Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. RICHARD P. MBOGO aliuliza:- Vifo vya mama na mtoto vinachangiwa na huduma hafifu ikiwemo ukosefu wa usafiri hasa gari la kubebea wagonjwa (ambulance). Je, ni lini Serikali itatoa gari la wagonjwa kwa Jimbo la Nsimbo?

Supplementary Question 1

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Serikali, naomba tu niipe taarifa Serikali kwamba hiyo fedha imetengwa sh.milioni 220 siyo sahihi ni fedha ambayo ipo kwenye maombi maalum, kwa sababu binafsi nilipitia bajeti ya Halmashauri yote, CDG tulipewa shilingi bilioni 1.24; allocation ya gari la wagonjwa haikuwepo kutokana na fedha kuwa ndogo na mahitaji ya Jimbo la Nsimbo kwa upande wa elimu, afya, na maeneo mengine kuwa na uhitaji zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hilo gari moja lililopo ni msaada ambao Jimbo la Nsimbo lilipata kutoka Shirika la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), tunashukuru kwa mgao huo, kutokana na Jimbo kuwa na makazi ya wakimbizi kwenye Kata ya Katumba.
Je, Serikali haioni ule mpango tuliouleta wa maombi maalum wakachukua kile kipengele tu cha gari la wagonjwa, watuidhinishie ile Halmashauri yetu tuweze kupata gari hilo au laa, hatuna wasiwasi na utekelezaji wa ahadi mbalimbali za Serikali kuhusiana na kujali afya za wananchi wake kwa kutoa magari ya wagonjwa, kama hivi juzi Mheshimiwa Rais ametoa mgari matatu je, Serikali haioni tena kuna umuhimu wa Jimbo la Nsimbo na lenyewe likaangaliwa kupata gari la wagonjwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana nimesema kwamba kwanza tumewashukuru wenzetu wa Nsimbo na Mheshimiwa Mbunge naomba nikushukuru sana kwa kuonesha commitment yenu kwamba kulikuwa na hili hitaji ya gari. Ndiyo maana naomba niseme kwamba, kwa kipindi hiki cha Serikali ya Awamu ya Tano, niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba, Mheshimiwa Rais na Serikali yake amejipanga sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri umesuhudia hapa kwamba, juzi Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Ally Kessy Mohamed na wenzie Mheshimiwa Rais alitoa magari matatu personally pale, lakini kuna magari mengine 50 yaliweza kupelekwa katika maeneo mbalimbali. Hii yote ni jukumu la Serikali kuwahudumia wananchi. Hivyo, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Richard Mbogo kwamba tutaangalia kile kinachowezekana ili kulisaidia Jimbo lako ambalo liko mpakani kabisa ili suala hili la gari la wagonjwa na yale mambo mengine ya msingi likiwemo suala zima la ujenzi wa kituo cha afya, kufanya ukarabati katika eneo lako tutalifanya. Serikali ya Awamu ya Tano lengo kubwa ni kuwapunguzia adha akina mama na watoto.

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. RICHARD P. MBOGO aliuliza:- Vifo vya mama na mtoto vinachangiwa na huduma hafifu ikiwemo ukosefu wa usafiri hasa gari la kubebea wagonjwa (ambulance). Je, ni lini Serikali itatoa gari la wagonjwa kwa Jimbo la Nsimbo?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mazingira yaliyopo Nsimbo yanafanana kabisa na mazingira yaliyopo katika katika Jimbo la Kavuu na kupitia initiative ya Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokuja kwenye ziara katika Jimbo la Kavuu alituomba tuanzishe Hospitali ya Halmashauri ya Mpimbwe kufuatia kuwepo na kadi za CHF kwa sababu za NHIF hazitumiki kule.
Je, Serikali sasa haioni kuna umuhimu, kutokana na juhudi za wananchi wa Jimbo la Kavuu kuwapatia gari la wagonjwa ambao wamekuwa wakitumia umbali mrefu kutoka Mpimbwe kwenda Mpanda na sasa tutumie katika Jimbo la Kavuu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, mara nyingi sana huwa nazungumza hapa Bungeni kwamba, issue ya gari la wagonjwa ni vema kwanza tukai-allocate katika bajeti zetu za kila mwaka, hilo ni jambo la msingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu sana Mheshimiwa Dkt. Kikwembe anavyohangaika kwa Jimbo lake, ndiyo maana hapa juzi alikuwa anahangaika tupeleke huduma za afya pale na ndiyo maana tulimhakikishia pamoja na Waziri wa Afya, na Mheshimiwa Waziri Mkuu alienda pale na akatoa ahadi, tutaenda kufanya ukarabati mkubwa wa kituo chake cha afya kwa kuingiza fedha nyingi ili akina mama na watoto sasa waweze kupata huduma nzuri, hasa huduma ya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Dkt. Kikwembe mahitaji yako ambayo umeongea mbele ya Waziri Mkuu, Serikali imeyachukua kwa ujumla wake, hata hivyo, naomba nipendekeze, kwa Wabunge mbalimbali katika suala la ambulance lazima tuliainishe katika bajeti zetu, likishakuwepo katika bajeti tunapata msingi mzuri wa kulifanya jambo hilo katika utekelezaji wake.

