Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 15 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 126 2017-05-02

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Primary Question

MHE. JULIUS K. LAIZER (K.n.y MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL) aliuliza:-
Wilaya ya Siha ina changamoto ya upungufu wa ardhi jambo ambalo limesababisha wananchi kushindwa kuendesha shughuli zao za kiuchumi kwa ufanisi na pia kuendeleza makazi yao katika maeneo hatarish.
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwagawia wananchi mashamba yaliyoko chini ya Hazina kama vile mashamba ya Foster, Journey’s End na Harlington ili wananchi wayatumie kwa kilimo ikizingatiwa kuwa wananchi Kata ya Nchimeta Ngarenairobi wanaishi kwenye maporomoko hatarishi hasa wakati wa mvua na majanga ya moto?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga ardhi
kwa ajili ya ufugaji kwa wananchi wa Siha ambao kwa sasa hawana maeneo ya malisho kwa mifugo yao?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Godwin Oloyce Mollel, Mbunge wa Siha, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, mwaka 2007 Serikali ilitoa maelekezo ya kusitisha uuzaji wa mashamba ambayo yalikuwa hayajabinafsishwa yakiwemo mashamba ya Forester, Journey’s End, Harlington na Kanamodo yaliyopo NAFCO, West Kilimanjaro. Serikali ilisitisha zoezi la uuzaji wa mashamba hayo baada ya wananchi wa Siha pamoja na Uongozi wa Wilaya na Mkoa kupinga zoezi la ubinafsishaji wa mashamba na kupendekeza mashamba hayo yagawiwe kwa wananchi. Serikali ilikubaliana na maoni ya wananchi na hivyo kumtafuta Mtaalam Mwelekezi kufanya utafiti na matumizi bora ya mashamba hayo.
Mheshimiwa Spika, tathmini ilifanyika na mapendekezo yalikuwa kama ifuatavyo:-
(i) Kuyagawa mashamba hayo katika mashamba madogo madogo kwa ajili ya shughuli za kilimo cha mazao na ufugaji kwa wakulima wadogo na wa kati na kisha kuyauza kwa njia ya zabuni; na
(ii) Baadhi ya maeneo kukabidhiwa kwa Halmashauri
ya Wilaya ya Siha kwa shughuli za maendeleo ikiwemo makazi, shule, vyuo, hospitali na magereza.
Mheshimiwa Spika, kwa kutilia maanani mapendekezo ya mtaalam mwelekezi, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ilielekezwa kuandaa Waraka wa Baraza la Mawaziri wenye mapendekezo ya namna bora ya matumizi ya mashamba hayo. Waraka huo ulishawasilishwa na kufikia ngazi ya Makatibu Wakuu na kutolewa maoni kwa ajili ya marekebisho.
Mheshimiwa Spika, baada ya kukamilisha marekebisho, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi itauwasilisha waraka huo kwenye Baraza la Mawaziri. Baada ya kujiridhisha na mapendekezo na ushauri, Serikali itatoa uamuzi kuhusu matumizi ya mashamba husika.
(c) Mheshimiwa Spika, Serikali imetoa maelekezo kwa Halmashauri zote nchini kukamilisha mpango wa matumizi bora ya ardhi.
Waheshimiwa Wabunge, sisi ni sehemu ya Baraza la Madiwani katika maeneo yetu, hivyo tunapaswa kusimamia maelekezo ya Serikali ili kuhakikisha kuwa wafugaji na wakulima wanatengewa maeneo yao. Tuhakikishe kila kundi linatengewa maeneo kwa ajili ya shughuli zao za kiuchumi. Hapo tutakuwa tumeandaa msingi bora wa maendeleo ya kiuchumi kwa watu wetu.