Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye Kata za Ifumbo, Lualaje, Mafyeko na Kambikatoto katika Wilaya ya Chunya?

Supplementary Question 1

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri ambayo nimeridhika nayo, bado nina maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa REA Awamu ya Kwanza, jimbo langu lilibahatika kupata umeme kwenye vijiji tano au sita na kwa kuwa mradi huu wa Awamu ya Kwanza haukuwa na kipengele cha kuweka umeme kwenye majengo ya huduma za jamii kama shule na vituo vya afya. Baada ya kuona hivyo ilibidi Mbunge nije hapa Bungeni nikope fedha kama shilingi milioni 150 ili nikalipe TANESCO waweke umeme kwenye sekondari saba; na kwa kuwa REA Awamu ya Pili nimepata vijiji vitano, lakini katika Kata ya Mtanila umeme haujaend kwenye Kituo cha Afya cha Mtanila. Swali langu sasa, je, hii REA Awamu ya Pili Mheshimiwa Naibu Waziri ananihakikishia majengo ya huduma za jamii kama vituo vya afya na shule yatapata umeme? La kwanza hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa amesema REA Awamu ya Tatu karibu itaanza; je, Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari kwenda na mimi Chunya wakati wa ufunguzi wa mradi huo hasa hasa kuanzia Kata ya Ifumbo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nimpongeze sana Mheshimiwa Mwambalaswa kwa kufuatilia mahitaji na maslahi ya wananchi wake katika Jimbo la Lupa na tunashirikiana naye kwa ukaribu sana hasa katika vijiji na kata ambazo zimebaki.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia nikubali kwamba katika REA Awamu ya Kwanza na ya Pili hatukuchukua maeneo mengi sana na hii ni kwa nchi nzima, siyo katika jimbo la Mheshimiwa. Nimhakikishie Mheshimiwa Mwambalaswa katika kata sita zilizobaki ambazo ameomba zipatiwe umeme ikiwemo Kata za Mtabila, Ifumbo, Itumbi, Kambikatoto pamoja na Matundasi A na B zote zitapelekewa umeme. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kama alivyouliza, REA Awamu ya Tatu majukumu yake ya kimsingi pamoja na mambo mengine ni kusambaza umeme katika taasisi zote za umma kama hospitali, vituo vya afya, zahanati, shule, mitambo ya maji, makanisa, misikiti na sokoni.
Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mwambalaswa na nichukue nafasi hii kuwaomba Waheshimiwa Wabunge wote kwenye Halmashauri zetu tuweze sasa kutenga walau pesa kwa ajili ya kuunganisha umeme kwenye taasisi zetu kwa sababu hili ni jukumu letu sote, na ndiyo maana wakandarasi tunapokwenda kuwakabidhi sasa tunawakabidhi Waheshimiwa Wabunge ili waweze kufuatilia utekelezaji wa miradi hii. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mwambalaswa nakuhakikishia kwamba vituo vya afya na taasisi nyingine zitapelekwa umeme. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili la kufuatana na Mheshimiwa Mwambalaswa, kwanza kabisa niko tayari lakini kabla sijafuatana nawe mkandarasi tumeshamtuma na tumeshazindua utekelezaji wa REA Awamu ya Tatu katika Mkoa wa Mbeya na Songwe. Sasa hivi mkandarasi yuko Ileje na tarehe 15 atafika kwako Mheshimiwa Mwambalaswa. Kwa hiyo, tuko pamoja na niko tayari kufauatana na wewe.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye Kata za Ifumbo, Lualaje, Mafyeko na Kambikatoto katika Wilaya ya Chunya?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwa kuwa Mbulu Vijijini katika REA Awamu ya Pili tumepata vijiji viwili tu na sasa Mbulu Vijijini hatuna sub-station tunapata umeme kutoka Katesh na Mheshimiwa Waziri anafahamu, amekuja, tunapata kutoka Babati na Mbulu Mjini. Je, mtatuhakikishiaje sasa katika awamu hii REA itafika maeneo yote ya kata na hasa katika vijiji vya mwanzo vya Mbulu Vijijini?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa Mheshimiwa Flatei nakupongeza, mwaka jana mwezi Novemba tulitembea na wewe kwenye jimbo lako lote na ukanionesha vijiji vyako vyote 78 ambavyo havijapata umeme pamoja na vijiji vya karibu kabisa na Wilaya za jirani. Hata hivyo, natambua katika utekelezaji wa REA Awamu ya Tatu kazi zinazofanyika ni pamoja na kufunga transfoma. Kinachokosekana katika Jimbo lako Mheshimiwa Flatei ni ufungaji wa transfoma katika vijiji ambavyo umevitaja ikiwa ni pamoja na Katesh.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Flatei kazi ambayo itafanyika sasa ni kukupelekea umeme katika vijiji vyako 78 vilivyobaki pamoja na vitongoji 120 kama ambavyo umeomba. Kwa hiyo, niwahakikishie wananchi wa Mbulu Vijijini kwamba wote watafikiwa na umeme vijijini, vitongojini pamoja na kwenye taasisi zako za umma.

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye Kata za Ifumbo, Lualaje, Mafyeko na Kambikatoto katika Wilaya ya Chunya?

Supplementary Question 3

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza kwenye Wizara ya Nishati na Madini. Wilaya ya Chemba ni miongoni mwa Wilaya mpya na upatikanaji wa huduma ya nishati kwa maana ya umeme ni kwa vijiji 60 tu kati ya vijiji 112. Nataka kufahamu ni lini sasa kwa REA Awamu ya Tatu itakwenda kukamilisha vijiji hivi 52 vilivyobaki ili Wilaya yetu na wananchi wale waweze kupata huduma hii ya umeme wa REA Awamu ya Tatu? Nashukuru.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa katika Jimbo la Chemba tulipeleka umeme katika vijiji 62 na vikabaki vijiji 52; kwa hiyo viko 124. Niseme tu vijiji 52 vilivyobaki tumeshazindua katika maeneo ya Chemba na Wilaya zote, Mkoa wa Dodoma na tunaelekea katika Mikoa ya Singida na mingine. Upelekaji wa umeme katika REA Awamu ya Tatu umeanza tangu mwezi Machi na utakamilika kwa nchi nzima ikiwemo pamoja na Jimbo la Chemba mwaka 2020. Mradi huu unakwenda kwa awamu, baadhi ya vijiji na vitongoji vitakamilika mwezi Machi, 2019 na baadhi yake kwenye densification ni miezi 15 kuanzia sasa. Kwa hiyo, vijiji vyote 52 kati yake vijiji 12 vitapatiwa umeme 2019 na vilivyobaki vya Chemba mwaka 2020.