Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:- Tatizo la makazi duni kwa wananchi husababisha afya mbovu na hivyo kupunguza nguvu ya uzalishaji. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kuwa wananchi wanapata makazi bora?

Supplementary Question 1

MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Wizara inatambua kwamba makazi duni huchangia katika kuleta afya mbovu kwa wananchi. Ni lini sasa Serikali itatekeleza ahadi yake ya kupunguza kodi kwenye vifaa vya ujenzi ili sasa wananchi waweze kujenga nyumba bora na kuepukana na nyumba za tembe na nyasi?
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, Sheria ya Madini
ya Mwaka 2010 inaongelea suala la resettlement; kwa wananchi wanaotokana na maeneo ambayo yana shughuli nyingi za wawekezaji, wakilipwa fidia hulipwa pesa na kuondoka, Sheria ya Madini ya mwaka 2010 inazungumzia kwamba ahamishwe na ahakikishe kama alikuwa na mwembe, basi ataachana naye pale ambapo mwembe utakuwa umeota na kuanza kuzaa. Ni lini sasa Serikali italeta ndani ya Bunge hili mabadiliko ili Bunge liweze kufanya mabadiliko katika Sheria ya Ardhi ili sasa hilo suala la resettlement liweze pia kuzungumziwa katika Sheria ya Ardhi ili wananchi wapate fidia ambayo ni sahihi na waweze kunufaika na uwekezaji huu ndani ya nchi yetu? Ahsante.(Makofi)

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, swali la kwanza amezungumzia hali duni ya makazi ya watu na kufanya pengine wasiwe na makazi bora, pengine yanachangiwa labda na vifaa kuwa na bei ya juu.
Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba suala la kupunguza kodi katika vifaa vya ujenzi ni suala ambalo linahitaji kupitiwa kwa upya katika utaratibu wake kwa sababu mwanzo Waheshimiwa Wabunge walileta suala la kutaka kupunga VAT katika vifaa vya ujenzi, lakini lilikuwa limelenga eneo moja. Katika kulitafakari ikaonekana kwamba ukishatoa loophole hiyo kwa sehemu moja; na ilikuwa imeongelewa upande wa National Housing, pengine lingeweza kuleta tatizo zaidi, watu wangetumia fursa hiyo vibaya.
Mheshimiwa Spika, tunachopendekeza pengine na kuona kwamba kina unafuu zaidi, ni pale ambapo tunaweza kutumia rasilimali tulizonazo katika maeneo yetu na hasa katika kutumia hivi vifaa vya ujenzi ambavyo vinaletwa kwa karibu zaidi. Sasa hivi ukiangalia hata cement imeshuka bei kulingana na uzalishaji umekuwa mkubwa. Kadri ambavyo uzalishaji unakuwa mkubwa, ndivyo jinsi na bei inashuka.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hapa tunachohimiza ni
ile sera ya viwanda; pale ambapo tutawezesha kuwa na viwanda vingi vitakavyoweza kutengeneza vifaa vya ujenzi bei zitashuka tu kwa sababu gharama zitakuwa zimepungua na viwanda vingi vitakuwa katika maeneo ambayo usafirishaji wa vifaa vyake utakuwa ni chini. Kwa hiyo, huwezi kusema tu kwamba utapunguza hili kwa sababu watu wengine watatumia fursa hii vibaya na tusingependa itumike hivyo.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunalipokea kama ni changamoto lakini pia tunahimiza kutumia rasilimali zilizopo katika maeneo yale ambapo pia ujenzi wa nyumba umeonekana kuwa ni nafuu zaidi.
Mheshimiwa Spika, hata ukiangalia katika ile Bodi ya Wakala wa Ujenzi wa Gharama Nafuu wa Nyumba ambayo iko kwenye Wizara yetu, wanatengeneza nyumba na vifaa vya ujenzi wanaandaa pale wanatengeneza, nyumba zake zinakuwa na gharama ya chini zaidi ukilinganisha na hali halisi.
Mheshimiwa Spika, swali la pili ameongelea habari
ya Sheria ya Madini kwamba unapotaka kufanya resettlement kwa watu, anatakiwa afanyiwe malipo stahiki na pia kuandaliwa makazi kwa maana ya kuwezeshwa kupata makazi mengine. Suala hili kisheria lipo isipokuwa katika utekelezaji ndiyo unakuwa kidogo haupo vizuri. Hili tumesema kwamba Serikali tutalisimamia kwa sababu ni wengi wanaoonewa katika hali hiyo.
Mheshimiwa Spika, unakuta kwamba unamuondoa katika makazi yake, unamlipa pengine stahiki yake ya fidia, lakini hukamilishi lile linalotakiwa kwamba umlipe fidia yake na bado pia aweze kupata resettlement mahali pengine. Hili tunalisisitiza kwamba lazima unapomwondoa mtu apate kiwanja aweze kujenga katika maeneo mengine, kwa sababu unalitumia eneo lile kwa uzalishaji.

