Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 22 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 187 2017-05-11

Name

Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. RICHARD P. MBOGO aliuliza:-
Vifo vya mama na mtoto vinachangiwa na huduma hafifu ikiwemo ukosefu wa usafiri hasa gari la kubebea wagonjwa (ambulance).
Je, ni lini Serikali itatoa gari la wagonjwa kwa Jimbo la Nsimbo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Richard Philip Mbogo, Mbunge wa Nsimbo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo ina jumla ya vituo vya afya vitatu. Kituo cha Afya cha Katumba, Kituo cha Afya cha Kanoge na Kituo cha Afya cha Mtisi vinavyohudumiwa na gari moja la wagonjwa. Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo ina upungufu wa magari mawili. Kwa kuzingatia changamoto hiyo, Halmashauri imetenga jumla ya shilingi milioni 220 katika mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya ununuzi wa gari la wagonjwa ili kuharakisha huduma za rufaa na kupunguza vifo vya akina mama na watoto.