Name

Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. RICHARD P. MBOGO aliuliza:- Vifo vya mama na mtoto vinachangiwa na huduma hafifu ikiwemo ukosefu wa usafiri hasa gari la kubebea wagonjwa (ambulance). Je, ni lini Serikali itatoa gari la wagonjwa kwa Jimbo la Nsimbo?

Supplementary Question 3

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la gari la wagonjwa Jimbo la Nsimbo ni sawasawa kabisa na tatizo hili linalotukabili Wilaya ya Manyoni. Tunayo Hospitali kubwa ya Wilaya pamoja na vituo viwili vya afya vya Nkonko pamoja na Kintinku. Magari tuliyonayo ni chakavu sana na kumekuwa na matukio mengi ya kubeba wagonjwa na magari yanaharibika njiani mpaka kulala njiani, inabidi utoe gari sasa kutoka Manyoni Mjini kwenda kufaulisha wale wagonjwa.
Je, ni lini Serikali sasa itatupatia nasi angalau gari la wagonjwa kwa Wilaya ya Manyoni ukizingatia hali halisi ya Manyoni pale, kuna ajali nyingi zinatokea kwenye ule mlima wa Saranda Sukamahela?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa lugha ya kwetu sisi, ndiyo maana mwanzo nilianza na kile kitu kinaitwa kingilambago. Nilieleza pale awali kwamba, lazima hili jambo tuliainishe katika suala zima la mpango wetu wa bajeti. Mheshimiwa Mtuka naomba nikuhakikishie kwa sababu nami nilifika pale Manyoni, kwanza nilitoa maelekezo katika hospitali yako kwa sababu, hata hili suala la referral ni lazima maeneo yetu watu wafanye kazi vizuri, niligundua baadhi ya uzembe pale katika watalaamu wetu, nikatoa maelekezo. Jambo hili naomba nikuhakikishie katika mpango wako wa bajeti 2018/2019 naomba liainishwe wazi na likifika kwetu katika Ofisi ya TAMISEMI tutalipa nguvu ili kwamba eneo la Manyoni pale tupate gari la wagonjwa.

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. RICHARD P. MBOGO aliuliza:- Vifo vya mama na mtoto vinachangiwa na huduma hafifu ikiwemo ukosefu wa usafiri hasa gari la kubebea wagonjwa (ambulance). Je, ni lini Serikali itatoa gari la wagonjwa kwa Jimbo la Nsimbo?

Supplementary Question 4

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Mimi swali langu dogo tu, nilikuwa naomba, maana uzoefu inaonekana kama Waziri Mkuu ama Waziri wa TAMISEMI anafika katika eneo kuangalia hali halisi ya matatizo ndiyo pale inapomuuma katika moyo na kutoa kipaumbele katika haya maeneo.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu ni kwamba ni lini sasa Waziri wa TAMISEMI ama Waziri Mkuu atafika kwenye Jimbo la Mlimba ili aangalie matatizo alie na machozi halafu aone sympathy ya kuwasaidia wananchi wa Mlimba katika masuala ya magari, afya na mambo mengine? Ni hapa tu.(Makofi/Kicheko)

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Kiwanga kwamba tulifanya ziara ofisi yetu, tumetembelea Halmashauri zote kati ya Halmashauri 185 tumebakisha chini ya Halmashauri kumi hivi sasa na moja ikiwa yako ya Mlimba. Ndiyo maana tumekubaliana hapa na nimezungumza katika kipindi mbalimbali kwamba baada ya Bunge nitakuwa na session maalum katika Mkoa wa Morogoro kumalizia Halmashauri zilizobaki na Mkoa wa Songwe, vilevile nitaenda kule Ukerewe pamoja na Mara ambako kuna Rorya, Tarime na Serengeti.
Mheshimiwa Naibu Spika, hayo tunaenda kuyafanya lengo kubwa ni kufikia maeneo mbalimbali tubadilishane mawazo tikiwa site kule tukubaliane, tubaini changamoto halafu tujadiliane, nini tutafanya ili kuwahudumia wananchi. Kwa hiyo, naomba nikutoe hofu katika hilo tutaenda kulifanya katika kipindi cha sasa.