Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALOME W. MAKAMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Rais aliyoitoa wakati wa kampeni kwa wananchi wa Jimbo la Kahama Mjini ya kujenga kwa kiwango cha lami kilometa 10 za barabara za mitaa ya Mji wa Kahama?

Supplementary Question 1

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Ningependa kuuliza maswali mawili ya nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI.
Mheshimiwa Waziri umetuaminisha kwamba mmetupatia shilingi milioni 600 kwa ajili ya kujenga barabara na pia mmetupa shilingi milioni 320 kwa ajili ya kukarabati barabara hizi. Mheshimiwa Waziri barabara ya Phantom-Majengo, ni barabara ya muhimu kweli na barabara hii inachangia pato la Halmashauri kwa asilimia 25. Barabara hii ina urefu wa mita tano na tunasema tunataka tufanye Serikali ya viwanda, kule kuna viwanda vidogo vidogo vya mazao ya mpunga na mahindi.
Mheshimiwa Waziri, hauoni kama kuna umuhimu wa kuingiza barabara hii katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha ili tuweze kutekeleza mpango huu wa Tanzania ya viwanda kwa kuendelea kuzalisha na magari yaweze kupita? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Ushetu, Mheshimiwa Waziri mmetenga shilingi milioni 181 tu kwa ajili ya barabara na tena ni kwa ajili ya ukarabati tu wa barabara, lakini nikufahamishe kwamba kule hakuna barabara hata moja ya lami, barabara zote ni za vumbi na fedha mliyotenga ni kidogo na ile ni Halmashauri mpya. Unawaambia nini Watanzania wa Ushetu, watawezaje kupata barabara nzuri za lami ilihali mmewatengea fedha kidogo namna hii, nini mpango wa Serikali kwa Halmashauri hii mpya?
Mheshimiwa Naibu Spika, nilimaanisha kilometa tano.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, Mji wa Kahama kimkakati tunafahamu na ndio maana hata ninyi katika Mji wa Kahama mlikuwa mnapeleka maombi kwa Mheshimiwa Waziri wa Nchi kwamba Mji ule sasa uwe Manispaa kwa kadri unavyokua. Ukiangalia barabara ya Phantom - Majengo ina kilometa 5.2 ni barabara ya kimkakati ina jukumu kubwa sana, ndiyo maana tumesema mwaka huu tumeanza kutenga fedha hizo. Hata hivyo, unafahamu Mji wa Kahama siyo barabara hii tu ndiyo tunaanza kujenga, kuna miundombinu ya barabara za lami pale zilikuwa zinaendelea na mimi nilifika pale miezi michache iliyopita kuja kukagua.
Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu letu kubwa tunajua kwamba eneo hili ni eneo la mkakati, kama Serikali tutafanya kila liwezekanalo, lakini siyo Mji huu peke yake. Serikali tumejipanga kuna ahadi za Mheshimiwa Rais katika maeneo mbalimbali, hivi sasa ukiangalia katika Halmashauri mbalimbali, juzi Mheshimiwa Rais alikuwa kwa ndugu yangu pale Mheshimiwa Mbowe, alikuwa akiangalia miundombinu ya barabara. Pia nchi nzima hata kwa Mzee Lubeleje kule Mpwapwa kuna ahadi ya Mheshimiwa Rais.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tunachotaka kufanya ni kwamba ndani ya miaka mitano tufanye mabadiliko makubwa sana katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hasa katika ujenzi wa barabara za lami.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwaondoe hofu Waheshimiwa Wabunge, siyo kwa Mji wa Kahama peke yake isipokuwa katika miji mbalimbali katika Halmashauri zetu hizi tutahakikisha ujenzi wa barabara za lami hasa kutumia fedha za World Bank ambayo Serikali imechukua commitment ya kutosha kubadilisha miji yake yote iweze kubadilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninyi ni mashahidi mnafahamu sasa hivi, Halmashauri za Miji nyingi sasa hivi na Manispaa zimebadilika katika suala la ujenzi wa barabara za lami TAMISEMI imeamua kufanya hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu eneo la Ushetu kama ulivyosema ni kwamba tunafahamu Ushetu ni Halmashauri mpya na ndiyo maana, ndugu yangu hapa Mheshimiwa Elias Kwandikwa kila siku anapambana na Jimbo lake la Ushetu, kama unavyopambana Mheshimiwa Mbunge hapa. Naomba kuahidi kwamba kwa kutumia Mfuko wa Barabara, nikuahidi tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo tutahakikisha maeneo ya Ushetu na maeneo mengine tutaweka nguvu za kutosha na hasa hizi Halmashauri mpya tutaweza kuzifungua ili wananchi kule waweze kupata huduma wajisikie huru kama wananchi wenzao wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Name

Peter Ambrose Lijualikali

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. SALOME W. MAKAMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Rais aliyoitoa wakati wa kampeni kwa wananchi wa Jimbo la Kahama Mjini ya kujenga kwa kiwango cha lami kilometa 10 za barabara za mitaa ya Mji wa Kahama?

