Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 7 Works, Transport and Communication Ofisi ya Rais TAMISEMI. 70 2016-11-08

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Primary Question

MHE. HUSSEIN M. BASHE aliuliza:-
Je, ni lini Serikali inakusidia kuanza utekelezaji wa ujenzi wa barabara ya kilometa 10 ndani ya Mji wa Nzega kama ambavyo Mheshimiwa Rais aliahidi wakati wa kampeni?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hussein Mohamed Bashe, Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, hatua za awali za utekelezaji wa ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kujenga kilometa 10 za barabara kwa kiwango cha lami zimeshaanza, ambapo kazi zilizofanyika ni upembuzi yakinifu, usanifu wa kina, kuandaa michoro na makisio ya kazi za ujenzi wa kilometa 10. Mtandao huo wa barabara utajengwa katika Kata ya Nzega Mjini Mashariki, sawa na kilometa tano na Nzega Mjini Magharibi kilometa tano zilizobaki.
Mheshimiwa Spika, gharama za kutekeleza mradi huo ni shilingi bilioni 5.2 ambazo zitahusisha ujenzi wa mitaro ya barabara na makalavati ikiwemo mitaro mikubwa katika eneo la Samora, ujenzi matabaka ya barabara ya changarawe na ujenzi wa mtabaka mawili ya lami nyepesi.
Mheshimiwa Spika, makisio ya gharama hizo yatazingatiwa katika bajeti ya Halmashauri kwa mwaka 2017/2018 kwa ajili ya kuanza utekelezaji kwa awamu.