Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 8 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 81 2016-11-09

Name

Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: aliuliza:-
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara inakabiliwa na Matatizo mbalimbali kama vile uhaba wa magari ya kubebea wagonjwa, uhaba wa vitanda hasa kwenye wodi za akinamama, uhaba wa dawa na kadhalika:-
Je, ni lini Serikali itayashughulikia matatizo hayo ili kuboresha huduma zinazotolewa hospitalini hapo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joyce Bitta Sokombi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara, inayo magari mawili ya kubebea wagonjwa ambayo ni STK 8368 na STK 7079. Gari namba STK 7079 lilipata ajali, lakini limeshafanyiwa matengenezo kupitia TEMESA Mkoa wa Mwanza ili liendelee kutoa huduma kwa wagonjwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali hiyo ina jumla ya vitanda 240 kati ya 420 vinavyohitajika. Kwa siku inalaza wagonjwa wanaofikia 169 katika wodi tatu za wazazi zilizopo. Mkoa kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo, wamepanga kujenga wodi (Postnatal Ward) ambayo itawezesha kuongeza idadi ya vitanda 20 kukidhi mahitaji ya sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, bajeti ya dawa katika hospitali imeongezeka kutoka shilingi milioni 710 kwa mwaka wa fedha 2015/2016 hadi shilingi bilioni1.8 kwa mwaka wa 2016/2017 sawa na ongezeko la asilimia 61. Mkakati wa Serikali hivi sasa ni kuimarisha makusanyo ya mapato ya huduma kwa njia ya kielektroniki ili kuongeza uwezo wa upatikanaji wa dawa na vifaa tiba katika hospitali zote nchini.