Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 22 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 186 2017-05-11

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALOME W. MAKAMBA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Rais aliyoitoa wakati wa kampeni kwa wananchi wa Jimbo la Kahama Mjini ya kujenga kwa kiwango cha lami kilometa 10 za barabara za mitaa ya Mji wa Kahama?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Salome Wcyliffe Makamba, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua ya kwanza ya utekelezaji wa ahadi ya Mheshimiwa Rais ilikuwa ni kuzitambua barabara zitakazojengwa kwa kiwango cha lami katika Halmashauri ya Mji wa Kahama ambayo imekamilika. Ujenzi huo utahusisha barabara ya Mama Farida yenye urefu wa kilometa 1.305; barabara ya Phantom -Majengo yenye urefu wa kilometa 5.214; barabara ya Malunga Mashineni - Mwamvua yenye urefu wa kilometa 1.852, barabara ya Nyihogo - Namanga yenye urefu wa kilometa 0.6, barabara ya Florida - Stendi ndogo yenye urefu wa kilometa 0.829 na barabara ya Royal ya Zamani - Stendi Ndogo yenye urefu wa kilometa 0.2.
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa barabara hizo utafanyika kwa awamu ambapo katika mwaka wa fedha 2017/2018, zimetengwa shilingi 603,604,733 kwa ajili ya kujenga barabara yenye urefu wa kilometa moja kwa kiwango cha lami. Vilevile, kupitia fedha za Mfuko wa Barabara, zimetengwa shilingi 320,000,000 kwa ajili ya ukarabati wa barabara za lami zenye urefu wa mita 800 katika Mji wa Kahama.