Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Joel Makanyaga Mwaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chilonwa

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA Aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia maji wananchi wa vijiji vya Jimbo la Chilonwa?

Supplementary Question 1

MHE. JOEL M. MAKANYAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, lakini niweke wazi tu kwamba vijiji vilivyofaidika mpaka sasa ni vijiji vitatu ambavyo ukilinganisha na jumla ya vijiji 47 vya Jimbo langu ni sawa na asilimia 6.4. Kuna vijiji kama 12 hivi vilikuwa na huduma hii ya maji kabla, vinakuwa vijiji 15 vinavyofaidika ambavyo ni sawa sawa na asilimia 31.9.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu Tanzania tunakimbilia kwenye Tanzania ya Viwanda. Tanzania inayotaka wananchi wafanye kazi kwa bidii, kwa nguvu bila maji, tukijua kwamba, maji ni muhimu katika maisha ya binadamu, tusipopata maji safi na salama uwezekano wa kuwa na magonjwa ya hapa na pale yatakayotufanya tushindwe kufanya kazi inayostahili na kwa hiyo, tushindwe kuipeleka Tanzania katika Tanzania ya Viwanda.
Je, Serikali ina mpango gani kuongeza kasi ya
upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi wa Jimbo la Chilonwa?
Swali la pili, je, Serikali haioni kwamba kuna umuhimu sasa siyo lazima kila kijiji kichimbiwe kisima chake au kiwe na chanzo chake, wakati mwingine chanzo kimoja kiweze kuhudumia hata vijiji viwili/vitatu. Serikali haioni kwamba kuna umuhimu wa kufanya hivyo? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu concern ya Mheshimiwa Mbunge ndiyo maana tukiangalia eneo la Wilaya ya Chamwino liko karibu katika Makao Makuu sasa ya nchi yetu. Mheshimiwa Mbunge ndiyo maana unafahamu takribani zipatato wiki Nne nilikuwa katika mradi wa maji wa Wihunze ambao nimeona kwamba Mkandarasi anafanya kazi kwa kusuasua na kutoa maagizo ikifika tarehe Tatu mwezi huu tulioanza nao mradi huo uweze kukamilika na ninasikia hali kidogo inaenda vizuri. Hiyo yote ni juhudi ya Serikali kuangalia jinsi gani tutafanya miradi hiyo ipatikane.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hali hiyo, ndiyo
maana hapa nimezungumza katika majibu yangu ya awali kwamba, mwaka huu tumetenga shilingi bilioni 1.058 kwa ajili ya kupeleka juhudi hii ya maji, hata hivyo naomba nikuhakikishie kwa sababu, eneo la Wilaya ya Chamwino hasa Jimbo lako ni eneo la kimkakati na Ikulu yetu ya Mheshimiwa Rais ndiyo inapojengwa pale. Naomba nikuhakikishie kwamba Serikali itafanya kila liwezekanalo kuhakikisha wananchi wa maeneo yale wanapata huduma ya maji kwa sababu, ndiyo sehemu ambayo ni pumulio la katikati la Jiji la Dodoma, lazima tuweke juhudi za kutosha. Naomba ondoa hofu, Serikali itakuwa na wewe daima kuhakikisha kwamba mambo yanakuwa vizuri katika Jimbo lako.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA Aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia maji wananchi wa vijiji vya Jimbo la Chilonwa?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Wananchi wa Tarafa ya Mikese, Wilayani Morogoro Vijijini, wameahidiwa muda mrefu mradi wa maji, lakini mpaka sasa wanapata taabu sana kwa kupata maji.
Je, ni lini wananchi wa Mikese watapata maji kusudi waondokane na tatizo hilo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niweke kumbukumbu sawa. Mheshimiwa Mama Ishengoma alikuwa
miongoni mwa Wajumbe wa Kamati ya Maji katika Bunge la Kumi na mimi tulikuwa katika Kamati moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri wakati ule Profesa Mark Mwandosya akiwa Waziri wetu wa Maji wa kwanza alikuwa akizungumzia sana suala zima la Mikese. Nadhani hapa tutakapo-table katika Bajeti ya Wizara ya Maji itakapofika, watazungumza jinsi gani Mfuko wa Maji ambao
mwaka huu tunatenga fedha kidogo za kutosha utagusa katika vijiji mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tusubiri Wizara ya Maji itakapokuja kuweka bajeti yake pale, tutajadili kwa upana zaidi jinsi gani tutawasaidia wananchi wa Mikese ambao najua kwamba kweli wana shida kubwa ya maji, lazima wapate mradi wa maji na ahadi ya siku nyingi.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA Aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia maji wananchi wa vijiji vya Jimbo la Chilonwa?

Supplementary Question 3

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Kwa kuwa tatizo la maji limekuwa ni kero ya nchi nzima, ni kwa nini sasa Serikali, hususan kupitia kwenye bajeti ya Bunge hili, isikubali kutengeneza Wakala wa Maji Vijijini ambaye atasaidia kupeleka maji vijijini kote kama ambavyo tumefanya katika REA ambapo kwenye suala la umeme wameweza kufanikiwa vizuri. Kwa nini wasifanye hivyo ili maji yafike hata kule Momba, Chitete, pamoja na vijiji vingine? Ahsante.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Naibu Spika, Bunge lako Tukufu katika bajeti iliyopita liliagiza Wizara ya Maji ianze taratibu za kuunda Wakala wa Maji nchini, tayari tumeshaanza kazi hiyo na wakati wowote itawasilishwa hapa kwa ajili ya kupewa mjadala na kupitishwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo suala hilo tayari
linafanyiwa kazi.