Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 14 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 112 2017-04-28

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye Kata za Ifumbo, Lualaje, Mafyeko na Kambikatoto katika Wilaya ya Chunya?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Victor Kilasile Mwambalaswa, Mbunge wa Lupa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Usambazaji Umeme Vijijini Awamu ya Tatu umeanza rasmi nchi nzima tangu mwezi Machi, 2017. Mradi huu utajumuisha vipengele-mradi vitatu vya densification, grid extension pamoja na off grid renewable ambapo inalenga kuongeza wingi wa usambazaji umeme kwenye vijiji ambavyo vimefikiwa na umeme lakini kwenye vitongoji havijaunganishwa. Kata za Ifumbo, Kambikatoto, Lualaje na Mafyeko zimejumuishwa katika mradi wa REA Awamu ya Tatu wa grid extension ambao utaanza na kukamilika mwaka 2020/2021.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya kupeleka umeme katika kata hizo itajumuisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 20, ujenzi wa njia ya umeme ya msongo ya kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 76, ufungaji wa transfoma kumi pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 1,145. Gharama ya kazi hii ni shilingi bilioni 3.142.