Supplementary Question 2

MHE. PETER A. P. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Mheshimiwa Waziri Mji wa Ifakara ni Halmashauri mpya, kutokana na upya wake bado ni changa. Barabara zetu bado ziko katika level ya tope, kutokana na mvua hizi ambazo kule zinanyesha barabara zinaharibika sana. Sisi kama Halmashauri tunajaribu kuziwekea vifusi lakini kwa sababu ni Halmashauri mpya, hatuna fedha za kutosha kuweza kujenga lami.
Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia Halmashauri ya Mji wa Ifakara, Halmashauri ambayo ni mpya ili iweze kuboresha barabara zake, ziweze kuwa katika kiwango cha lami?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nafahamu Kilombero na maeneo mengine, naomba niwape pole Wabunge wote kwa sababu nikijua wazi kwamba kipindi hiki mvua zinanyesha, barabara nyingi sana katika maeneo yetu zimeharibika vya kutosha. Ndiyo maana katika bajeti yetu ya mwaka huu, tuliyoipitisha tumetenga karibuni shilingi milioni 247 mwaka huu wa fedha 2017/2018 ili kuhakikisha tunafikia maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, hapa sitaki kutoa commitment ya uwongo kusema kesho Kilombero pale Ifakara tutakuja kujenga barabara za lami, itakuwa ni uwongo. Kikubwa zaidi tutaangalia jinsi gani tutafanya kwa bajeti iliyopo sasa, kwa sababu tunakwenda awamu kwa awamu. Tulikuwa na miji mikuu, tumeenda na manispaa, tunaenda katika halmashauri za miji, tunaangalia jinsi gani tutafanya kwa sababu kila barabara zingine zinawekewa kifusi ili barabara iweze kupitika.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba commitment ya Serikali ni kuhakikisha wananchi wake wanaweza kufikiwa, wanaweza kusafirisha mazao yao na hata kusafiri sehemu zingine, hii ni commitment ya Serikali. Hivyo, tutajitahidi kufanya kila liwezekanalo bajeti iliyotengwa katika eneo hilo tutaisimamia vizuri, kwa sababu changamoto kubwa ni usimamizi wa bajeti katika maeneo yetu wakati mwingine.

Name

Freeman Aikaeli Mbowe

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SALOME W. MAKAMBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Rais aliyoitoa wakati wa kampeni kwa wananchi wa Jimbo la Kahama Mjini ya kujenga kwa kiwango cha lami kilometa 10 za barabara za mitaa ya Mji wa Kahama?

Supplementary Question 3

MHE. FREEMAN A. MBOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu tatizo la Mji wa Kahama kama sahihi kabisa alivyozungumza Mheshimiwa Naibu Waziri linafanana kwa njia moja au nyingine na ahadi za Rais alizotoa wakati wa kampeni, ni kweli Rais wakati wa kampeni alitoa ahadi ya kujengea Halmashauri ya Wilaya ya Hai kilometa tano za lami katika Mji wa Hai katika kipindi chake cha uongozi. Na ni kweli kwamba hivi majuzi Rais alivyokuwa katika ziara kwenye Mkoa wetu wa Kilimanjaro aliulizwa kuhusu ahadi yake na Rais akauliza vilevile Halmashauri imegawiwa fedha kiasi gani katika mwaka huu wa fedha kwa ajili ya Mfuko wa Barabara. Taarifa ambazo Rais alipewa ni fedha ambayo ilikuwa imepangwa kwenye bajeti ambayo ni shilingi bilioni 1.3 lakini hiyo fedha haijapokelewa kwa sababu haijatolewa na Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, natambua kwamba Rais aliagiza kwamba TAMISEMI wakafanye uchunguzi, nakaribisha sana TAMISEMI mkafanye uchunguzi, lakini ukweli ni kwamba fedha pekee ambayo ilishapokelewa ni kama shilingi bilioni 300 ambayo ni lazima mtambue kwamba Wilaya ya Hai ina zaidi ya kilometa 200 za barabara zinazoteleza za milimani ambazo ni lazima zifanyiwe routine maintanace.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sasa Mheshimiwa Naibu Waziri ni wewe kutoa commitment ya kwenda kufuatilizia alichokizungumza Rais, lakini vilevile kukumbushia ahadi ya Rais ya kilometa tano za Halmashauri ya Wilaya ya Hai katika Mji wa Hai, bado ni muhimu sana kwa sababu Mji unakuwa kwa kasi na una zaidi ya wakazi 50,000 ambao kwa kweli hawana hata robo kilometa ya lami katika Mji wa Hai ukiacha barabara ya kwenda Arusha. Mheshimiwa Waziri naomba commitment yako.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA
NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni na hata baada ya kampeni amekuwa akiahidi kufanya mambo mbalimbali hasa anapoona maeneo fulani yana matatizo. Katika eneo la barabara ametoa ahadi maeneo mbalimbali ikiwemo Kasulu kilometa sita na hapa Mheshimiwa Mbowe anasema kilometa tano na hasa barabara za milimani, lakini ameahidi maeneo mengi, Waheshimiwa Wabunge wana ahadi na wana kumbukumbu hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge, kwamba ahadi za Mheshimiwa Rais zitatekelezwa na kwa sababu bado tunao muda na tutaangalia kama utaratibu mzuri ni wa kuzingatia wakati wa bajeti zetu lakini nafahamu mnafahamu kwamba bajeti zetu huwa zina ukomo, kwa hiyo tutajaribu kuangalia namna ya modality nzuri ya kuweza kutekekeleza hili tukimshirikisha aliyeahidi.
Pia nitoe rai tu kwa wenzangu kwamba wakati tunaposimamia ahadi za Mheshimiwa Rais pia tuwe tunakumbuka kuishi naye vizuri na kumheshimu. Ahsante sana.(Makofi)