Name

Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Primary Question

MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:- Tatizo la makazi duni kwa wananchi husababisha afya mbovu na hivyo kupunguza nguvu ya uzalishaji. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kuwa wananchi wanapata makazi bora?

Supplementary Question 2

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tatizo kubwa ni kwamba Halmashauri zetu hazina uwezo wa kutosha wa kupima maeneo yao ili kugawa viwanja na hivyo kuwepo na makazi bora, Serikali sasa ina mpango gani mahususi wa kutoa fungu maalum kwa ajili ya Halmashauri iwe kama revolving fund, wakishapima maeneo waweze kuyauza then warudishe ile fedha na hivyo kuhamishiwa kwenye Halmashauri nyingine ili Halmashauri zote hapa nchini ziweze kupima maeneo yao na hivyo kuwa na makazi bora kwa wananchi wetu? Ahsante.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, suala alilolizungumza Mheshimiwa Sakaya, ni kweli, Halmashauri nyingi hazina uwezo wa kufanya kazi hiyo, lakini ndani ya Wizara tulikuwa tumeanzisha mfuko huu kwa ajili ya kuwezesha Halmashauri mbalimbali kuweza kupima na kuuza viwanja na baadaye kurejesha madeni yao.
Mheshimiwa Spika, lakini kumekuwa na mfano mbaya ambapo Halmashauri nyingi hazirejeshi na mpaka sasa tunadai zaidi ya Halmashauri saba ambazo zimechukua na hazijarejesha na wengine wamerejesha kiasi, na ninadhani kama Mjumbe pia anayo taarifa, tulishawasilisha wale ambao wanadaiwa.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tusingependa pia kuendeleza kuwa na madeni haya na ndiyo maana Serikali inahimiza makusanyo ya ndani ya Halmashauri zenyewe zinazohusika. Pia wanayo fursa ya kupata mikopo kutoka katika mabenki mbalimbali ambayo yanaweza kutumika katika zoezi hilo. Ndiyo maana pia tumeruhusu wataalam mbalimbali wa kutoka kwenye private sector kufanya zoezi hilo la upimaji. Katika kupima, siyo lazima ulipe cash, kuna ile barter trade tunayosema wanaweza wakafanya.
Kwa hiyo, kuna maeneo mengine ambayo wameshaanza; ukiangalia Mkoa wa Katavi, kuna maeneo mengi wanafanya kwa kukubaliana mpimaji na Halmashauri, wanaachiana asilimia kadhaa, hawalipi cash isipokuwa vile viwanja anavyopima anauza anapata hela yake na Halmashauri inaachiwa vingine kwa ajili ya kuweza kutengeneza miundombinu.
Mheshimiwa Spika, hata yule mmiliki wa kiwanja, kama ana kiwanja kikubwa kimetoa viwanja labda vitano, wanakubaliana asilimia kadhaa; anaachiwa viwanja vyake vingine wanachukua Halmashauri wanauza wanatengeneza miundombinu.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, siyo lazima kuwe na cash, ni namna ambayo unaweza ukaifanya na hasa kwa maeneo ya vijijini. Kwa mijini inaweza ikawa ngumu kidogo, lakini vijijini inawezekana kwa kufanya barter trade na bado zoezi la upimaji likafanyika vizuri.