Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 7 | Sitting 19 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa | 157 | 2017-05-08 |
Name
Saed Ahmed Kubenea
Sex
Male
Party
CHADEMA
Constituent
Ubungo
Primary Question
MHE. JOHN J. MNYIKA (k.n.y MHE. SAED A. KUBENEA) aliuliza:-
Serikali iliahidi kuhamisha Kituo cha Mabasi cha Ubungo na kukipeleka eneo la Mbezi katika Jimbo la Kibamba lakini mpaka sasa jambo hilo halijatelekezwa.
(a) Je, Serikali imefikia hatua gani ktaika kutekeleza ahadi hiyo?
(b) Je, mradi wa kuhamisha Kituo cha Mabasi unatarajiwa kutumia kiasi gani cha fedha?
Name
Selemani Said Jafo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kisarawe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Rais-TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saed Ahmed Kubenea, Mbunge wa Ubungo lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, hadi sasa tayari Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kushirikiana na mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Serikali za Mitaa (LAPF) umeanzisha kampuni ya ubia ya Mzizima Properties Limited ambayo itahusikana usimamizi na uendeshaji wa shughuli za kituo za kila siku. Kazi inayoendelea ni kutafuta Mtaalam Mshauri kwa ajili ya kuthibitisha usanifu wa mwisho wa kina wa mradi ili kumpata mkandarasi wa ujenzi wa mradi.
Mheshimiwa Spika, gharama za ujenzi wa kituo kikuu cha mabasi cha Mbezi Luis zinakadiriwa kuwa shilingi bilioni 28.71 zitakazotolewa kwa ushirikiano wa Halmashauri ya Jiji na LAPF. Gharama halisi zitajulikana baada ya usanifu wa kina (detailed design) utakapofanywa na Mtaalam Mshauri.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved