Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: aliuliza:- Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara inakabiliwa na Matatizo mbalimbali kama vile uhaba wa magari ya kubebea wagonjwa, uhaba wa vitanda hasa kwenye wodi za akinamama, uhaba wa dawa na kadhalika:- Je, ni lini Serikali itayashughulikia matatizo hayo ili kuboresha huduma zinazotolewa hospitalini hapo?

Supplementary Question 1

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Majibu ya Naibu Waziri hayajaniridhisha, ukilinganisha na kwamba vifaa tiba na madawa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa havitoshelezi. Je, ni lini atahakikisha Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara itakuwa na vifaa ambavyo vitakuwa vinatosheleza kwa asilimia mia moja? (Makofi)
Swali la pili; kwa kuwa gari lililopo ni moja ambalo lina uhakika wa kubeba mgonjwa mahututi kumtoa Hospitali ya Rufaa Musoma kumpeleka Mwanza na ile nyingine ni hizi gari ndogo: Je, ni lini atatuletea ambulance nyingine katika Hospitali yetu ya Rufaa ya Mkoa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba nikwambie kwamba najua, kwa sababu wakati nakwenda kufunga Mkutano wa ALAT kule Musoma, nilitembelea mpaka Mkoa wa Mara kuona mpango mkakati wa kujenga Hospitali hii ya Rufaa ya Mkoa wa Mara. Nimetembelea pale, nimeona na tumebadilishana mambo mengi sana na Katibu Tawala wa Mkoa ule. Kwa hiyo, najua kuna changamoto, ndiyo maana katika majibu yangu ya msingi nilisema kweli kuna changamoto katika hospitali hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo letu ni nini? Ni kuhakikisha kwamba sasa tunasukuma jambo lile. Naomba tushirikiane na Waheshimiwa Wabunge; kama mnavyojua kwamba commitment za afya zina cross cut maeneo mbalimbali nchini. Kwa hiyo, ni imani yangu kwamba, tutaendelea kushirikiana. Commitment ya Serikali, tukiangalia sasa hivi bajeti ambayo imetoka, shilingi milioni 700 mpaka shilingi bilioni 1.8, ni ongezeko la asilimia 61. Hili ni jambo kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kinachofanyika sasa hivi ni nini? Ni kusaidia kusukuma nguvu sasa ili fedha zipatikane na wananchi wapate huduma. Katika mchanganuo wa bajeti katika eneo hilo, ndiyo unagusa katika maeneo mbalimbali ya vifaa tiba na madawa kuiwezesha hospitali hii iweze kufanya vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo Mheshimiwa Mbunge amezungumzia suala la ambulance; ni kweli. Najua kwamba ambulance moja inafanya kazi vizuri, lakini na hizi nyingine zina changamoto kubwa. Sasa naomba nimsisitize Mheshimiwa Mbunge kwa kushirikiana na wadau wengine mbalimbali, katika mchakato huu wa bajeti unaokuja wa 2017/2018, tuweke kipaumbele kinachojiainisha katika upatikanaji wa ambulance. Serikali haitasita kulisukuma hili. Lengo ni kupata ambulance ya maana katika kusaidia wakati wowote emergency inapotokea, wananchi waweze kupata fursa za tiba. Kwa hiyo, nakubali ombi hilo, tutaenda kulifanyia kazi kwa pamoja kama Wabunge na Serikali.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: aliuliza:- Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara inakabiliwa na Matatizo mbalimbali kama vile uhaba wa magari ya kubebea wagonjwa, uhaba wa vitanda hasa kwenye wodi za akinamama, uhaba wa dawa na kadhalika:- Je, ni lini Serikali itayashughulikia matatizo hayo ili kuboresha huduma zinazotolewa hospitalini hapo?

