Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. JOHN J. MNYIKA (k.n.y MHE. SAED A. KUBENEA) aliuliza:- Serikali iliahidi kuhamisha Kituo cha Mabasi cha Ubungo na kukipeleka eneo la Mbezi katika Jimbo la Kibamba lakini mpaka sasa jambo hilo halijatelekezwa. (a) Je, Serikali imefikia hatua gani ktaika kutekeleza ahadi hiyo? (b) Je, mradi wa kuhamisha Kituo cha Mabasi unatarajiwa kutumia kiasi gani cha fedha?

Supplementary Question 1

MHE. JOHN J. MNYIKA. Mheshimiwa Spika, nashukuru. Inasikitisha majibu yanatoka ya namna hii, hili suala ni la tangu mwaka 2012 kilipovunjwa kituo cha mabasi cha Ubungo; na mwezi Oktoba, mwaka 2014 aliyekuwa Rais, Mheshimiwa Jakaya Kikwete alitamka kwamba kituo kitaanza kujengwa na akatoa mpaka muda mfupi wa kukamilika kwa kituo, lakini majibu mpaka sasa mwaka 2017 yanakuja namna hii.
Sasa swali, ni lini hasa hiki kituo kitakamilika ili kuondoa msongamano ulioko Kituo cha Ubungo ambacho kimeshavunjwa na kiko kwenye hali mbaya?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kituo hiki kinajengwa pembeni ya barabara ya Morogoro, na siku chache zilizopita TANROADS wametoa notice kwa wananchi wote wanaoishi pembezoni ya barabara ya Morogoro mita 121 kutoka katikati ya barabara kila upande. Kuweza ndani ya siku 28 kubomoa majengo yao. Ndani ya siku 28 mita 121 pande zote mbili za barabara kutoka katikati ya barabara. Sasa kwa kuangalia umbali ambao TANROADS umeutaja ni wazi ubomoaji huu utahusu kituo cha sasa cha mabasi ya kawaida ya Mbezi kilichopo. Vilevile kama umbali ni huu wa mita 121 kutoka katikati ya barabara hata hiki kituo kipya kitaguswa.
Mheshimiwa Spika, swali langu kwa Serikali ama Waziri mwenyewe ama Wizara hii ya TAMISEMI ama Wizara ya Ujenzi ijibu; kwa sababu huu umbali utaingilia hiki kituo ni kwa nini Serikali isitengue hili Tangazo lilitolewa na TANROADS la siku 28 ili majadiliano kwanza yafanyike kuhusu huu upana wa barabara sababu ni upana mkubwa sana ambao hauko kwenye barabara yoyote Tanzania? Mita 121 pande zote mbili za barabara kutoka katikati, naomba majibu ya Serikali.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: MheshimiwaMwenyekiti, Mheshimiwa Mnyika kwanza umesema kwamba muda umepita sana, ni kweli. Tuelewe kwamba hata suala zima la kituo hiki ni kituo mkakati sana nadhani na wewe liko katika jimbo lako pale. Ni kituo mkakati ambacho ukiangalia sasa hivi hata hizi barabara za kwenda kasi zinaishia pale Mbezi Mwisho. Nashukuru sana tumepata ushauri wa kamati ya TAMISEMI, walipofika kukagua kile kituo wametoa mapendekezo mengi sana.
Mheshimiwa Spika, hata suala hili la la reserve ya barabara waliliona na wakasema ikiwezekana sasa Jiji la Dar es Salaam na kushirikiana na LAPF lifanye mkakati ili kuhakikisha kwamba wenye zile nyumba za jirani wanalipwa fidia ili ni kuongeza kituo. Vilevile wameenda mbali zaidi kwa kusema kwamba kwa uzoefu uliokuwepo maeneo mbalimbali yanapojengwa vituo ili watu watu wakatishe inabidi kutengeneza madaraja ya juu.
Mheshimiwa Spika, Wajumbe wakapendekeza hata ikiwezekana kujengwe tunnel kupitia katika kituo Mbezi cha zamani, kwa hiyo ilikuwa ni ushauri mbalimbali. Hata hivyo jambo hili linaitaji fedha nyingi sana, na kuhusu suala la fedha tunafahamu, wasitani wa shilingi bilioni 28 si jambo dogo; ndiyo maana kuna kitu negotiation kilifanyika kati ya Jiji na wenzetu wa LAPF na jambo hili bahati nzuri tulivyokwenda site siku ile watu wote walikuwepo pale site ili kukubaliana nini kifanyike. Yote hii ni kwa sababu LAPF wameonekeana kwamba wameshafanya mambo mazuri ya mfano. Kwa mfano pale Msamvu wamejenga stand ya kisasa. LAPF wamekuwa commited, wamesema kwamba tunataka tutengeneze stand ambayo hapa Dar es Salaam itakuwa ni stand kubwa ambayo ita-accommodate magari mengi zaidi kwa ajili ya eneo lile.
Kwa hiyo suala la lini mradi utaanza naomba nikuhakikishe, kwa sababu LAPF walishakuwa committed katika utoaji wa fedha, kwa sababu Jiji halitoi fedha; isipokuwa wataingia katika ile joint venture business ambayo itafanyika vizuri na kwa bahati nzuri na wewe Mheshimiwa Mnyika utakuwa miongoni mwa wafaidika kwa sababu stand ile nawe itanufaisha kwenye mapato katika Jiji lako la Dar es Salaam.
Mheshimiwa Spika, suala lingine ni kuhusu uvunjaji, kwamba ikiwezekana tutoe tamko hapa ili suala hili lisitishwe. Mimi niseme kwamba Serikali imesikia hiyo concern yako basi kama Serikali itaangalia nini kifanyike kwa ajili ya maslahi mapana kwa ajili ya Dar es Salaam lakini pia kwa wakazi wa Tanzania. Hata hivyo tumependekeza kwamba wataalam wetu wa detailed design waangalie vya kutosha ili ikiwezekana zile barabara ziweze kusogea mpaka hapa Mbezi Luis Mwisho; kwa sababu hata tukijenga ile stand kubwa pale bila kuitanua ile barabara vya kutosha bado tutakuwa na changamoto kubwa sana kwa sababu magari yatazidi kufungana.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo mambo haya yote kama Serikali inayachukua kwa maslahi mapana kwa mustakabali wa nchini yetu ili kukuza uchumi wetu na wananchi waweze kusafiri vizuri.