Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Primary Question

MHE. JULIUS K. LAIZER (K.n.y MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL) aliuliza:- Wilaya ya Siha ina changamoto ya upungufu wa ardhi jambo ambalo limesababisha wananchi kushindwa kuendesha shughuli zao za kiuchumi kwa ufanisi na pia kuendeleza makazi yao katika maeneo hatarish. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwagawia wananchi mashamba yaliyoko chini ya Hazina kama vile mashamba ya Foster, Journey’s End na Harlington ili wananchi wayatumie kwa kilimo ikizingatiwa kuwa wananchi Kata ya Nchimeta Ngarenairobi wanaishi kwenye maporomoko hatarishi hasa wakati wa mvua na majanga ya moto? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga ardhi kwa ajili ya ufugaji kwa wananchi wa Siha ambao kwa sasa hawana maeneo ya malisho kwa mifugo yao?

Supplementary Question 1

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa jambo hili sasa limechukua muda mrefu tangu 2007 mpaka sasa ni zaidi ya miaka kumi na wananchi wa Enduimet na Ngarenairobi wameendelea kupata matatizo ya ardhi na maeneo ya kujenga.
Je, ni lini Serikali itakamilisha mchakato huo na kuyagawa mashamba hayo kwa wananchi hao? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa jambo hili
la ardhi pia limefanana na maeneo mengine ya Monduli na kwa kuwa Serikali iliyafuta mashamba 13 mwaka 2015 na mashamba hayo mpaka sasa pamoja na mapendekezo ya wananchi bado hayajagawanywa.
Je, ni nini kauli ya Serikali katika kuyagawa mashamba haya, iko katika mazingira gani ili wananchi waweze kunufaika nayo?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la nyongeza lililoulizwa na Mbunge wa Monduli, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Waziri, ni wazi Monduli kuna mashamba mengi ambayo wameleta kwa ajili ya kufutwa na yaweze kupata umiliki mwingine, lakini mpaka sasa mashamba mengi bado yapo kwenye mchakato; zile hatua za awali zimeshafanyika lakini mpaka yaweze kugawiwa ni pale ambapo umiliki wake utakuwa umeshafutwa rasmi na kuweza kuwarejeshea ili wao waweze kupanga tena matumizi kwa ajili ya wananchi wao au kwa ajili ya uwekezaji. Kwa hiyo, hatua hiyo itakapokuwa imekamilika, watapewa na watafanya zoezi la kugawa upya kama ambavyo waliomba toka awali.

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. JULIUS K. LAIZER (K.n.y MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL) aliuliza:- Wilaya ya Siha ina changamoto ya upungufu wa ardhi jambo ambalo limesababisha wananchi kushindwa kuendesha shughuli zao za kiuchumi kwa ufanisi na pia kuendeleza makazi yao katika maeneo hatarish. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwagawia wananchi mashamba yaliyoko chini ya Hazina kama vile mashamba ya Foster, Journey’s End na Harlington ili wananchi wayatumie kwa kilimo ikizingatiwa kuwa wananchi Kata ya Nchimeta Ngarenairobi wanaishi kwenye maporomoko hatarishi hasa wakati wa mvua na majanga ya moto? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga ardhi kwa ajili ya ufugaji kwa wananchi wa Siha ambao kwa sasa hawana maeneo ya malisho kwa mifugo yao?

Supplementary Question 2

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Na mimi nilitaka kumwuliza Mheshimiwa Waziri, ni lini Serikali itakuja kutatua mgogoro wa wananchi katika Kata ya Kakese katika shamba la Benki ya NBC? Shamba hili lilikuwa la uwekezaji lakini mpaka sasa shamba lile lipo limekaa dormant na wananchi hawakuweza kuendelea kulima shamba lile na shamba lile bado lina mgogoro.
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri haoni kwamba
ule ni upotevu wa malighafi na wananchi wanashindwa kuendelea kuendeleza lile shamba ili waendelee kujipatia kipato?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Rhoda Kunchela, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, nitoe ufafanuzi tu kwamba migogoro yote kwa ngazi tofauti siyo kwamba lazima itatuliwe na ngazi ya Wizara. Migogoro mingi na hasa ya kwenye kata na vijiji inatatuliwa na mamlaka zilizoko kule ikiwemo Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, kuna Ofisi ya Kanda ya Ardhi katika maeneo yale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu amesema mgogoro huu uko kwenye ngazi ya Kata, naomba tu Mkuu wa Wilaya wa eneo husika pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri husika waende kwenye Kata yenye mgogoro waweze kutatua mgogoro ule na wananchi waweze kupewa haki yao kama wanastahili kwa sababu amesema lilikuwa linamilikiwa na NBC, lakini siyo kila mgogoro lazima uje Wizarani.
Waheshimiwa Wabunge, nawaomba sana, migogoro mingi wakati mwingine hata tunapokwenda kufanya ziara, unakuta ni mgogoro ambao ungeweza kumalizwa na Mkuu wa Wilaya pale au Mkuu wa Mkoa au Mkurugenzi mwenyewe husika katika eneo lile. Ukienda pale unakuta wewe unakuwa kama mtazamaji, watu wanamaliza wenyewe.
Mheshimiwa Spika, nashauri tu ile ambayo inahitaji Wizara basi ijulikane na ile inayohudumiwa na Mkoa na Wilaya basi nao wachukue nafasi yao kuhakikisha kwamba wanatatua migogoro hii na isiwe ni kikwazo kwa wananachi.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. JULIUS K. LAIZER (K.n.y MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL) aliuliza:- Wilaya ya Siha ina changamoto ya upungufu wa ardhi jambo ambalo limesababisha wananchi kushindwa kuendesha shughuli zao za kiuchumi kwa ufanisi na pia kuendeleza makazi yao katika maeneo hatarish. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwagawia wananchi mashamba yaliyoko chini ya Hazina kama vile mashamba ya Foster, Journey’s End na Harlington ili wananchi wayatumie kwa kilimo ikizingatiwa kuwa wananchi Kata ya Nchimeta Ngarenairobi wanaishi kwenye maporomoko hatarishi hasa wakati wa mvua na majanga ya moto? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga ardhi kwa ajili ya ufugaji kwa wananchi wa Siha ambao kwa sasa hawana maeneo ya malisho kwa mifugo yao?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Hanang kama ilivyo Wilaya ya Siha inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa Ardhi na tuna mashamba ambayo yalikuwa chini ya NAFCO ikiwemo Basotu Plantation na tuliomba kwamba shamba hili lirudi kwa wananchi; Mheshimiwa Waziri anaweza kutueleza ombi letu limefika wapi?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mary Nagu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kwamba kuna maombi ya Shamba la Basotu Plantation ambalo lilikuwepo mikononi mwa NAFCO liweze kugaiwa kwa wananchi. Utaratibu ambao ulikuja kubadilika baadaye ni kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Hanang’ ikabidhiwe hilo shamba ili wenyewe waweze kukodisha kwa wakulima wadogo, kwa sababu tayari jitihada za kugawa mashamba mengine ililileta mgogoro mkubwa sana ambao ulikuwa unatishia amani.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwa sasa utaratibu ambao umetumika ni huo wa kujaribu kukabidhi kwa Halmashauri huku jitihada zikiendelea za kuangalia namna bora ya kuweza kuligawa. Kwa hiyo, namtaka Mheshimiwa Mbunge aendelee kuwa mvumilivu tukiangalia utaratibu huu ili huko mbele ya safari tuweze kuligawa kwa utaratibu.