Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Primary Question

MHE. HUSSEIN M. BASHE aliuliza:- Je, ni lini Serikali inakusidia kuanza utekelezaji wa ujenzi wa barabara ya kilometa 10 ndani ya Mji wa Nzega kama ambavyo Mheshimiwa Rais aliahidi wakati wa kampeni?

Supplementary Question 1

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, ninashukuru. Nilitaka kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa shilingi bilioni 5.2 ni sawa sawa na mapato ya ndani ya Halmashauri kwa zaidi ya miaka mitatu, na kwa kuwa Halmashauri ya Mji wa Nzega haina uwezo wa kifedha na ndio ilikuwa mantiki ya kumuomba Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete na baadaye Rais John Pombe Magufuli kwamba miradi hii ya ujenzi wa kilometa 10 iende chini ya TANROADS.
Je, sasa Serikali iko tayari kuwaambia wananchi wa Jimbo la Nzega kwamba miradi hii ya kilometa 10 itajengwa chini ya utaratibu wa TANROADS na si kwa kutumia fedha za Halmashauri ya Mji?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli nafahamu Halmashauri ya Mji wa Nzega mapato yake ni madogo, na Mheshimiwa atakumbuka takribani wiki tatu na nusu au wiki nne tulikuwa wote kule Nzega tukihamasisha shughuli za maendeleo. Nipende kumshukuru sana kwa juhudi kubwa anazozifanya katika Jimbo lake
Mheshimiwa Spika, naomba nikuhakikishieni kwamba hii ni commitment ya Serikali na ahadi ya Mheshimiwa Rais. Katika hivi ukiachia hata huo uchache wa mapato, hata ujenzi wa miundombinu katika maeneo mengine tunayoyafanya hivi sasa si kwamba Halmashauri hizo zinauwezo huo.
Mheshimiwa Spika, si muda mrefu tutaanza mchakato hata katika Mji wa Mpwapwa na maeneo mengine mbalimbali hapa nchini. Naomba nisema wazi Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa makusudi imeamua kubadilisha miundombinu ya Manispaa na Majiji ya maeneo mbalimbali, na ndiyo maana utakuta katika miji mikubwa, Manispaa na Halmashauri za Miji sasa hivi mitandao ya barabara imeimarika.
Mheshimiwa Spika, bahati nzuri Mheshimiwa Bashe amepata fursa kubwa, ambapo Mamlaka ya Mji wake vile vile tayari umesha-qualify sasa kuingizwa katika mipango ya ujenzi wa barabara za lami. Kwa hiyo, naomba nimtoe hofu, Serikali itahakikisha ahadi ya Mheshimiwa Rais inatekelezwa, tunajua mapato yenu ni madogo. Lakini pia ni commitment ya Ofisi ya Rais – TAMISEMI kuhakikisha kwamba miji yote inajengewa barabara za lami. Ondoa hofu Serikali itatekeleza hilo kwa kadiri iwezekanavyo.