Supplementary Question 2

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tatizo lililopo kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara, linafanana kabisa na tatizo ambalo lipo kwenye Hospitali ya Mkoa wa Tabora ya Rufaa ya Kitete. Kuna tatizo kubwa sana la wagonjwa na hasa akinamama wanapoenda kujifungua, wodi ile ni ndogo na wengi wanalala chini wakiwa hata wale wachache wanakuwa wana-share kitanda kimoja:-
Je, Serikali inajipanga vipi kutatua hili tatizo la muda mrefu la msongamano wa akinamama wanapojifungua pale Hospitali ya Mkoa wa Tabora ya Kitete?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Hospitali ya Kitete pale Tabora ina changamoto kubwa na ndiyo maana ukifanya rejea ya majibu yangu mbalimbali niliyoyatoa hapa Bungeni, tumesema kwamba catchment area ya Mkoa wa Tabora, ukubwa wake na jiografia yake ilivyo ina kila sababu tuweke nguvu. Ndiyo maana katika bajeti ya mwaka huu sitaki kutaja figure hapa exactly, tuna fungu ambalo tumelitenga kwa ajili ya suala zima la ukarabati pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutaangalia ni kipi kilichotengwa katika mwaka huu. Lengo ni kwamba ile fedha ipatikane tu ikafanye kazi na value for money ionekane. Naamini ule ukarabati utaanza mara moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nikuhakikishie kwamba katika majibu yangu ambayo nayakukumbuka hapa Bungeni niliyoyatoa ni suala zima la Hospitali ya Kitete; naomba tuwasiliane kwa karibu zaidi ili tujue ni fungu kiasi gani limetengwa, lakini tuhimize sasa ile fedha ili iweze kufanya kazi vizuri.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: aliuliza:- Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara inakabiliwa na Matatizo mbalimbali kama vile uhaba wa magari ya kubebea wagonjwa, uhaba wa vitanda hasa kwenye wodi za akinamama, uhaba wa dawa na kadhalika:- Je, ni lini Serikali itayashughulikia matatizo hayo ili kuboresha huduma zinazotolewa hospitalini hapo?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa tatizo la Mara la vifaa tiba pamoja na gari la wagonjwa, ni kama la Rungwe. Napenda kujua commitment ya Serikali kwa Hospitali ya Makandana katika Wilaya ya Rungwe, ni lini watatuletea gari na kutuongezea vifaa tiba kwa ajili ya kuwasaidia wanawake wa Wilaya ya Rungwe katika Hospitali ya Makandana?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikupongeze na niwashukuru sana kwa dua zenu njema. Nakumbuka siku ile nilivyotoka kule baada ya kutoa maagizo kwamba mfumo wa kielectroniki ufanye kazi pale, baada ya muda fulani nikapata ajali, watu wakasema, watu wa huko wamekushughulikia? Nikasema hapana. (Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nishukuru sana. Agizo langu nililotoa ndani ya mwezi mmoja lilitekelezeka katika hospitali ile na nilipata mrejesho kwamba makusanyo yamebadilika sana katika hospitali ile ya Makandana. Kwa hiyo, naomba niseme kwamba kweli nilitembelea pale nikakuta gari za wagonjwa hali yake sio nzuri sana. Tulibadilishana mawazo na bahati nzuri wana Mkuu wa Wilaya mzuri sana katika eneo lao.
Mheshimiwa Naibu Spika, nami naomba nilichukue hili kwa sababu kuna vitu vingine tumeshaanza kuvizungumza kuona ni jinsi gani tutafanya kuboresha hospitali ile, tutajadili kwa pamoja ili hospitali hii iweze kupata huduma nzuri, kwa sababu kuna network nzuri ya Waheshimiwa Wabunge katika eneo hilo, mnaofanya kazi kwa pamoja kwa agenda kubwa ya hospitali yenu, basi naamini jambo hili tutalitatua kwa pamoja, kama mawazo shirikishi kuhusu tufanye nini katika mpango wa muda mfupi na mpango wa muda mrefu.

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: aliuliza:- Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara inakabiliwa na Matatizo mbalimbali kama vile uhaba wa magari ya kubebea wagonjwa, uhaba wa vitanda hasa kwenye wodi za akinamama, uhaba wa dawa na kadhalika:- Je, ni lini Serikali itayashughulikia matatizo hayo ili kuboresha huduma zinazotolewa hospitalini hapo?

Supplementary Question 4

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tatizo lililoko Mara la ambulance ya kuwachukua wagonjwa, ni sawasawa na tatizo lililopo Wilaya ya Kondoa ambako Kituo cha Afya cha Wilaya ya Kondoa hakina ambulance kwa muda mrefu sasa; iliyopo ni mbovu ya mwaka 2008 na inahitaji matengenezo makubwa sana kiasi kwamba Halmashauri haiwezi kumudu. Je, Serikali iko tayari kutuletea ambulance Wilaya ya Kondoa ili wagonjwa ambao wanatakiwa kupata Rufaa ya kuja Dodoma Mjini wapate usafiri?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, tumelisikia suala zima la request katika Wilaya ya Kondoa. Niseme wazi, ukiangalia hata katika database ya mwaka huu, katika Halmashauri ambazo ziliomba kupata ambulance zilikuwa 18, katika kumbukumbu yangu ya karibuni. Hili sina hakika hapa kama tuliweza kuliainisha katika mpango wetu wa bajeti wa Halmashauri ya Kondoa kwa mwaka huu wa fedha, lakini tutaenda kuliangalia. Kama Kondoa haipo, itabidi tujipange kwa pamoja, tuone ni jinsi gani tutafanya katika mchakato wa bajeti ambao utaanza siyo muda mrefu; na mpango wake tumeujadili hapa siyo muda mrefu, tujadili kwa pamoja kwa sababu hii needs assessment inaanzia kutoka katika vikao vyetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, tutakapolifanya hivi na kwa sababu jambo hili ni pana na ninavyojua, mgonjwa kutoka Kondoa mpaka aletwe Hospital ya General hapa Dodoma ambapo ni mbali sana, tuna kila sababu kuwezesha eneo hilo lipate vifaa vizuri hasa ambulance kuwafikisha wagonjwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Felister Bura kwamba, hili tutaliangalia kwa upana wake, tuone ni jinsi gani tutafanya ili eneo lile lipate huduma bora.