Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 71 2017-04-19

Name

Eng. Joel Makanyaga Mwaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chilonwa

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA Aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia maji wananchi wa vijiji vya Jimbo la Chilonwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA Alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joel Mwaka Makanyaga, Mbunge wa Chilonwa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Maji nchini, kuanzia mwaka 2012/2013 hadi mwaka 2014/2015 imetekeleza miradi ya maji kwa vijiji vya Itiso na Membe kwa jumla ya shilingi milioni 758.7 vikiwa na jumla ya vituo vya kuchotea maji 23 ambavyo vinahudumia wakazi wapatao 7,475.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2016/2017 Halmashauri inakamilisha mradi wa maji katika kijiji cha Wilunze ambao utahudumia jumla ya watu 2,867 kwa maeneo ya Makaravati, Mbelezungu, Majengo na Chalinze Nyama kwa jumla ya shilingi milioni 347.9 katika Jimbo la Chilonwa.
Aidha, katika mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri imepanga kutumia shilingi bilioni 1.053 kwa ajili ya kujenga miradi ya maji ikiwa ni pamoja na vijiji vya Magungu na Segala katika Jimbo la Chilonwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuboresha huduma ya maji katika Jimbo la Chilonwa na maeneo mengine nchini kwa kadri rasilimali fedha itakavyopatikana.