Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 9 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 97 2017-02-09

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. JORAM I. HONGOLI aliuliza:-
Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ilianzishwa mwaka 1982, lakini mpaka leo hii haina Hospitali ya Wilaya na ina Vituo vitatu vya Afya:-
(a) Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya?
(b) Je, ni lini Serikali itatoa fedha za kuviwezesha Vituo hivi vya Afya kutoa huduma ndogo ya upasuaji ili kupunguza vifo vya akinamama na watoto pamoja na wananchi wengine?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joram Ismail Hongoli, Mbunge wa Lupembe, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2016/2017, Serikali imetenga shilingi milioni 82.0 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Njombe na itaanza kwa jengo la wagonjwa wa nje, yaani OPD. Fedha hizo bado hazijatolewa kutoka HAZINA.
(b) Mheshimiwa Spika, ukarabati wa chumba cha upasuaji katika Kituo cha Afya cha Lupembe umekamilika kwa gharama ya shilingi milioni 21.0 kutokana na mapato ya ndani ya Halmashauri. Vile vile, katika mwaka wa fedha 2017/2018, Halmashauri imepanga kutumia shilingi milioni 36.0 kwa ajili ya kukarabati chumba cha upasuaji katika Kituo cha Afya cha Kichiwa.