Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. JORAM I. HONGOLI aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ilianzishwa mwaka 1982, lakini mpaka leo hii haina Hospitali ya Wilaya na ina Vituo vitatu vya Afya:- (a) Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya? (b) Je, ni lini Serikali itatoa fedha za kuviwezesha Vituo hivi vya Afya kutoa huduma ndogo ya upasuaji ili kupunguza vifo vya akinamama na watoto pamoja na wananchi wengine?

Supplementary Question 1

MHE. JORAM I. HONGOLI: Ahsante sana Mheshimiwa Spika. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, naomba niulize swali moja la nyongeza. Kwa kuwa sasa tutakuwa na huduma ya upasuaji mdogo katika Kituo cha Afya Lupembe na hatimaye Kichiwa ili kuboresha huduma ya madawa kwa kuwa dawa ni tatizo: Je, Serikali ina mpango gani wa kufungua duka la dawa kwa maana ya MSD katika Kituo cha Afya Lupembe na baadaye Kichiwa? Ahsante sana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza lazima nikiri kwamba harakati za Mbunge huyu na watu wa Mkoa wa Njombe kwa ujumla wake tutajitahidi kuziunga mkono. Lengo kubwa ni Mkoa mpya wa Njombe uweze kupata huduma ya afya. Ndiyo maana hata Waziri wangu Mkuu juzi juzi alikuwepo kule kwa ajili ya mipango ya kimkakati katika Mkoa ule mpya.
Mheshimiwa Spika, suala zima la ujenzi wa duka la madawa katika vituo hivyo, siwezi kukiri kwamba katika hivyo Vituo vya Afya tutafanyaje, lakini kwa sababu pale tuna hospitali yetu ya Rufaa ya Mkoa ambayo inajengwa sasa hivi, tutafanya mpango mkakati tufanyeje katika eneo lile tupate duka maalum la MSD. Nia ya Serikali ni watu wa ukanda ule waweze kupata dawa kwa ukaribu zaidi.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, naomba niwahimize Waheshimiwa Wabunge wote, kwa sababu sasa hivi tunaelekeza fedha nyingi sana katika Halmashauri na nashukuru sana, juzi juzi karibu kila Mbunge hapa amepata orodha ya idadi ya fedha kwa ajili ya madawa katika eneo lake, sasa ni kuona jinsi gani twende tukazisimamie.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, nilisema katika siku za nyuma kwamba, tumeelekeza fedha nyingi za basket fund ambazo fedha zile lengo lake ni kwamba one third nikwa ajili ya ununuzi wa madawa na vifaa tiba. Naomba tukasimamie tutatue kero za madawa kwa wananchi wetu, kwa sababu tukifanya hivi, naamini Watanzania wote watafarijika kupata dawa bora katika maeneo yao kwa sababu Serikali sasa hivi imepeleka fedha nyingi sana katika Sekta ya Afya.

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Primary Question

MHE. JORAM I. HONGOLI aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ilianzishwa mwaka 1982, lakini mpaka leo hii haina Hospitali ya Wilaya na ina Vituo vitatu vya Afya:- (a) Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya? (b) Je, ni lini Serikali itatoa fedha za kuviwezesha Vituo hivi vya Afya kutoa huduma ndogo ya upasuaji ili kupunguza vifo vya akinamama na watoto pamoja na wananchi wengine?

Supplementary Question 2

MHE. DOTO M. BITEKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi hii. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa wepesi wake katika kutatua changamoto tulizonazo kwenye Halmashauri zetu.
Mheshimiwa Spika, chumba cha upasuaji cha Hospitali ya Wilaya ya Bukombe kilikuwa kimejengwa kwa ajili ya kutumika kwa muda baadaye ijengwe theatre. Mheshimiwa Naibu Waziri wa Afya alikuja pale akaona hali halisi ilivyokuwa. Nataka tu kujua commitment ya Serikali, ni lini wataisaidia Hospitali ya Wilaya ya Bukombe na yenyewe ipate chumba cha upasuaji cha kisasa kwa ajili ya kuwapatia huduma wananchi wa Bukombe?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza nikiri wazi kwamba nilifika Jimboni kwa Mheshimiwa Mbunge na ni kweli nimeenda kuitembelea hospitali yetu ya Wilaya angalau pale upasuaji unaendelea. Kwa kuwa eneo lile lina changamoto kubwa sana, ndiyo maana tuna mpango vile vile siyo kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ile peke yake, isipokuwa hata katika Kituo chako cha Afya cha Uyovu kama tulivyoongea.
Mheshimiwa Spika, tutaangalia jinsi gani tutafanya ili tupeleke huduma katika maeneo yale, tupate na back up strategy katika Kituo cha Afya cha Uyovu, tupunguze idadi kubwa ya wagonjwa ambao wataendelea katika Hospitali yetu ya Wilaya. (Makofi)
Kwa hiyo, amini Serikali yako kwa sababu tumekuja kule, tumefanya survey, tumetembelea, tumekutana na wananchi, tumebaini changamoto. Baada ya kubaini changamoto, Serikali tunapanga mkakati wa kuweza kuwasaidia wananchi wa Bukombe.