikilizaji wa kesi zao. Kwa hawa ambao walishahukumiwa wawe katika magereza ambako kazi ya kuwarekebisha inaweza ikafanyika huku kukiwa na kazi ya uzalishaji inayoendelea katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la umeme kukatwa, jambo hilo lilishashughulikiwa kwa sababu tayari Hazina ilishatoa fedha kwa ajili ya mafungu yetu ya Polisi, Magereza pamoja na maeneo mengine. Mimi niwasisitizie Waheshimiwa Wabunge, nia na maelekezo aliyoyatoa Mheshimiwa Rais yanarekebisha kwa kiwango kikubwa Maafisa Masuuli wanapopewa fedha zilizokuwa zimeelekezwa kwa ajili ya utilities waweze kutumia katika maeneo yale ambayo yalikusudiwa fedha hizo ziweze kutumika. Kwa maana hiyo, badiliko hili linaweza likaathiri katika kipindi ambacho tu madeni yalikuwa yamelimbikizwa lakini itajenga nidhamu ya kudumu ya Maafisa Masuuli kuweza kuelekeza fedha zilipokuwa zimeelekezwa ili kupata jawabu la kudumu la matumizi bora ya fedha zinazotolewa na Serikali. (Makofi)

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA (K.n.y. MHE. ZUBEDA H. SAKURU) aliuliza:- Magereza mengi nchini hayapo katika viwango na ubora unaotakiwa na hivyo kuvunja haki za wafungwa. Je, Serikali ina mkakati gani katika kufanya matengenezo na kulinda haki za wafungwa?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kunipa nafasi ya kuuliza swali fupi la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa magereza mengi nchini yamekuwa chakavu likiwemo Gereza la Kalilamkurukuru lililopo Wilaya ya Tanganyika. Nini mkakati wa Serikali kuimarisha magereza haya kwa kuyafanyia ukarabati sambasamba na nyumba za askari?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Kakoso kwa swali lake zuri la nyongeza. Niseme tu kwamba tuna mikakati ya aina mbili, kwa upande wa nyumba za askari kama nilivyoelezea wakati wa bajeti tunaenda hatua kwa hatua, tuna miradi midogo na mikubwa ambayo tunaitekeleza. Kwenye ukarabati sambasamba na upande wa ujenzi wa nyumba tumekubaliana kutumia bajeti inayotengwa lakini pamoja na nguvukazi tunayoipata kutokana na wajuzi tulionao kwa upande wa askari, lakini wajuzi tulionao kwa wale walioko magerezani ili tuunganishe nguvu zote hizo na bajeti inayopatikana tuweze kufanya marekebisho pamoja na ujenzi wa makazi mapya pamoja na mabweni kwa ajili ya wafungwa.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA (K.n.y. MHE. ZUBEDA H. SAKURU) aliuliza:- Magereza mengi nchini hayapo katika viwango na ubora unaotakiwa na hivyo kuvunja haki za wafungwa. Je, Serikali ina mkakati gani katika kufanya matengenezo na kulinda haki za wafungwa?

Supplementary Question 3

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa kumekuwa na tabia mbaya kwa baadhi ya askari kudhalilisha raia na hata kuwatolea kauli mbaya ikiwemo hata sisi Wabunge tumekuwa tukikutana na kauli mbaya kutoka kwa baadhi ya askari lakini inapokuja kwenye kutetea maslahi yao sisi ndiyo tumekuwa wa kwanza kuwatetea. Je, Serikali inatoa kauli gani? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, moja, askari wetu wa Jeshi la Polisi pamoja na askari wengine ni Watanzania na wanafanya kazi kwa gharama za maisha yao. Kwa hiyo, tuna wajibu wa kutimiza kama Taifa kwa kutambua kwamba askari wanafanya kazi kwa mujibu wa sheria na hakuna haki isiyo na wajibu. Sisi kama Wizara ya Mambo ya Ndani pamoja na taasisi zingine tuna utaratibu wa kuchukua hatua punde inapotokea askari amefanya kazi kinyume na taratibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuna wajibu ambao Watanzania, wananchi kwa ujumla wanatakiwa watimize wanapokuwa wamekutana na askari wetu. Kwa mfano, afadhali sisi ni viongozi, wengi wetu tunatoa uongozi tunapokutana na askari lakini kuna watu wengine ambao hawatoi heshima inayostahili kwa vyombo vyetu vya dola. Sasa vyombo vyetu vya dola vimepitia mafunzo na mimi kama kiongozi wao nisingependa kuona Jeshi la Polisi linafanana na green guard, blue guard au red brigade.(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lazima Watanzania watambue kwamba vyombo vyetu vya dola vina heshima, vinafanya kazi kubwa na vinastahili kupewa heshima kama vyombo vya dola. Ukitaka kupambana na vyombo vya dola wana sehemu ambayo wanaruhusiwa kutumia nguvu wanapoona kile kinachofanywa na raia kinaweza kikahatarisha ama kikaleta athari iliyo kubwa zaidi. Kwa kuwa Waheshimiwa Wabunge tunakutana na watu wetu, tuendelee kuitoa elimu hiyo ili vyombo vya dola katika nchi yetu kama ilivyo katika nchi zingine viweze kupewa heshima vinavyostahili.

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA (K.n.y. MHE. ZUBEDA H. SAKURU) aliuliza:- Magereza mengi nchini hayapo katika viwango na ubora unaotakiwa na hivyo kuvunja haki za wafungwa. Je, Serikali ina mkakati gani katika kufanya matengenezo na kulinda haki za wafungwa?

Supplementary Question 4

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, moja ya haki za wafungwa zinazovunjwa ni pamoja na makazi duni sambamba na kukosekana kabisa kwa rufaa za hukumu jambo ambalo linafanywa kwa makusudi na baadhi ya maafisa husika na Case Flow Management Committees haziendi kwa wakati. Swali, Serikali ina mkakati gani wa ziada kukamilisha taratibu hizi ili wafungwa wapate haki zao inavyostahili? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Masoud kwa swali hilo. Niseme tu kama nilivyotaja baadhi ya haki, zile nilizotaja ni baadhi tu, lakini kwa upana wake kuna vitu vingine vingi zaidi na kama Serikali tumejipanga na hivi vinahusisha zaidi ya Wizara moja. Utaona Mheshimiwa Rais anapoweka nguvu upande wa mahakama anamaanisha kesi zisikae sana kwa sababu haki ikicheleweshwa inakuwa haki iliyokataliwa, unaona jambo hilo linavyofanyika. Anavyoiwezesha magereza kupata magari ya kubebea mahabusu waweze kupelekwa kusikilizwa kesi zao anawezesha connection kati ya mahakama, magereza pamoja na polisi waweze kufanya kazi hizo ambazo zote hizo zikipunguza mahabusu waliokuwa magerezani automatically inakuwa zimepunguza msongamano kwenye magereza hayo na kuwafanya wapate haki hiyo mojawapo aliyoitaja.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini niseme tu maswali yenu yote mliyouliza yale ambayo yana mlengo wa kiushauri kama Serikali tumepokea na tutaenda kuyafanyia kazi ili kuweza kuleta ustawi katika maeneo haya mliyoyataja.